Wajumbe walikuwa na sababu gani kumuengua Master Jay?

Wajumbe walikuwa na sababu gani kumuengua Master Jay?

Hana tofauti yoyote na Steve Nyerere
 
Wasanii wakiona followers wengi fb na insta wanadhani ndo wapiga kura,kumbe wajumbe hawana hata smartphone,followers wakikuambia gombea unavimba kichwa unadhani unakubalika
Mitaani huwa wanawapita Sana, kumbe ndio wajumbe wenyewe
IMG-20200725-WA0000.jpg
 
Anamuda gani yupo kwenye chama kwanza? wajumbe sio wajinga jua hilo kwanza wanajua kile wanachokifanya maana wao ndio watu wanojua wapi wanachama waonguli huwezi kuibuka ovyo ukapewa kura kirahisi rahisi hivyo.
Kula mkono kwanza🤝 mkuu kama upo sehemu agiza kinywaji nakuja kulipa au sorry utalipa tu maana ntachelewa kuja🤦😜😅
 
Hiyo Picture Ya Mjumbe Kasimama Chooni Hapo Halafu Ulete Mchezo!!😐🤔🤨😑😄😐
 
Wajumbe hawataki longolongo, uwe na degree hata kumi wao wana vigezo vyao bana.....sasa ukikaa kusubiri uwasikie wakipayuka "mkono mtupu haulambwi" basi utakula za uso kila kukicha.
 
Ni takribani wiki na ushee sasa Master Jay kakaa kimya sana na page zake za mitandao ya kijamii zipo kimya zaidi ya wiki.

Master Jay ni msomi mwenye degree ya Uingereza katika fani ya uhandisi na aliwahi kufanya kazi kama engineer kwenye kampuni ya Mobitel (kwa sasa Tigo) ila aliiacha kazi hio yenye mshahara si haba ili aje kuinua sanaa ya Bongo Fleva lakini uzalendo wake nahisi wajumbe wameupuuza kitu ambacho si kizuri.

Pia alijiandaa mapema sana katika ishu ya kutia nia ya kuwa mbunge kwa kunyoa rasta zake.

]
View attachment 1516716
Mkuu, wajumbe sio watu wazuri.
🤣🤣🤣🤣
 
Simu walinipigia,
Sifa zangu kunipatia,
Wakanisihi nitie nia,
Wajumbe sio watu wazuri

Walisema nakubalika,
Nitapita bila shaka,
Kura zao walinipa uhakika,
Wajumbe sio watu wazuri

Mara nyingi tulikutana,
Mipango tuliweka bayana,
Nilipambana usiku na mchana,
Wajumbe sio watu wazuri,

Ukimbini tulipoingia,
Sera kuwamwagia,
Kwa kweli walishangilia,
Wajumbe sio watu wazuri,

Kura zikawekwa mezani,
Kila mtu na yake mkononi,
Walichonifanya wajumbe sikuamini,
Wajumbe sio watu wazuri

Sikupata hata kura moja,
Hata ya wale tuliokuwa pamoja,
Ningejinyonga ningekuwa kihoja,
Wajumbe sio watu wazuri
 
Back
Top Bottom