Wakala wa Meddie Kagere, Mnyarwanda Patrick Gakumba atoa siri nzito za Kocha wa Simba SC Didier Gomez Da Rosa

Wakala wa Meddie Kagere, Mnyarwanda Patrick Gakumba atoa siri nzito za Kocha wa Simba SC Didier Gomez Da Rosa

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
"Huyu Kocha nimejuana nae Siku nyingi hata kabla ya kuja hapo Simba SC. Anafanya mambo ambayo najua yatakuja Kumrudia na ataumbuka kwani hata Mwenyezi Mungu anayaona na atamuadhibu. Ana Chuki Binafsi na Mimi kwakuwa nilikataa Kumpigia Chapuo kwa Ushawishi wangu mkubwa katika Soka la hapa nchini Kwetu Rwanda ili awe Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Rwanda Amavubi ".

" Amehamishia Chuki zake dhidi yangu kwa Mchezaji wangu Meddie Kagere kitu ambacho naona anamuonea sana. Hivi karibuni na hata Sauti yake ninayo nimemrekodi Simba SC wakiitaka nitawapa ambapo alinipigia na Kulalamika kuwa Simba SC haimlipi vizuri kama vile alivyotegemea na kwamba taratibu ameanza Mipango ya kutaka kujiunga na Klabu ya Ismailia ya nchini Misri ".

" Aliyewanyima Simba SC nafasi ya Kufuzu Juzi ni Kocha Gomez kwani nina uhakika kwa ule Ubora wa Nahodha John Boko angeingia Meddie Kagere na kwa ninavyomjua angefunga Magoli hata Mawili tofauti na Mapungufu makubwa aliyoyaonyesha Mshambuliaji Butu Chris Mugalu "

Chanzo: Spoti Leo Radio One
==========

Juzi GENTAMYCINE nilipokuja na ' Post Match Analysis ' yangu hapa juu ya Mechi ya Marudiano ya Simba SC na Kaizer Chiefs FC niliutaka Uongozi wa Simba SC ukae chini na Kocha Gomez kwani nilihisi kuwa alikuwa na Chuki Binafsi na Mshambuliaji Meddie Kagere.

Ninamshukuru sana Wakala wa Mchezaji husika aitwae Patrick Gakumba ambaye muda mfupi tu uliopita akizungumza na Mtangazaji Amri Masare wa Radio One / ITV katika Kipindi Kizuri cha Michezo cha Spoti Leo ameweza kutoa SIRI na Kukamilisha kile ambacho nilikihisi kwa Kocha Gomez.

Simba SC limalizeni hili haraka sana tu.
 
Ikiwa hizi tuhuma ni za kweli, najiuliza simba itafukuza makocha wangapi? Na kwa nini nguvu kubwa ya kocha kufukuzwa hapa bongo inatoka kwa waandishi? Huu utaratibu wa kocha kutumika mwaka mmoja au miwili, kiuhalisia hauufaidishi klabu kabisa..#ninaimaninaGomes#
 
Ikiwa hizi tuhuma ni za kweli, najiuliza simba itafukuza makocha wangapi? Na kwa nini nguvu kubwa ya kocha kufukuzwa hapa bongo inatoka kwa waandishi? Huu utaratibu wa kocha kutumika mwaka mmoja au miwili, kiuhalisia hauufaidishi klabu kabisa..#ninaimaninaGomes#
Namuamini Wakala Gakumba kwa 85%,
 
Kagere amalize muda wake aondoke zake, wakala mpuuzi saana. Kipindi cha Sven alileta shutuma za hivi hivi na sasa analeta hizi pia. Kagere mi mchezaji kama wachezaji wengine tuu . Simba kuna wachezaji wazuri tuu hawachezi na hatuna habari za kipuuzi kama za huyu wakala. Simba ni kubwa kuliko mchezaji , kagere amalize mkataba wake aondoke tuu.

Wakala anajua kagere umri umeenda na hawezi kupata dili nono zaidi kama hachezi . Hivyo analazimisha ili apate chance ili kagere aweze kupata dili la kumalizia career yake either kwa kuongezewa mkataba simba au kwa kupata sehemu nyingine na yote haya hayawezi kufanyika pasipo kagere kucheza. Hivyo huyo wakala analeta hizi stori kumtafutia soko mchezaji wake ( ambacho siyo kibaya) , ila kwa simba sasa anataka kuwayumbisha saana . Uongozi ufanye jambo.
 
Ndugu Sub zinakuwa tano na sio tatu nachokumbuka Simba alifanya sub 3 na zilibaki 2.
Hujajua kanuni za Sub tano, zinavyofanyika kwenye mashindano yale. Sub ni tano ila utaingiza kwa awamu tatu tu, hivyo awamu ya kwa unaweza kuingiza Sub tatu, inayofuata mmoja alafu unamalizia mmoja, ama utaingiza wawili wawili, ama wote kwa mpigo, ilimradi uwagawe kwa awamu tatu.
Hivyo Simba waliingiza Mmoja mmoja kwa awamu tatu, Na kuhesabika wamemaliza Sub.
 
Back
Top Bottom