Wakati dunia inapigana na ukatili kwa watoto ikiwemo viboko mashuleni, Tanzania ukatili wa watu wazima unafanyika hadharani

Wakati dunia inapigana na ukatili kwa watoto ikiwemo viboko mashuleni, Tanzania ukatili wa watu wazima unafanyika hadharani

Ni

Nimekuzoea kwa maneno yako ya Hovyo..... Hivi kile walichofanya mpaka kupelekea kupigwa Viboko wewe Hamnazo Unaona ni sahihi?
Jitathimin sana, watu kama nyie ndiyo mnasababisha wanawake waonekane hamnazo kumbe siyo kweli
 
Jibu swali kwanza waliochapwa viboko wamefanya kosa gani? Mkuu imekuaje tena Mbona hivyo....?
Inaonekana bado una akili zakikoloni wewe.Mambo yakupiga kama punda yalishapitwa na wakati ndo maana taratibu zakisheria zipo haijalishi mtu kafanya kosa gani.Acha kutetea upuuzi kwasababu tu hayajakukuta.dunia duara.
 
Hahahahaaaa,... unajua jana nimeangalia ile clip nikajichukulia ndio mm asee yule mama ananichapa bakola aseee angekula RKO moja akashuka nayo ardhin akizinduka adabu atakuwa nayo.
keyboard warrior, ila ungebananishwa eneo la tukio chini ya vyombo vya usalama, ungekubali yaishe sana sana labda ungeenda kumpiga kipapai
 
Unamaanisha aliechapa ndio ana hadhi waliochapwa hawana hadhi?

Swala la utu halina ngazi za cheo, tuhuma walizonazo zinaweza kuwa za msingi na kukutwa na makosa na sijasema nawaunga mkono kwa tabia hiyo ila hatua iliyochukuliwa na hao manyampala si sawa na siwez kuunga mkono swala kama hili hata nipelekwe kaburini.

Unajua mambo mengine kabla ya kumhukum mtu jiweke wewe kama mhusika natumain utafanya maamuzi ya hekima, ebu niambie watoto wa hao waliochapwa sasa wapo katika hali gani hapo mtaani.

Jitafakari mwenyewe mambo mangapi unakosea je, na wewe uwajibishwe kwa kucharazwa hadharani?
hatuwezi kuendesha nchi kwa kubembelezana, ukizingua unakula mboko😂😂😂
 
Naskia baadhi ya nchi hata kumnyooshea kidole binadamu mwenzako ni kosa, ila hapa Bongo tunachapana viboko kabisaa
 
Inaonekana bado una akili zakikoloni wewe.Mambo yakupiga kama punda yalishapitwa na wakati ndo maana taratibu zakisheria zipo haijalishi mtu kafanya kosa gani.Acha kutetea upuuzi kwasababu tu hayajakukuta.dunia duara.
Huu Utumbo uliouweka hapa wazazi wako wanajua...?
 
Unarudi nyumbani unamwambia mke wako nimetoka kucharazwa bakora.
Hapana. Ukirudi nyumbani unakuwa mpole, na kama mke wako akikuuliza ni yepi yaliyojiri huko, unamwambia nilipata katatizo kidogo njiani lakini tumeyamaliza huko-huko kiume.
NB: Mtu anaweza kukubali kulambwa njiti kwa kuangalia/kupima yatakayokupata endapo utaghairi bakora (Kupanga ni kuchagua) kwa mfano: Dereva mzembe njiani au anaonesha ubabe barabarani na akajeruhi mtu. Hapo hapo sasa ikatokea Watu wenye hasira kali wakamkamata. Hapo unaonaje akubali bakora au gari litiwe moto na yeye wampoteze au aingizwe katika mchakato wa Sheria (Polisi) ambao utachukuwa mda mrefu, leseni itazuiliwa n.k n.k. si ni bora akubali yaishe na maisha yasonge mbele - kazi iendelee?
Mazingira yanaweza kukulazimisha ukubaliane na matokeo. Hizo habari za kudhalilishwa ni baadaye sana mjomba.(Ni mtazamo wangu tu)
 
Hii tabia ya viongozi kuchapa raia viboko ni udhalikishaji na ukatili unaopaswa kukemewa kwa nguvu zote. Ki tendo cha kumpigia viboko mtu mzima hadharani ni kumshushia thamani na utu wake. Maafa ya kisaikolojia atakaa nayo mtu yule kwa muda mrefu na wengine hatutaelewa wameathirika kiasi gani.

Hivi tukifunga milango na kuwachapa bakora hawa viongozi. Kama wanategemea polisi mpaka polisi wafike tumesha walamba bakora za kutosha. Kutoka hapo tutaheshimiana.

Watoto wa masikini hao mnaowapa elimu bure mna wachapa vya kutosha. Na sasa mmeamua kuwachapa wazazi wao. Shule zinazo jielewa zimesha achana na adhabu za viboko leo mnapiga viboko watu wazima hadharani.

Tukifurahia maafa ya viongozi mnatuona wabaya wakati chuki mnaitengezeza wenyewe.
Nani kachapwa hadharani kwani?
 
Back
Top Bottom