Hii ilikuwa lini ? Bado tunaduru katika Historia,nataka nikuonyeshe Historia sahihi ni ile yenye "chain".
Usiniulize swali ambalo unapaswa kujibu wewe,hekalu ni nini ? Ni kanisa ? Au hekalu ni soko ?
Huwa najiuliza inakuwaje mnajadili mambo msiyo kuwa na elimu nayo ?
Uislamu umegawanyika sehemu kuu mbili :
1. Uislamu wa ujumla huu ni ule ambao mitume na manabii wote waliufundisha ya kwamba aabudiwe Mola peke yake wala wasimshirikishe na chochote na kuwapiga vita mataghuti na washirikina kwa hali zao zote. Mafundisho haya yalifundishwa na mitume wote na manabii,ndiyo kuanzia Nuhu mpaka Mtume muhammad imani yao ilikuwa moja.
2. Kuna Uislamu maalumu ambao huu amekuja nao Mtume Muhammad.
Usipate shida kijana,thibitisha wapi Suleyman alikuwa myahudi,sababu Uyahudi ulilaaniwa kwa ulimi wa Yesu (Issa) na ulimi wa Dawood (Baba yake Suleyman).
Ukinithibitishia ya kuwa Suleyman alikuwa Myahudi kiimani mimi nitakuwa Myahudi.
Wewe niambie tu lini Uyahudi ulianza na nani alikuwa wa mwanzo katika dini hii. Hizi stori nyingine hazina maana hapa,sababu hazielezei chimbuko la Uyahudi.
Ushawahi kukisoma hicho kitabu kwanza ? Ukweli uko hivi baada ya Qur'aan kwa usahihi hakuna kitabu kinazidi sahihi Bukhari kwa usahihi,kusanya vitabu vyote mpaka vya Sayansi hakuna duniani.
Sasa unatakiwa ujiuliza Bukhari ni nani na alikusanya vipi hizo hadithi je aliota au ilikuwaje kisha uje kujadiliana na mimi kuhusu Hadithi. Elimu yake ni elimu yenye sharafu.
Ndiyo maana sisi tunataka chain,Bukhari alikuwa na chain inayofika mpaka kwa mtume kupitia watu walio waona wanafunzi wa mtume mpaka walio muona mtume. Leo hii hapo ulipo unaamini ya kuwa Isaac Newton alikuwepo lakini tukikuuliza unamjua yeyote aliyemuona Newton na akatupasha sisi habari mpaka kufika leo hii,swali hili huwezi kujiuliza zaidi ya kukariri nw kufurahia stori za Sayansi,lakini huki kwetu lazima tumjue nani amesimulia toka kwa nani mpaka inafika kwa wa kwanza. Hii ndiyo Elimu ya Haidithi.
Tuendelee...