Wakati Jenerali Ulimwengu akiwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Wilaya ilikuwa chafu sana, dampo Kila mahali, barabara mbovu na uhalifu mwingi

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Nakumbuka wakati Jenerali akiwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Wilaya hii iliongoza kwa uchafu Tanzania nzima, malundo ya taka, madampo, barabara chafu, zenye mashimo, usimamizi wa hovyo kabisa wa shughuli za umma na ufisadi ulitamalaki.

Katika utawala wake, hakuna mradi wowote wa maendeleo ulizinduliwa wilaya ya Ilala. Wilaya ilikothiri kwa umangimeza.

Uamuzi wa Mzee Mwinyi ulikuwa ni kumfurusha na kwenda kumtupa singida. Malalamiko yalikithiri kutokana na uongozi usioridhisha.

#Historia
 
Wajibu wa mkuu wa Wilaya ni upi kwa katiba ya mwaka 1977?
 
Chuki binafsi.kwa hiyo unatakaje?
 
Huyo jamaa alikua anajiona kapewa cheo kidogo sana wakati ambition yake ilikua kubwa sana kwenye nchi wala sio yake maana alikuja gunduliwa wala sio raia wa nchi hii. Alikua mkimbizi tu.
 
Halafu anavyojifanya sasa hivi kuwa mkosoaji wa viongozi wengine utafikiri yeye uDC haukumshinda!
 
Mkuu wa wilaya ndiye anaye-allocate hela za miradi eeh?

Unajua kwann alijiuzulu?

Sasa kama kulikuwa na ubadhirifu wa fedha za umma na bado akaendelea kuteuliwa, si udhaifu wa mamlaka za uteuzi? Na kama ni udhaifu wa mamlaka za uteuzi, kwa hiyo unauhabarisha umma kwamba Nyerere na Mwinyi ni viongozi dhaifu kwa kukumbatia mafisadi? Very interesting
 
Huyo jamaa alikua anajiona kapewa cheo kidogo sana wakati ambition yake ilikua kubwa sana kwenye nchi wala sio yake maana alikuja gunduliwa wala sio raia wa nchi hii. Alikua mkimbizi tu.
Ni raia,huo ugunduzi wa mkapa(mmakua wa msumbiji) kwamba ulimwengu siyo raia ni baada ya ulimwengu kuandika ufisadi wa mkapa kwenye gazeti lake la Rai,maana mkapa aliruhusu uwekezaji uwanja wa ndegge DIA wenye Thamani ya beberu 11 ukiacha uwekezaji mwingine wa kipopoma alifanya kiasi Cha kumliza baba wa taifa
 
Askofu wa Kanisa Katoliki Severin Niwemugizi baada ya kuikosoa serikali naye pia walimtuhumu si raia. It's a known trend.
 
Je wakati huo alikuwa ameshapata uraia wa Tanzania au alikuwa bado. Kama alikuwa bado yawezekana hakuwa na uchungu wa nchi
 
Thibitisha au futa kauli hii.
Mods, taarifa zele lengo ovu, linalolenga kuwachafua waliokuwa Viongozi wa zamani wa Mkoa na Jiji la Dar es Salaam, ziambatane na ushahidi wa uthibisho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…