Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
Tukiwa tunaelekea kwenye bunge la katiba, bunge ambalo sehemu kubwa sana ya mjadala utakuwa ni juu ya muungano, kuna kila dalili kwamba mjadala utakaochukua nafasi kubwa utaendelea kuwa ni ule juu ya Muungano, hasa suala la Tanganyika. Dalili ya hili imeonekana pia kwenye mchakato wa katiba mpya ambapo tume ya warioba imeweka wazi kwaba zaidi ya nusu ya wachangiaji walikuwa na maoni juu ya mfumo wa muungano. Katika hali hii, kuna kila dalili kwamba wajumbe watakaopinga Tanganyika watamtumia sana baba wa taifa Mwalimu Nyerere kwamba hata yeye hakuitaka Tanganyika.
Dhumuni la mada yangu ni kujaribu kumchambua na kumwelewa vyema Mwalimu, hasa iwapo angekuwa hai leo, angesimamia upande upi wa hoja ya Tanganyika. Ni imani yangu kwamba kwa kufanya hivi tutapunguza uwezekano wa matuizi mabaya ya jina la Mwaliu katika kupinga hoja ya Tanganyika, ndani ya bunge la katiba lakini pia kuelekea kura ya maoni.
Ili kufanikisha dhumuni hili, ni muhimu tukajadili na kuchambua swali kuu lifuatalo:
Kwa kufanya hivi tutaweza kufanikisha yafuatayo:
*Kubaini hofu ya msingi ya Mwalimu Nyerere juu ya kuirudisha Tanganyika.
*Kubaini iwapo angekuwa hai na katika mazingira ya sasa ya taifa, Mwalimu bado leo hii angekuwa na hofu juu ya kuirudisha Tanganyika.
*Kubaini iwapo ya Mwalimu angekuwa hai, hofu yake juu ujio wa Tanganyika wakati wa sakata la G55 ingekuwa ni ilele miaka 20 baadae.
Kwa kufanya hivyo:
*Tutaweza kuzuia wanasiasa (hasa wa CCM) kwenda kumtumia Nyerere vibaya na visivyo katika kukandamiza matakwa ya wengi juu ya Tanganyika.
*Tutawasaidia wawakilishi wetu kwenye bunge la Katiba wenye uchungu na Tanganyika kupata hoja za kuitetea Tanganyika.
Moja na njia sahihi kwetu za kumwelewa mwalimu nyerere juu ya suala husika ni pamoja na kupitia hotuba zake mbalimbali kama zilivyonukuliwa sehemu mbalimbali. Kwa kufungua mjadala, ningependa nianze na hotuba ifuatayo ya mwalimu aliyoitoa wakati wa sakata la G55 miaka ya mwanzo ya tisini kama ilivyonukuliwa na professor issa shivji in "Let the People Speak:Tanzania Down the Road to Neo-Liberalism" (2006):
Maswali ya msingi yanayofuatia ni kwamba - kwa mtazamo huu wa mwalimu:
*Je ina maana kwamba mwalimu hakuwa na hofu nyingine nje ya ile ya udini, ukabila na ubaguzi?
*Je Mwalimu angekaribisha mjadala wa Tanganyika ili mradi unajadiliwa kama "Political and Democratic issues" na sio religious and tribal issue?
Katika muktadha huu, ni muhimu tukatilia maanani masuala makuu sita:
-Kwanza, katika kipindi chote cha muungano, kati ya Zanzibar na Tanzania Bara, upande ambao umekuwa ukishinikiza zaidi hoja juu ya umuhimu wa kuirudisha Tanganyika ni upande wa zanzibar kuliko wa tanganyika; sababu kubwa nyuma ya hoja hii ni kwamba kwa kuirudisha Tanganyika, wazanzibari wamekuwa wakiamini kwamba hivyo ndivyo ndoto yao ya kuwa na mamlaka yake kamili itatekelezeka.
-Pili, version ya kwanza ya sheria ya mabadiliko ya katiba ilizuia suala la muungano (hivyo Tanganyika) lisijadiliwe katika mchakato wa katiba chini ya tume ya Warioba. Ni pale baada ya wazanzibari kukata muswada huo mbele ya waziri sitta zanzibar kwa kuuchoma moto ndio serikali ya JMT ikaamua kugeuza msimamo wake wa awali uliozuia suala la muungano lisijadiliwe.
-Tatu, tukiangaloa hoja ya mwalimu juu ya udini na madai ya Tanganyika, ni upande wa Tanzania bara ndio wenye waislau na wakristo wengi kuliko upande wa zanzibar lakini hadi sasa, kuna ushahidi ulio wazi kwamba madai ya watanzania bara juu ya haja ya kuirudisha Tanganyika yanasukumwa na hoja nyingine nje kabisa ya uislamu na ukristo na badala yake hoja zinajengwa kwa misingi ya self determination kama mmoja ya mshirika wa muungano, misingi ya kiuchumi (usawa katika gharama za kuendesha muungano) na demokrasia (mfumo wa muungano utokane na maoni ya walio wengi).
-Nne, kwa mara ya kwanza tangia muungano uzaliwe, wananchi wamepewa fursa ya kutoa maoni yao juu ya aina ya mfumo wa muungano wanaoutaka, na kwa mujibu wa tume ya warioba, pande zote mbili za muungano zimependelea zaidi kurudi kwa Tanganyika.
Tano, katika kikao cha OAU kilichofanyika Julai 1964 jijini Cairo, Misri, kikao hicho ambacho Mwalimu Nyerere alikuwa na ushawishi mkubwa, mwalimu alitoa hotuba iliyojaa hamasa kubwa kuunga mkono mfumo wa shirikisho na sio serikali oja au mbili, na mtazamo huu ndio mwalimu alienda nao katika maandalizi na hatimaye kusaini mkataba wa muungano na zanzibar (1964) ambao kwa mujibu wa content yake ulilenga serikali tatu, na ndio maana tume ya warioba katika utangulizi wa rasimu ya katiba unambulisha jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa mujibu wa mkataba wa muungano uliokuwa na signature ya Mwalimu. Katika hotuba yake kwenye kikao cha OAU Cairo mwaka 1964 kabla tu ya muungano wa Tanganyika na zanzibar, mwalimu alisema hivi (source: "The nature and requirements of african unity in 'African Forum', Volume 1 No. 1 (1965, p.46), na pia kusisitizwa in Nyerere (1966), "Uhuru na Umoja", Oxford University Press, pp 300-304.
Na sita, Mwalimu alinukuliwa na gazeti la Observer la uingereza Aprili 20, 1968 akisema kwamba:
Cc Nguruvi3, Nape Nnauye JokaKuu Jasusi happyfeet, Bongolander, Mag3 Candid Scope MTAZAMO Kimbunga Mkandara Pasco, Zinedine, Zakumi, gfsonwin Kobello, zumbekuu, Kichuguu JingalaFalsafa ZeMarcopolo Ritz, Mzee Mwanakijiji, zomba MwanaDiwani, EMT, AshaDii, ukwelikitugani, na wengine wote niliowasahau;
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Dhumuni la mada yangu ni kujaribu kumchambua na kumwelewa vyema Mwalimu, hasa iwapo angekuwa hai leo, angesimamia upande upi wa hoja ya Tanganyika. Ni imani yangu kwamba kwa kufanya hivi tutapunguza uwezekano wa matuizi mabaya ya jina la Mwaliu katika kupinga hoja ya Tanganyika, ndani ya bunge la katiba lakini pia kuelekea kura ya maoni.
Ili kufanikisha dhumuni hili, ni muhimu tukajadili na kuchambua swali kuu lifuatalo:
Je, hofu kubwa ya Mwalimu juu ya kuirudisha Tanganyika ilikuwa ni nini?
Kwa kufanya hivi tutaweza kufanikisha yafuatayo:
*Kubaini hofu ya msingi ya Mwalimu Nyerere juu ya kuirudisha Tanganyika.
*Kubaini iwapo angekuwa hai na katika mazingira ya sasa ya taifa, Mwalimu bado leo hii angekuwa na hofu juu ya kuirudisha Tanganyika.
*Kubaini iwapo ya Mwalimu angekuwa hai, hofu yake juu ujio wa Tanganyika wakati wa sakata la G55 ingekuwa ni ilele miaka 20 baadae.
Kwa kufanya hivyo:
*Tutaweza kuzuia wanasiasa (hasa wa CCM) kwenda kumtumia Nyerere vibaya na visivyo katika kukandamiza matakwa ya wengi juu ya Tanganyika.
*Tutawasaidia wawakilishi wetu kwenye bunge la Katiba wenye uchungu na Tanganyika kupata hoja za kuitetea Tanganyika.
Moja na njia sahihi kwetu za kumwelewa mwalimu nyerere juu ya suala husika ni pamoja na kupitia hotuba zake mbalimbali kama zilivyonukuliwa sehemu mbalimbali. Kwa kufungua mjadala, ningependa nianze na hotuba ifuatayo ya mwalimu aliyoitoa wakati wa sakata la G55 miaka ya mwanzo ya tisini kama ilivyonukuliwa na professor issa shivji in "Let the People Speak:Tanzania Down the Road to Neo-Liberalism" (2006):
Na katika mazungumzo tuliyonayo, haya tunayozungumza haya, wakubwa wanatuita tuje tuanze maelewano ya kupunguza chuki...wanajua wakubwa kwamba hali tuliyonayo ni ya chuki... Tumechoka na wazanzibari , Tumechoka na wazanzibari...Hayo ndio mazungumzo...Mkiunda serikali ya Tanganyika kutokana na msukumo huu unaowasukumeni wa chuki wa Zanzibari na Uislamu... Nasema mbele yenu, na nasema mbele ya Mungu, kwa msukumo "tumechoka na wazanzibari" na ndani humo humo kuna uislamu, kuna udini ndani..."Tumechoka na wazanzibari" na ndani yake humo umo udini... Nimewatest watu mimi, umo udini mkubwa ndani...kwa sababu wewe ndugu Rais, wewe muislamu, wewe mzanzibari, umefanya madhambi. Basi rais, mzanzibari, muislamu amefanya makosa, mzanzibari, muislamu amefanya makosa. Kwahiyo kuna msukumo, msukumo huu wa uzanzibari na uislamu unaosukuma jambo hili. Kwahiyo nasema nini mimi? Nasema mkijenga, mkiunda serikali ya Tanganyika kutokana na misingi hiyo ya kuchoka na wazanzibari - na chini chini mmechoka na uislamu. Sababu hizo mbili, hizo hizo zitakazoua muungano... Mkiunda serikali ya Tanganyika kwa msukumo huu, muungano utakufa, na muungano ukifa kwa ukabila (maana uzanzibari ni ukabila tu) na udini, sababu hizi hizi mbili za ukabila na udini zitakazoua muungano, zitaua Tanganyika
Maswali ya msingi yanayofuatia ni kwamba - kwa mtazamo huu wa mwalimu:
*Je ina maana kwamba mwalimu hakuwa na hofu nyingine nje ya ile ya udini, ukabila na ubaguzi?
*Je Mwalimu angekaribisha mjadala wa Tanganyika ili mradi unajadiliwa kama "Political and Democratic issues" na sio religious and tribal issue?
Katika muktadha huu, ni muhimu tukatilia maanani masuala makuu sita:
-Kwanza, katika kipindi chote cha muungano, kati ya Zanzibar na Tanzania Bara, upande ambao umekuwa ukishinikiza zaidi hoja juu ya umuhimu wa kuirudisha Tanganyika ni upande wa zanzibar kuliko wa tanganyika; sababu kubwa nyuma ya hoja hii ni kwamba kwa kuirudisha Tanganyika, wazanzibari wamekuwa wakiamini kwamba hivyo ndivyo ndoto yao ya kuwa na mamlaka yake kamili itatekelezeka.
-Pili, version ya kwanza ya sheria ya mabadiliko ya katiba ilizuia suala la muungano (hivyo Tanganyika) lisijadiliwe katika mchakato wa katiba chini ya tume ya Warioba. Ni pale baada ya wazanzibari kukata muswada huo mbele ya waziri sitta zanzibar kwa kuuchoma moto ndio serikali ya JMT ikaamua kugeuza msimamo wake wa awali uliozuia suala la muungano lisijadiliwe.
-Tatu, tukiangaloa hoja ya mwalimu juu ya udini na madai ya Tanganyika, ni upande wa Tanzania bara ndio wenye waislau na wakristo wengi kuliko upande wa zanzibar lakini hadi sasa, kuna ushahidi ulio wazi kwamba madai ya watanzania bara juu ya haja ya kuirudisha Tanganyika yanasukumwa na hoja nyingine nje kabisa ya uislamu na ukristo na badala yake hoja zinajengwa kwa misingi ya self determination kama mmoja ya mshirika wa muungano, misingi ya kiuchumi (usawa katika gharama za kuendesha muungano) na demokrasia (mfumo wa muungano utokane na maoni ya walio wengi).
-Nne, kwa mara ya kwanza tangia muungano uzaliwe, wananchi wamepewa fursa ya kutoa maoni yao juu ya aina ya mfumo wa muungano wanaoutaka, na kwa mujibu wa tume ya warioba, pande zote mbili za muungano zimependelea zaidi kurudi kwa Tanganyika.
Tano, katika kikao cha OAU kilichofanyika Julai 1964 jijini Cairo, Misri, kikao hicho ambacho Mwalimu Nyerere alikuwa na ushawishi mkubwa, mwalimu alitoa hotuba iliyojaa hamasa kubwa kuunga mkono mfumo wa shirikisho na sio serikali oja au mbili, na mtazamo huu ndio mwalimu alienda nao katika maandalizi na hatimaye kusaini mkataba wa muungano na zanzibar (1964) ambao kwa mujibu wa content yake ulilenga serikali tatu, na ndio maana tume ya warioba katika utangulizi wa rasimu ya katiba unambulisha jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa mujibu wa mkataba wa muungano uliokuwa na signature ya Mwalimu. Katika hotuba yake kwenye kikao cha OAU Cairo mwaka 1964 kabla tu ya muungano wa Tanganyika na zanzibar, mwalimu alisema hivi (source: "The nature and requirements of african unity in 'African Forum', Volume 1 No. 1 (1965, p.46), na pia kusisitizwa in Nyerere (1966), "Uhuru na Umoja", Oxford University Press, pp 300-304.
Bara lenye ukubwa wake kamili, moja na lisilogawika, ndilo nataka liwepo. Hii haina maana huku ni kuwa na serikali moja kwa bara lote, katika hali ya kuwa na serikali kuu yenye mamlaka yote. Kinachotakiwa ni kuwa na serikali moja inayounganishwa na nyingi na kuwa na mamlaka katika maeneo fulani. Zaidi ya hapo kunaweza kuwepo na serikali nyinginezo, hizi zikiwa na mamlaka yalio hafifu kidogo, na mamlaka hayo yakiwa yanatokana zaidi na "katiba za ndani na sio kutoka serikali kuu". Hii ni sawa na kusema kuwa afrika mpya inaweza kuwa ni dola ya "shirikisho", ambayo nguvu zake zitagawiwa baina ya serikali kuu na serikali za mataifa washiriki "kwa mujibu wa matakwa ya waanzilishi na vizazi vijavyo".
Na sita, Mwalimu alinukuliwa na gazeti la Observer la uingereza Aprili 20, 1968 akisema kwamba:
Iwapo umma wa zanzibar bila ya ushawishi kutoka nje na kwa sababu zao wenyewe wataona kuwa muungano una hasara kwa uhai wao, sitowapiga mabomu kuwalazimisha. Muungano utakuwa hauna tena sababu ya kuendelea kuwepo iwapo washirika wake wataamua kuukana.
Cc Nguruvi3, Nape Nnauye JokaKuu Jasusi happyfeet, Bongolander, Mag3 Candid Scope MTAZAMO Kimbunga Mkandara Pasco, Zinedine, Zakumi, gfsonwin Kobello, zumbekuu, Kichuguu JingalaFalsafa ZeMarcopolo Ritz, Mzee Mwanakijiji, zomba MwanaDiwani, EMT, AshaDii, ukwelikitugani, na wengine wote niliowasahau;
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Last edited by a moderator: