Resurrection
JF-Expert Member
- Jun 8, 2020
- 952
- 1,267
Nafikiri Busara ikitumika ushenzi utapungua solution ni kumpangia mazingara mazuri kazini na sio kumfukuza ,ukimrudisha mtaani utakuwa hukumsaidia ,kama una imani na Mwenyezi Mungu basi hupotezi kitu bali mapato yako yatazidi .Comments nyingi utapata za lawama utadhani wao malaika. Mtimue atakufilisi huyo hapo kaongeza familia mtoto na baba mtoto. Wazazi hawaachani utajikuta duka lako linalea hio familia. Akiwa jobless akili zitamkaa atajua jinsi ya kubalance malezi ya mwanae na kujali kazi.
Ukiishi kwa huruma utafilisika mkuu
Mzee wa St Kayumba hata mimi kama mzee wa mitishamba nilishaliona hilo ila kiukweli kwa sasa ni sawa tunalea mtoto hapa dukani. No efficiencyMvumilie ana nyota ya biashara huyo. Usije ukarogwa ukamfukuza.
Thank me later
Kumpangia mazingira gani boss? Hebu fafanuaNafikiri Busara ikitumika ushenzi utapungua solution ni kumpangia mazingara mazuri kazini na sio kumfukuza ,ukimrudisha mtaani utakuwa hukumsaidia ,kama una imani na Mwenyezi Mungu basi hupotezi kitu bali mapato yako yatazidi .
Asante kwa pongezi. Ushauri wako ni mzuri sana. Kama Nikimwongezea miezi mitatu nitampa nusu mshahara.Kwanza nikupongeze Kwa Subra na busara ulizonazo Kupitia maisha uliyonayo Kupitia wewe na wafanyakazi wako maana kumlipa mfanyakazi Ambaye yupo nje ya kazi mara nyingi imezoeleka sehemu za Ajira za serikalini ndio wanafanya hivyo...βοΈ
Ushauri wangu kwako ni kwamba...πππ
π Point Yako Kubwa Ni Ufanisi wa kazi kuwa Tofauti na mwanzo baada ya kuanza kulea mtoto...
"Wanasema Kujua Tatizo Ndio Mwanzo Wa Kujua Tiba"
... Tayari Ushajua Kwamba Binti Kapoteza Ufanisi wa kazi kwasababu ya Mtoto yaani malezi Kwahiyo kama itakupendeza muongezee Muda Wa kuendelea kumlea Mtoto wake kwasababu miezi 3 mtoto bado anakua Katika stage ya usumbufu utulivu unakua mdogo...
πKama ulivyokua unamlipa Kipindi Cha miezi 3 basi muongezee Tena miezi 3 iwe 6 then ndio arudi kazini na wakati huo unampa hiyo nafasi unamweleza Kabisa kuwa nakuongezea Muda Wa kulea mtoto kwasababu Sahivi utendaji wako wa kazi umeshuka nakupa Muda Ili ukirejea Tena uwe sawa...
πAta kushukuru kwakuona unamjali na kumthamini ata atakaporejea Tena atajitahidi Kupambana Zaidi...
π€Hao wanaoshauri sijui kwasababu amezaa na mwamme Ambaye hatoi huduma basi biashara yako itatumika Kuhudumia familia yake Hilo halina ukweli kwasababu misingi na taratibu za biashara zako zitakua vilevile kama mtu akiamua kuiba ata asingekua na mtoto angeiba tu....
πUmepata mtu anayejua biashara yako inakwendaje... Ametengeneza urafiki na wateja... Kumuacha huyo Binti Kuna Namna Fulani ya biashara kupungua mapato na pia akimpata mtu Katika wateja na kumshawishi afungue biashara kama Yako endapo utamfukuza ni rahisi kuama na wateja pia...
ENDELEA KUTUMIA HEKIMA NA BUSARA KATIKA MAAMUZI YAKO ATA KULETA HII MADA HUMU NI HEKIMA ULIYONAYO PIA KILA LA KHERI...πππ
Kumpangia mazingira gani boss? Hebu fafanua
Nafikiri Busara ikitumika ushenzi utapungua solution ni kumpangia mazingara mazuri kazini na sio kumfukuza ,ukimrudisha mtaani utakuwa hukumsaidia ,kama una imani na Mwenyezi Mungu basi hupotezi kitu bali mapato yako yatazidi .
Hapa dukani kwetu tuna binti mmoja ambaye mwaka jana alipata ujauzito. Ulipofika muda wa kujifungua tulimpa likizo ya miezi 3 ambapo pia tuliendelea kumlipa. Mwezi huu wa kwanza tarehe 1 alirudi tena kazini ila akiwa na mtoto wake. Binafsi nilidhani baada ya miezi 3 angeweza kurudi na kuchapa kazi kama kawaida ila imekuwa tofauti. Kimsingi performance yake ni ya chini mno huku kukiwa na excuses mbalimbali zinazomfanya atumie muda wa kazi kwenye shughuli zake. Pia kufika kazini kwa muda unaotakiwa imekuwa changamoto kwake. Nimeshajiridhisha kuwa itachukua muda kurudi kwenye ufanisi wake wa awali kabla ya mimba.
Nimewaza kuachana naye mwisho wa mwezi huu na kumpa mkono wa kwaheri. Lakini kabla hatujafika hiyo tarehe naomba ndugu zangu wa JF mnishauri maana suala la kumwachisha mtu kazi ni zito mno. Kazi ni uhai.
Ninawasihi mabinti waache ngono kabisa ila wakishindwa watumie condom badala ya kubeba mimba na kuishia kubebeshwa mzigo wa malezi. Pia kwepa kubeba mimba ya mtu maskini ambaye sio mumeo. Usimwamini kijana maskini ambaye hajakuoa anaekudanganya kuwa hatakukimbia ukipata mimba.
Mkuu haya mambo ukiyafikiria yanakera mno. Vibinti badala ya kuwaza maisha vinawaza mapenzi matokeo yake wanajiingiza kwenye shida. Itoshe kusema rasmi huyu binti ni SINGLE MAMA. Ninachotaka kufanya ni kumwondoa bila kuacha damage kubwa kwenye nafsi yake. Hawachelewi kutupa kichanga chooni.Labda anamaanisha umuwekee hausigel na kumlipa mshahara bila kusahau formula ya mtoto ni juu yako pia. Hawaulizi kabisa alipo baba wa mtoto
Ni kweli,bado hajawa serious kwenye biasharaWewe Bado Sana mkuu...ma capitalists hufukuza yeyote muda wowote..