Mwarukuni
JF-Expert Member
- Nov 28, 2012
- 369
- 371
Wakati umebaki kuwa kitendawili...binadamu mpaka leo karne ya 21 tumeshindwa kuufanyia "figisu" angalau tuweze kuUrudisha au kuongeza japo sekunde moja, TUMESHINDWA. Hatuna hayo mamlaka. Ukizaliwa unakuja na "time frame" ambayo hata wewe huijui...
KWa hizo picha kuna mengi ya kujifunza. Ujana ni maji ya moto, tusijisahau tukaona kuwa yatabaki kuwa ya moto milele. Kama yalivyoanza kuwa ya moto taratibu mpaka kufikia kuwa ya moto sana ndivyo hivyo hivyo yatakavyoanza kupoa mpaka kufikia hatua kuwa umoto haufai hata kukandia kidole.
Tukiutumia ujana wetu vizuri, hakika uzeeni hatutopata tabu na wala hatutokuwa na usumbufu kwa jamaa zetu.
Ujana ndio wakati wa kupiga kazi hasa, usichoke wala kupumzika ila pale inapobidi...nguvu zikishapotea yanabaki majuto tu.
Utatizama nyuma kujutia nafasi ulizopoteza na hakika huwezi kurudisha wakati nyuma kuzipata tena...majuto ni mjukuu.
Naamini hao Arnold and Co. wametumia ujana wao vyema kwa kufanya kila walichokipenda, ni wazi kabisa wana machache sana ya kujutia. Sasa ni watu wazima wakitizama nyuma wanatabasamu kwa kumbukumbu nzuri.
KWa hizo picha kuna mengi ya kujifunza. Ujana ni maji ya moto, tusijisahau tukaona kuwa yatabaki kuwa ya moto milele. Kama yalivyoanza kuwa ya moto taratibu mpaka kufikia kuwa ya moto sana ndivyo hivyo hivyo yatakavyoanza kupoa mpaka kufikia hatua kuwa umoto haufai hata kukandia kidole.
Tukiutumia ujana wetu vizuri, hakika uzeeni hatutopata tabu na wala hatutokuwa na usumbufu kwa jamaa zetu.
Ujana ndio wakati wa kupiga kazi hasa, usichoke wala kupumzika ila pale inapobidi...nguvu zikishapotea yanabaki majuto tu.
Utatizama nyuma kujutia nafasi ulizopoteza na hakika huwezi kurudisha wakati nyuma kuzipata tena...majuto ni mjukuu.
Naamini hao Arnold and Co. wametumia ujana wao vyema kwa kufanya kila walichokipenda, ni wazi kabisa wana machache sana ya kujutia. Sasa ni watu wazima wakitizama nyuma wanatabasamu kwa kumbukumbu nzuri.