Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
Wanabodi,
Kama kawa, kila nipatapo fursa, huwapiga tuu watu darsa humu, leo naliendesha darasa nikitokea Tanga kwa waja leo, warudi leo. na ni darsa kuhusu muungano wa kweli. Swali ni Je Wajua Muungano wa Kweli, Ni Muungano wa Serikali Moja?. Wajua Karume, Alitaka Serikali Moja, Nyerere Ndiye Akazuia?. Jee Wazanzibari Watakubali?.
Hizi ni makala mwendelezo kuhusu kauli za kibaguzi za kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, nikazungumzia kuwa zinasababishwa na ukosefu wa elimu ya uraia, kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, leo nitaumalizia mjadala huu kwa kuangazia eleza watu na haswa Wazanzibari kuwa Karume, alitaka muungano wa serikali moja, Mwalimu Nyerere ndie alimgomea na kuamua tuanze kwanza na serikali mbili, kisha twende kwenye serikali moja.
Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, tuko R mtangamano wa kuunda shirikisho la Afrika Mashariki. Nyerere na Karume ndio ma pioneers wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kuunda JMT. Rais Samia na rais Mwinyi, wana fursa ya kuipeleka Tanzania kwenye serikali moja, Tanzania ikawa kinanara wa utangamano wa Afrika Mashariki kuelekea shirikisho.
Kuungana kwa TANU na ASP
Vyama vya TANU na ASP vilipoungana ile 1977, sii wengi humu walikuwa wamezaliwa!, wengi humu wamezaliwa, wameikuta CCM, hawakuikuta TANU na ASP, hivyo hawajui kwanini TANU na ASP viliungana, na viliungana ili iweje?.
Mimi ni mtu wa 60s, hivyo ile 1977, TANU na ASP zilipoungana nilikuwa darasa la tatu, kijijini Itonjanda, nikikaa kwa bibi mzaa Baba, Bibi Wakawombwe, (RIP) baada ya Baba Mzee Mayalla(RIP) kuhusika na yale mambo fulani ya Mwanza ya 1976!.
Sababu ya TANU na ASP kuungana, ni kuelekea kwenye serikali moja!. Baba wa taifa, Mwalimu Nyerere alisema huu muungano wa vyama vya TANU na ASP na kuzaliwa chama kipya, Chama cha Mapinduzi, CCM, ni mwanzo wa safari ya kuondoka kwenye serikali mbili, kuelekea kwenye serikali moja!.
Watanzania wanahitaji sana kuelimishwa kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu. Baada ya muungano, nchi zote mbili zilitoweka, hakuna nchi ya Tanganyika wala hakuna nchi ya Zanzibar, bali nchi ni moja tuu ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Zanzibar.
Rais Samia ni Fursa Adimu na Adhimu Kutupeleka Kwenye Serikali Moja.
Kuna wengi wamemfahamu Rais Samia baada ya lile tukio la March 17, 2021, lakini tuko akina sisi, tuliomfahamu kabla na kuzungumza nae ana kwa ana kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu.
Mara ya kwanza nilizungumza nae, akiwa Waziri wa nchi Ofisi ya Makamo wa Rais anayeshughulikia muungano, mwaka 2014 wakati wa miaka 50 ya Muungano, kisha nikaja kuzungumza nae tena akiwa M/M mwenyekitii Bunge Maalum la Katiba.
Samia yule niliyemjua mimi ni Samia huyu niliyewaletea humu wana jf. Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth!”
Na kuhusu Muungano "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza, alisema
Hitimisho
Kwa vile Rais Samia, ndiye aliruhusu watu wawe huru kuujadili muungano, na anakwenda kutupatia katiba mpya, nashauri hili la mkanganyika wa katiba kati ya katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, pia litarekebishwa, na kwa maoni yangu, dawa pekee ya uhakika na ya kudumu ambayo ni mwarobaini wa kuondoa hii sumu ya ubaguzi wa Utanganyika na Uzanzibari, ni kwenda kwenye serikali moja. Kidonge hicho japo ni kichungu kumeza kwa wenzetu wa Zanzibar, wenzetu nao walazimishwe wameze, waipoteze Zanzibar yao, kama Watanganyika tulivyopoteza Tanganyika yetu, kunakuwa hakuna Tanganyika, hakuna Zanzibar, kuna Tanzania tuu!. Tena kidoge hiki ndio muarobaini au kidoge cha anti bayotiki ya kuzitibu na kuzimaliza kabisa kero zote za muungano.
Wasalaam.
Paskali
Rejea za Mwandishi kuhusu serikali moja.
- Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, then "Twende kwenye Serikali Moja!"
- Je, umefika wakati kutimiza Uzalendo wa kweli wa kwenda kwenye Serikali moja?
Kama kawa, kila nipatapo fursa, huwapiga tuu watu darsa humu, leo naliendesha darasa nikitokea Tanga kwa waja leo, warudi leo. na ni darsa kuhusu muungano wa kweli. Swali ni Je Wajua Muungano wa Kweli, Ni Muungano wa Serikali Moja?. Wajua Karume, Alitaka Serikali Moja, Nyerere Ndiye Akazuia?. Jee Wazanzibari Watakubali?.
Hizi ni makala mwendelezo kuhusu kauli za kibaguzi za kunyoosheana vidole vya Utanganyika na Uzanzibari, nikazungumzia kuwa zinasababishwa na ukosefu wa elimu ya uraia, kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu, leo nitaumalizia mjadala huu kwa kuangazia eleza watu na haswa Wazanzibari kuwa Karume, alitaka muungano wa serikali moja, Mwalimu Nyerere ndie alimgomea na kuamua tuanze kwanza na serikali mbili, kisha twende kwenye serikali moja.
Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, tuko R mtangamano wa kuunda shirikisho la Afrika Mashariki. Nyerere na Karume ndio ma pioneers wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kuunda JMT. Rais Samia na rais Mwinyi, wana fursa ya kuipeleka Tanzania kwenye serikali moja, Tanzania ikawa kinanara wa utangamano wa Afrika Mashariki kuelekea shirikisho.
Kuungana kwa TANU na ASP
Vyama vya TANU na ASP vilipoungana ile 1977, sii wengi humu walikuwa wamezaliwa!, wengi humu wamezaliwa, wameikuta CCM, hawakuikuta TANU na ASP, hivyo hawajui kwanini TANU na ASP viliungana, na viliungana ili iweje?.
Mimi ni mtu wa 60s, hivyo ile 1977, TANU na ASP zilipoungana nilikuwa darasa la tatu, kijijini Itonjanda, nikikaa kwa bibi mzaa Baba, Bibi Wakawombwe, (RIP) baada ya Baba Mzee Mayalla(RIP) kuhusika na yale mambo fulani ya Mwanza ya 1976!.
Sababu ya TANU na ASP kuungana, ni kuelekea kwenye serikali moja!. Baba wa taifa, Mwalimu Nyerere alisema huu muungano wa vyama vya TANU na ASP na kuzaliwa chama kipya, Chama cha Mapinduzi, CCM, ni mwanzo wa safari ya kuondoka kwenye serikali mbili, kuelekea kwenye serikali moja!.
Watanzania wanahitaji sana kuelimishwa kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu. Baada ya muungano, nchi zote mbili zilitoweka, hakuna nchi ya Tanganyika wala hakuna nchi ya Zanzibar, bali nchi ni moja tuu ya JMT yenye sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Zanzibar.
Rais Samia ni Fursa Adimu na Adhimu Kutupeleka Kwenye Serikali Moja.
Kuna wengi wamemfahamu Rais Samia baada ya lile tukio la March 17, 2021, lakini tuko akina sisi, tuliomfahamu kabla na kuzungumza nae ana kwa ana kuhusu huu muungano wetu adimu na adhimu.
Mara ya kwanza nilizungumza nae, akiwa Waziri wa nchi Ofisi ya Makamo wa Rais anayeshughulikia muungano, mwaka 2014 wakati wa miaka 50 ya Muungano, kisha nikaja kuzungumza nae tena akiwa M/M mwenyekitii Bunge Maalum la Katiba.
Samia yule niliyemjua mimi ni Samia huyu niliyewaletea humu wana jf. Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth!”
Na kuhusu Muungano "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza, alisema
hivyo sina hata chembe ya shaka kuhusu uzalendo wake wa kudumisha muungano,Wanabodi,
Kwa hoja za muungano Mama Samia alizoshusha, ningekuwa ni uwezo wangu, ningeshauri October 2020, Mama Samia ndiye ampokee Dr. Shein kule Zanzibar, ili 2025, aje ampokee Magufuli, maana kwa maoni yangu, kwa uongeaji huu, huyu mama ndiye Mzanzibari pekee anayekubalika kuweza kuchagulika kuwa rais wa JMT kutokea Zanzibar, vinginevyo Wazanzibari wausahau kabisa urais wa Muungano, wao mwisho wao ni umakamo wa rais pekee.
Anasema Zanzibar inafaidika sana na muungano, kisiasa, kiuchumi na kijamii, ikiwemo kufaidika kielimu, wakati wa muungano, Zanzibar haikuwa na chuo kikuu chake hivyo Wanzanzibari wote wa enzi hizo waliofika elimu ya vyuo vikuu, wamesomea bara.
Mama Samia amesema watu waachiwe kuujadili muungano kadri watakavyo na hata kutema nyongo kuhusu muungano, na serikali inazitumia hizo hoja zinazolalamikiwa kuimarisha muungano, akasema ni heri watu wafunguke na kusema hivyo kuyatoa madukuduku yao, kuliko kunyamaza na madukuduka ndani yao, siku wakilipuka moto utawaka, hivyo watu waachwe waseme.
Amesema Zanzibar ni visiwa hivyo viko wazi pande zote, hivyo faida kubwa kabisa ya muungano ni ulinzi usalamax amani na na utulivu wa Zanzibar, bila muungano, ilikuwa ni rahisi sana kuivamia Zanzibar na Zanzibar ikivamiwa ni rahisi sana kuivamia bara, hivyo muungano umeimarisha sana ulinzi na usalama, amani na utulivu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kuna kitu Mama Samia amekisema sikuwahi kukijua!. Kumbe Wizara ya Mambo ya Nje ilipokiwa ikiitwa Wizara ya Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa ndio ilikuwa ya Muungano iki handle issues zote za Zanzibar kimataifa, lakini , ilipobadilishwa jina na kuitwa Wizara ya Mambo, ya Nje na Ushirikiano wa Africa Mashariki, sasa ina handle mambo ya Zanzibar ndani ya Africa Mashariki tuu, lakini kimataifa, kwa yale mambo ambayo sio ya muungano, SMZ ya Zanzibar imepewa uhuru wa kunegotiate ufadhili, misaada, na mikopo na mikataba ya kimataifa kwaniaba ya Zanzibar, ila kwenye kutiliana saini, anayetia saini ni serikali ya JMT, kwasababu Zanzibar haina sovereignty, sovereignty ni moja tuu ambayo iko kwenye JMT pekee!.
Hili sikuwahi kulijua, hivyo kumbe sasa Zanzibar inaweza kupata misaada na mikopo ya kimataifa, sasa kwavile uwiano wa kugawana misaada ya kutoka nchi wafadhili na wahisani, Zanzibar inastahili kupata asilimia 4.5% ya misaada yote kwa Tanzania, sasa kwa vile Zanzibar nayo inaweza kuomba ufadhili wa kimataifa, jee hii misaada ya kimataifa ya Zanzibar inayoomba, Tanzania bara pia tunapewa ule mgao wa asilimia 95.5% ya misaada ya Zanzibar, au misaada ya Tanzania tuu, ndio Zanzibar inapaswa kugaiwa asilimia 4.5%, lakini kwa misaada ya Zanzibar, then misaada hiyo ni ya Zanzibar pekee?.
Mama Samia amezungumzia kero za muungano na kusema kero nyingi zimeisha tatuliwa ila utekelezaji ndio unasua sua, na kutolea mfano deni lililokuwa la umeme la Tanesco, deni hilo lilisababishwa na double taxation, kwa Tanesco kuwachaji SMZ VAT huku shirika la umeme la Zanzibar, Zesco nalo likiwachaji kodi ya ongezeko la thamani Vat, wateja watumiaji wa umeme zao nao wakilipishwa Vat, kero hiyo imetatuliwa kwa Tenesco hawaichaji tena Vat kwa SMZ, hivyo Zanzibar haidaiwi tena deni lolote la umeme na Tanesco.
Ninachokumbuka kwenye deni la umeme la Zanzibar, lilitokana na Tenesco kuuza umeme kwa bei ya juu kwa Zesco, halafu Zesco wanauza umeme huo kwa bei ya chini Zanzibar, kumbe ilikuwa ni issue ya VAT!.
Pia amezungumzia kero za muungano kadri zinavyotatuliwa, kero nyingine zinaibuka, hivyo issue za kero za muungano ni issue endelevu.
Amezungumza mengi na kumalizia kwa kusisitiza Muungano ni jambo jema, tuulinde na kuuenzi.
Kwa hoja kama hizi za huyu mama Samia, kama age sio issue sana, si huyu mama atatufaa sana 2025 au tuwashauri kwa vile Magufuli analamika sana kuhusu urais, mara ni mateso, mara ni kazi ngumu, mara ni mzigo mzito, tumshauri rais Magufuli, kwa vile Samia anatosha sana, hivyo tumpunguzie mateso, hana haja ya kuendelea na mateso, mzigo mzito na kazi ngumu ya urais, na hata kama ni wale tausi au wanyama wa Magogoni, au yale majabali ya Chamwino, tutamjengea Chato na kumuomba bora apumzike tuu mapema, na kumpisha Mama Samia ndio amalizie ngwe yake iliyobakia?. Hili mnalionaje?.
Paskal
Hitimisho
Kwa vile Rais Samia, ndiye aliruhusu watu wawe huru kuujadili muungano, na anakwenda kutupatia katiba mpya, nashauri hili la mkanganyika wa katiba kati ya katiba ya JMT na Katiba ya Zanzibar, pia litarekebishwa, na kwa maoni yangu, dawa pekee ya uhakika na ya kudumu ambayo ni mwarobaini wa kuondoa hii sumu ya ubaguzi wa Utanganyika na Uzanzibari, ni kwenda kwenye serikali moja. Kidonge hicho japo ni kichungu kumeza kwa wenzetu wa Zanzibar, wenzetu nao walazimishwe wameze, waipoteze Zanzibar yao, kama Watanganyika tulivyopoteza Tanganyika yetu, kunakuwa hakuna Tanganyika, hakuna Zanzibar, kuna Tanzania tuu!. Tena kidoge hiki ndio muarobaini au kidoge cha anti bayotiki ya kuzitibu na kuzimaliza kabisa kero zote za muungano.
Wasalaam.
Paskali
Rejea za Mwandishi kuhusu serikali moja.
- Pongezi za Miaka 60 ya Muungano: Twende Kwenye Muungano Kamili wa Ukweli wa Nchi Moja, Serikali Moja na Rais Mmoja? Kero Zote za Muungano Zitayeyuka!
- Suluhisho la Kudumu la Kero Zote za Muungano, na Dawa ya Kutibu Sumu ya Ubaguzi wa Utanganyika na Uzanzibari ni Kuwa na Serikali Moja ya JMT?
- Kama kweli nia ya dhati ni kuimarisha Muungano, then "Twende kwenye Serikali Moja!"
- Je, umefika wakati kutimiza Uzalendo wa kweli wa kwenda kwenye Serikali moja?
