Song of Solomon
JF-Expert Member
- Aug 5, 2021
- 2,752
- 5,609
Tafakuri Tunduizi kutoka kwa George RWECHUNGURA
LIGI DHAIFU AMA SIMBA DHAIFU?
Twende na hoja ya Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally kuhusu @nbc_premierleague_tanzania msimu huu ni dhaifu.
Tucheze na namba kwa sababu namba hazidanganyi.
TOFAUTI YA KWANZA
Hadi Mei 5, 2021 kulikuwa na mechi 14 zilizotoa tofauti kubwa ya mabao, Mwadui walifungwa mabao mengi mara nne ( 5-1 Vs Ruvu, 5-0 Vs Yanga, 6-1 Vs JKT Tz, 5-0 Vs Simba).
Hadi leo hii, mechi mbili tu zilizotoa mshindi mwenye tofauti kubwa ya mabao (Yanga 4-0 Dodoma Jiji, Prisons 0-4 Azam).
TOFAUTI YA PILI
Msimu uliopita, Simba ilikuwa kileleni na alama 61 baada ya mechi 25 (wastani wa alama 2.44 kwa kila mchezo), nafasi ya pili Yanga walikuwa na alama 57 baada ya michezo 27 (wastani wa alama 2.11)...mkiani (Mwadui) alikuwa na alama 19 katika michezo 28 (wastani wa alama 0.68).
Msimu huu, kinara ana alama 56 katika michezo 22 (wastani alama 2.54), nafasi ya pili alama 43 baada ya michezo 21 (wastani alama 2.05) na mkiani Coastal Union alama 21 baada ya michezo 21 (wastani wa alama 1 kwa kila mchezo).
TAFSIRI
Wastani wa alama kwa kinara umeongezeka kwa alama 0.1 kutoka alama 2.44 msimu uliopita hadi alama 2.54 msimu huu huku mkiani wastani ukiongezeka kwa alama 0.32 kutoka wastani wa alama 0.68 za Mwadui hadi wastani wa alama 1 kwa Coastal Union msimu huu.
TOFAUTI YA TATU
Uwiano wa mabao (goal difference-GD)... walikuwa na GD 48 (wastani mabao 1.92 kwa kila mechi), Yanga GD 24 (wastani wa bao 0.89) na mkiani palikuwa na GD -32.
Msimu huu kinara Yanga ana GD 35 (wastani wa mabao 1.59), Simba GD 25 (wastani wa mabao 1.19) na mkiani Coastal Union ana GD -10.
TAFSIRI
Timu nyingi zimeimarika,lakini data za Simba za msimu uliopita ni bora sana kuliko data za Simba za msimu huu, hivyo ligi imeimarika lakini Simba imedhoofika.
SABABU
Timu vibonde zilishuka msimu uliopita. Mwadui ( 1-5 Ruvu, 0-5 Yanga, 1-6 JKT na 0-5 Simba), JKT (1-6 Mbeya City na 0-4 Simba).
Timu vibonde wa Simba zimeimarika.
Msimu uliopita Simba 4-0 Biashara, Coastal 0-7 Simba na Simba 5-0 Mtibwa.
Msimu huu, Biashara 0-0 Simba, Simba 0-0 Coastal, Mtibwa 0-0 Simba.
HITIMISHO
Namba zinaonesha ligi imeimarika, Simba SC imedhooka
LIGI DHAIFU AMA SIMBA DHAIFU?
Twende na hoja ya Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally kuhusu @nbc_premierleague_tanzania msimu huu ni dhaifu.
Tucheze na namba kwa sababu namba hazidanganyi.
TOFAUTI YA KWANZA
Hadi Mei 5, 2021 kulikuwa na mechi 14 zilizotoa tofauti kubwa ya mabao, Mwadui walifungwa mabao mengi mara nne ( 5-1 Vs Ruvu, 5-0 Vs Yanga, 6-1 Vs JKT Tz, 5-0 Vs Simba).
Hadi leo hii, mechi mbili tu zilizotoa mshindi mwenye tofauti kubwa ya mabao (Yanga 4-0 Dodoma Jiji, Prisons 0-4 Azam).
TOFAUTI YA PILI
Msimu uliopita, Simba ilikuwa kileleni na alama 61 baada ya mechi 25 (wastani wa alama 2.44 kwa kila mchezo), nafasi ya pili Yanga walikuwa na alama 57 baada ya michezo 27 (wastani wa alama 2.11)...mkiani (Mwadui) alikuwa na alama 19 katika michezo 28 (wastani wa alama 0.68).
Msimu huu, kinara ana alama 56 katika michezo 22 (wastani alama 2.54), nafasi ya pili alama 43 baada ya michezo 21 (wastani alama 2.05) na mkiani Coastal Union alama 21 baada ya michezo 21 (wastani wa alama 1 kwa kila mchezo).
TAFSIRI
Wastani wa alama kwa kinara umeongezeka kwa alama 0.1 kutoka alama 2.44 msimu uliopita hadi alama 2.54 msimu huu huku mkiani wastani ukiongezeka kwa alama 0.32 kutoka wastani wa alama 0.68 za Mwadui hadi wastani wa alama 1 kwa Coastal Union msimu huu.
TOFAUTI YA TATU
Uwiano wa mabao (goal difference-GD)... walikuwa na GD 48 (wastani mabao 1.92 kwa kila mechi), Yanga GD 24 (wastani wa bao 0.89) na mkiani palikuwa na GD -32.
Msimu huu kinara Yanga ana GD 35 (wastani wa mabao 1.59), Simba GD 25 (wastani wa mabao 1.19) na mkiani Coastal Union ana GD -10.
TAFSIRI
Timu nyingi zimeimarika,lakini data za Simba za msimu uliopita ni bora sana kuliko data za Simba za msimu huu, hivyo ligi imeimarika lakini Simba imedhoofika.
SABABU
Timu vibonde zilishuka msimu uliopita. Mwadui ( 1-5 Ruvu, 0-5 Yanga, 1-6 JKT na 0-5 Simba), JKT (1-6 Mbeya City na 0-4 Simba).
Timu vibonde wa Simba zimeimarika.
Msimu uliopita Simba 4-0 Biashara, Coastal 0-7 Simba na Simba 5-0 Mtibwa.
Msimu huu, Biashara 0-0 Simba, Simba 0-0 Coastal, Mtibwa 0-0 Simba.
HITIMISHO
Namba zinaonesha ligi imeimarika, Simba SC imedhooka