Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,259
- 20,891
Ni kama miezi minne iliyopita niliwahi kulalamikiwa na jirani yangu kuwa Net za misaada zinasababisha kunguni,nilishangaa sana lakini sikuonesha kushangaa huko kwa yule aliyeniambia
Baada kama ya wiki moja tangu niambiwe kituko kile na jirani yangu nilifika nyumbani nikakuta wapangaji wenzangu wanajadili jambo hilohilo lakini kulikuwa kumeongezeka kitu kingine,kilichoongezeka ni kuwa eti net hizo zinasababisha "uzembe" kwa akina baba ndoani,nilizidi kushangaa,ilibidi niwaulize kama wanajua wanachokiongea na walinihakikishia kuwa ni kweli
Nikaona isiwe tabu,niliamua tu kuwa wakati ambapo nitakuwa na muda nitakuwa nafanya ka uchunguzi kangu ili kujua kama mambo hayo ni kweli
Nilifanikiwa kuwahoji akina mama 82 wa maeneo ya Gedeli,Nyakato national,Nyakato sokoni,Buzuruga pamoja na mahango,kati ya hao 75 walikiri kupata kunguni baada ya kuanza kuzitumia net hizo na 5 walisema kuwa ndani mwao kuliwahi kuwa na kunguni kabla ya kutumia hizo net hivyo waliporudi hao kunguni walijua ni kutokana na kuwepo kwao mwanzo,2 waliobaki waliniambia kuwa wanazo hizo net lakini hawajazitumia
Nilipowauliza kuhusiana na suala la "uzembe" wa akina baba kwenye ndoa zao walisema kuwa kuna mabadiliko lakini hawawezi kuthibitisha kama mabadiliko hayo yanasababishwa na hizo net au laa,kimsingi suala la uzembe halina ushahidi wa kutosha lakini hilo la kunguni linaonesha kwa utafiti huo mdogo tu lina ushahidi
Jambo hili limenishangaza sana na nimejiuliza sana maswali na kukosa majibu,nadhani kuna haja ya serikali kupitia wizara ya afya kulichunguza jambo hili kama lina ukweli basi hatua stahiki zichukuliwe
Kiukweli hadi sasa nastaajabu kuwa kama ni kweli inakuwaje net hizi zisababishe hii kitu
Najua JF kuna watu wenye maisha tofauti tofauti na kuna wengine hawawajui hawa wadudu ambao sisi wa uswazi tunawajua na tunakimbizana nao kwenye majumba tunayoishi
Kama huwajui hawa hapa ..........
Suala hili sijui kama kuna mwingine amewahi kilisikia hapa,na kama ni kubwa kwa kiasi nadhani kuna haja ya kuchukua hatua,waswahili wanasema "bure gharama" naona hii ndio gharama ya bure!!!!!!!!!
Baada kama ya wiki moja tangu niambiwe kituko kile na jirani yangu nilifika nyumbani nikakuta wapangaji wenzangu wanajadili jambo hilohilo lakini kulikuwa kumeongezeka kitu kingine,kilichoongezeka ni kuwa eti net hizo zinasababisha "uzembe" kwa akina baba ndoani,nilizidi kushangaa,ilibidi niwaulize kama wanajua wanachokiongea na walinihakikishia kuwa ni kweli
Nikaona isiwe tabu,niliamua tu kuwa wakati ambapo nitakuwa na muda nitakuwa nafanya ka uchunguzi kangu ili kujua kama mambo hayo ni kweli
Nilifanikiwa kuwahoji akina mama 82 wa maeneo ya Gedeli,Nyakato national,Nyakato sokoni,Buzuruga pamoja na mahango,kati ya hao 75 walikiri kupata kunguni baada ya kuanza kuzitumia net hizo na 5 walisema kuwa ndani mwao kuliwahi kuwa na kunguni kabla ya kutumia hizo net hivyo waliporudi hao kunguni walijua ni kutokana na kuwepo kwao mwanzo,2 waliobaki waliniambia kuwa wanazo hizo net lakini hawajazitumia
Nilipowauliza kuhusiana na suala la "uzembe" wa akina baba kwenye ndoa zao walisema kuwa kuna mabadiliko lakini hawawezi kuthibitisha kama mabadiliko hayo yanasababishwa na hizo net au laa,kimsingi suala la uzembe halina ushahidi wa kutosha lakini hilo la kunguni linaonesha kwa utafiti huo mdogo tu lina ushahidi
Jambo hili limenishangaza sana na nimejiuliza sana maswali na kukosa majibu,nadhani kuna haja ya serikali kupitia wizara ya afya kulichunguza jambo hili kama lina ukweli basi hatua stahiki zichukuliwe
Kiukweli hadi sasa nastaajabu kuwa kama ni kweli inakuwaje net hizi zisababishe hii kitu
Najua JF kuna watu wenye maisha tofauti tofauti na kuna wengine hawawajui hawa wadudu ambao sisi wa uswazi tunawajua na tunakimbizana nao kwenye majumba tunayoishi
Kama huwajui hawa hapa ..........
Suala hili sijui kama kuna mwingine amewahi kilisikia hapa,na kama ni kubwa kwa kiasi nadhani kuna haja ya kuchukua hatua,waswahili wanasema "bure gharama" naona hii ndio gharama ya bure!!!!!!!!!