Wajerumani Walificha Mali Nyingi Kwenye Ardhi ya Tanzania

Wajerumani Walificha Mali Nyingi Kwenye Ardhi ya Tanzania

Mkuu, ni hatariii.....Ngoja nikupe kisa changu kilichonipata katika hizo pilika.

Kwanza nilivutiwa na jamaa fulani hivi tukiwa Mbeya huko wilaya XYZ,jamaa walifankkiwa kuopoa sanduku la dhahabu kwa Style hyhy ya kusaka Mali za wajerumani. Walikula bata sana na hadi muda huu ni malordilofa,yaani pesa bado wanayo.

Basi bhana,nikasafiri hadi wilaya kwa wajomba zangu baada ya kujifunza Code chache ambazo wajelumani walitumia kama alama na nikagundua hivi vitu nilivionaga kwa wajomba zangu nikiwa nachunga ng'ombe milimani.

Nilipofika kwa babu,nikanyoosha msituni kwenda kuhakiki kama zile alama kwenye miti,mawe na michoro kama ipo, bahati nzuri bhana nikavikuta kama vilivyo,wala havijaharibiwa sana na waharibifu wa mazingira. Nikashauriana na vijana wa pale tukaanza utaratbu wa kuchimba.

Huku tukiendelea kukutana na code na ninazisoma vizuri na kusonga mbele,baada ya siku 6 hatimaye tukalifikia sanduku bhana....!! Tulichokiona humo......mmamaye ,nikikumbuka huwa hata sijielewagi,maana ni hatari.

Tulikutana na marehemu mzungu humo.....ashamong'onyoka kawa unga tu,sijui walimtia nini hakuoza,kawa vumbi tu na mifupa, hilo vumbi likaingia vifuani, tulikohoa karibia ya kunya......!!!!

Aisee.....tulirudi nyumbani tukatengeezwa kienyehi ndio mambo yakawa sawa, lakini kuna mzee akasema mgetoa lile sanduku ndio mgekutana na mzigo wenyewe....!! Alinistua mbaya,lakini cha ajabu,nasema tena chaa ajabu niliporudi kule porini ile sehemu sijaikuta na wala sikuiona tena hadi leo, nilienda takribani mara 6 kwa siku tofauti lakini mpaka leo sipajui eti.....!!

Kuna sehemu tena nipo ugenini,nilikwenda kucheki shamba la kununua nimekutana na code tena za ajabu aisee.....!!! Sasa sijajua nini wameficha...!!

Kwanza nilikuta Mti mkubwa una mzizi upo nje,mzizi huo umetobolewa,nikaufuatilia kidogo nikakuta tobo la pili, nikaendelea kufukua nikakuta nikakuta tena mzizi umekunjwa kuelekea direction ya kusini,nikaendelea kuufuata, mbele ya huo mzizi kulikuwa na jiwe kubwa sana kama tani 30 hivi, nilipolizoom vizuri kabisa na kulichunguza,nikagundua kuwa huyo ni picha iliyojchongwa picha ya bundi...!!!! Nikafukuafukua kuzungua hilo hiwe nikakuta ramani aisee.....!!! Bahati mbaya sijui kijerumani .

Mzee nikaazimia kazi, tukaenda kwa mchawi wetu akasema kuna mzigo wa kufa jamaa....vizuri vyote ruby,gold na sapphire akasema zipo. Akatupa masharti tukaingia mzigoni...!!

Baba tumefungua ardhi huku tukifuata masharti makamanda tulikuwa 6, tuliikosea ramani kidogo tukajikuta kuna mwamba una ninginia juu yetu.

Tulichokifikia ni kwanza kuna vigae vya mawe vimefunika kitu tusichokijua hapo chini, pili kuna ukuta umejengwa kwa mawe ya kupondekezwa hapo chini shimoni...!!

Tuliogopa kupondwa na tulikuwa tumechoka sana,maana kazi ilikuwa ya ngumu na ilituchukua miezi 3,tukasema labda tusake katapila.


Sasa tumeliacha tu na tumeamua tulime tu kwanza lakini tukiwa na matumaini kwamba ipo siku.
Sasa najiuliza,au tutakuta marehemu mzungu tena au la ....nakaribisha wadau,kama unaweza kuleta Scaveta njoo tujaribu bahati.





Sent using Jamii Forums mobile app
@Mbwichichi hizi code unazifahamu??

Nimefananisha na ile habari yako!
 
Kusaka huwa hatuachi, tutaacha kusaka na kupumzika siku tukifa....kaburini ndio pahala sahihi pa kupumzika,tena unapumzika saaana baada ya tabu nyingi za KUJILISHA UPEPO.

Sasa tuje kwenye mada. Huyu ndugu alikuja na kipimo, nikamuomba twende tukapime dhahabu maeneo flani,tukafanikiwa kupima. Sasa nikamuuliza kuhusu uwezo wa kutoa hazina za mjerumani,akasema za mapangoni ni dk chache tu,ila za ardhini hawezi,ni zike za wazi tu ndio anaweza...hizo za ardhini anaweza tu kupima na kugundua point ya site.Nikamuomba twende shimoni kuleee...akagundua kuwa ni pale chini kuna mabox matatu, lakini pia akagundua site zingine mbili karibu na eneo hilo, akaongeza pia kuwa site mbili zinalindwa na mashetani,na site moja ni mitego. Alichoomba tu kuwa tuwe share kwa yeye kutoa dawa na kutoa mzigo baada ya kufuufukua,hapa tunalia kupata Scaveta ya kuchimba..kama unalo karibu.
Kwahiyo mkuu! Hadi sasa unatafuta kifaa cha kuchimbia??? Au umeshajua hamna issue sasa unatafuta hela kwa namna nyingine?
 
BInafsi sijawahi kutamani wala kufikiria kuhusu haya mambo ya mali kale,lakini naamini na nathibitisha kabisa zipo

Babu yangu alishawahi kuniadithia sana kuhusu haya mambo maana yeye ndo alikuwa anajishughulisha na haya mambo

Na anasema enzi za ujana wake, walifanikiwa kupata mali nyingi sana na walikuwa matajiri kweli,sema walianza kufilisika taratibu baada ya kukosea miongozo flani

Kipindi ananiadithia alikua akinificha baadhi ya Siri kubwa kubwa kuhusu haya mambo,kwasababu alishanisoma ndani ya moyo wangu kuwa sina interest kabisa na hayo mambo.

Anasema kama ningeonyesha interest kidogo,basi angenifungukia siri zooote na kunirithisha rasmi nyenzo zake za kufanya izo kazi.

Anasema lengo lake kuu alitaka mimi nizitafute izo mali ili niweze kuukomboa ukoo wangu na umaskini,maana yeye alipewa iyo nafasi akaichezea...( yeye naye alifundishwa na baba ake,yaaan baba wa babu yangu)

Babu yangu alifariki 2014 akiwa na miaka 98...kuna sehemu moja uko kijijini kwetu katika mashamba yake,aliacha usia kwamba pasichimbwe ,wala kupandwa kitu chochote kile juu ya ile ardhi mpaka pale atakapotokea mteule katika ukoo wetu na atapewa ishara maalumu

Iyo sehemu katika shamba,kwa juu kuna mchanga mweupee ambao ni mkavu kipindi chote hata mvua inyeshe namna gani hapaloi

Ukoo wote unaamini pengine ilo eneo ndo sehemu alipohifadhia nyenzo zake za kufanya izo kazi za kutafuta mali za kale.
 
JAMANI TULIENI KIDOGO MNISIKIE:
Japo natumia maandishi ila najua mnanisikia. Unapokuwa mtu mzima inamaanisha unakuwa na uwezo wa kuhandle situation yoyote na kufikia mwisho wenye manufaa kwako. Unapopata habari handle situation halafu utafute possibility kama ipo.
Hazina ya mjerumani kubaki nchini ilinifikisha hapa;
1.Story kuhusu meli ya MV LIEMBA kuzama katika ziwa Tanganyika. Mjerumani alikuwa anachukua Mali kutoka DRC kuja TZ kwakutumia meli ile na inasadikika meli ile ilizamishwa na hii iliyopo leo ni tela lake tu,na wajerumani walishaomba kuja kuichukua kwa ofa ya meli mbili mpya. POINT TO VIEW: je wajerumani walikuja kuchukua mali afrika na kuzipeleka kwao au kuzitawanya Tanganyika? Je kama hii MV LIEMBA iliyopo ilikuwa ni tela la ile iliyozamishwa ni kweli teknolojia ya usafiri wa majini ina mambo ya kuvutana kama barabarani mfano wa lori na tela lake?
2.Story ya kuacha mali zake kwa kukimbia vita. POINT TO VIEW. Tunajua mjerumani alipigana kumuondoa mwarabu Tanganyika,Je historia inasemaje kuhusu namna alivyoondoka mjerumani nchini Tanganyika? Je, Hakuondoka kwa baraza tu? Wataalamu wa historia mtuelezee kidogo hapa.
3. Mjerumani kupigwa na mrusi na kushindwa kuitawala dunia.POINT TO VIEW. Je, hizi sifa na uwezo mkubwa wa nanma hii juu kuficha malizake alipewa tu kutoka kusikojulikana ama ilikuwakuwaje maana ukisikiliza utagundua ni uchawi mkubwa sana sio wa kushindwa kupigana vita.
Hapo ndipo nilipofika mimi na kuhitimisha kuwa kitu kisicho na uthibitisho ni imani tu. Sijui upande wenu.




MAGUFULI4LIFE.

Umeandika nini sasa !!? Umeanza vizuri ila kumaliza ukamalizia utopolo
 
laiti ungejua inapata kiasi gani kwenye haya maswala wala usingekuwa mtu wa ku critsize jumla jumla...... shida iliyopo mpaka sasa jamii kubwa haina elimu juu ya mali kale na Bahati mbaya jamii forum kila aliyejisajili humu ni Mjuaji sana hata kama ni mweupe juu ya jambo.
Mkuu,kwa majibu yako inaoneka una uelewa wa haya mambo tunaomba utoe shule na uzoefu wako ili kuondoa sintofahamu na dhana potofu kuhusu hizi mali

Unaweza kuanzisha Uzi wako au hata hapahapa ili tupate kuuliza maswali ya ufahamu
 
Mkuu,kwa majibu yako inaoneka una uelewa wa haya mambo tunaomba utoe shule na uzoefu wako ili kuondoa sintofahamu na dhana potofu kuhusu hizi mali

Unaweza kuanzisha Uzi wako au hata hapahapa ili tupate kuuliza maswali ya ufahamu
Changamoto hapa,watu wanaodhaniwa wanauelewa,uzoefu wa habari hizi hawapo tayari kuelezea kwa kina,Mimi no zaidi ya Juma moja lililopita,nilishauri kama ulivyoshauri hapa.
 
Changamoto hapa,watu wanaodhaniwa wanauelewa,uzoefu wa habari hizi hawapo tayari kuelezea kwa kina,Mimi no zaidi ya Juma moja lililopita,nilishauri kama ulivyoshauri hapa.
Hilo ndio tatizo,hawa wenye uelewa wafunguke ukweli wote kuhusu habari nzima ili watu wapate elimu,huenda ikasaidia watu kuacha kukurupuka na kuishia kutapeliwa au kufanya utafutaji bila kujua taratibu zake
 
Changamoto hapa,watu wanaodhaniwa wanauelewa,uzoefu wa habari hizi hawapo tayari kuelezea kwa kina,Mimi no zaidi ya Juma moja lililopita,nilishauri kama ulivyoshauri hapa.
hapana siyo kwamba watu hawapo tayari ila unajua na majukumu mengine lazima yaende na kipindi chance ipatikanapo kuingia huku basi unajibu kwa kadiri uwezavyo na kwa uelea huo huo mchanga uliopo kujaribu kusaidia mwingine na mwingine na yote nikusaidia ili wengine waisiende kichwa kichwa na kuingia kwene utapeli na kuzidi kuharibu sifa ya hazina hizi.
 
BInafsi sijawahi kutamani wala kufikiria kuhusu haya mambo ya mali kale,lakini naamini na nathibitisha kabisa zipo

Babu yangu alishawahi kuniadithia sana kuhusu haya mambo maana yeye ndo alikuwa anajishughulisha na haya mambo

Na anasema enzi za ujana wake, walifanikiwa kupata mali nyingi sana na walikuwa matajiri kweli,sema walianza kufilisika taratibu baada ya kukosea miongozo flani

Kipindi ananiadithia alikua akinificha baadhi ya Siri kubwa kubwa kuhusu haya mambo,kwasababu alishanisoma ndani ya moyo wangu kuwa sina interest kabisa na hayo mambo.

Anasema kama ningeonyesha interest kidogo,basi angenifungukia siri zooote na kunirithisha rasmi nyenzo zake za kufanya izo kazi.

Anasema lengo lake kuu alitaka mimi nizitafute izo mali ili niweze kuukomboa ukoo wangu na umaskini,maana yeye alipewa iyo nafasi akaichezea...( yeye naye alifundishwa na baba ake,yaaan baba wa babu yangu)

Babu yangu alifariki 2014 akiwa na miaka 98...kuna sehemu moja uko kijijini kwetu katika mashamba yake,aliacha usia kwamba pasichimbwe ,wala kupandwa kitu chochote kile juu ya ile ardhi mpaka pale atakapotokea mteule katika ukoo wetu na atapewa ishara maalumu

Iyo sehemu katika shamba,kwa juu kuna mchanga mweupee ambao ni mkavu kipindi chote hata mvua inyeshe namna gani hapaloi

Ukoo wote unaamini pengine ilo eneo ndo sehemu alipohifadhia nyenzo zake za kufanya izo kazi za kutafuta mali za kale.
iliyopo hapo Mzee wako alikuwa anashindwa kukwambia kuwa Mahali hapo palikuwa na hizi mali lakini wao na ukoo wao walitumia kwa matambiko iwe kwa wazi au kwa siri na kama ukishaanza kufanya matambiko basi zina anza kuwa control kwa namna yake.... kwa ufupi tu ni hivyo
 
Kama kina kinjeketile, mkwawa , milambo etc wangepata hata elimu ya kuandika, may be wangetuandikia vitabu vya siri ili kuturahisishia kazi zama hizi
 
Ma
Huyu jamaa alikuwa na extra power gani mkuu?na kwanini watumie power yake kwenye hivi vitu?
kuna maombi aliyofanya kwa ajili ya kupata zile items na ukumbuke vile vitu havikutengenezwa na mwanadamu awaye yote.
 
Mkuu,kwa majibu yako inaoneka una uelewa wa haya mambo tunaomba utoe shule na uzoefu wako ili kuondoa sintofahamu na dhana potofu kuhusu hizi mali

Unaweza kuanzisha Uzi wako au hata hapahapa ili tupate kuuliza maswali ya ufahamu
Mkuu swala la Mali kale ya Mjerumani lina elimu pana sana sana sana zaid na huwezi anzisha thread tu lakini uonapo mwenzio amezungumza ambacho unajua na unaona ameenda wrong basi unaanzia pale kumuweka sawa hata kwa kielimu kidogo mtu ulichonacho🙂
 
Natafta share...... Na awe mtaalamu wa kusoma code.... Kuna eneo lina Mali, serious tu ndio anitafte
unatafuta share!, kwavipi?
awemtaalamu wa kusoma Code?
Jaribu kuelezea ulichonacho na inaweza pelekea ukapata wa kukusaidia.
 
Masoko ya kuuza hizo bidhaa yap

Masoko ya kuuza hizo bidhaa yapo wapi?
Tuanzie hapo zile siyo bidhaa na ile siyo Biashara bali kwa kanuni na sheria zake na malipo ya pesa yake wanaita ni sadaka kwa maana moja hakuna mtu afanyae biashara na Mfalme bali Mfalme huwa anatoa sadaka yake kwa watu......
CAESAR WILHELM II alikuwa ndiye Mfalme wa mwisho Ujerumani na Vyombo vyote vitafutwavyo vina alama ya sura yake sasa ukipeleka kwa waliokula kiapo cha kuwa wakusanyaji wa zile item basi wanakupa kiasi ambacho ile familia imepanga kwa kushukuru vile vyombo kurudishwa kwenye ufalme wao.
Kuhusu wachukuaji wapo na Mmoja ndiye sahihi na Yupo vizuri zaidi.
 
Ma

kuna maombi aliyofanya kwa ajili ya kupata zile items na ukumbuke vile vitu havikutengenezwa na mwanadamu awaye yote.
Mkuu hivyo vitu havikutengenezwa na mwanadamu kivipi?? Yani vilitokea wapi sasa??
 
Back
Top Bottom