Binafsi Sijaona kama ni Mzigo wowote kwangu na Kwa mtu yeyote kulipa Tsh 5 katika kila vocha ya 1000 Kama Kodi ili iende kwenye miradi ya maji, barabara,afya n.k
Tunalalamika kupitiliza, tukikuta barabara mbovu malalamiko, changia sh 5 tujenge barabara bado malalamiko eti ni Mzigo.Tulipe Kodi ili tupate haki ya kuilalamikia serikali na kuikosoa.
Sio kwamba tuna umasikini wa hivyo wa kuelemewa na sh 5,10,100 ,ni akili tu za kimaskini.
Kwa wale waliopata kutembelea nchi za huko ulimwengu wa kwanza, watakubaliana na mimi kwamba sisi bado hatulipi Kodi tunafanya mchezo.
Tulipe Kodi Wakuu tuache porojo za kijinga, hii nchi ni yetu itajengwa Kwa jasho letu