Wakati vitu vinazidi kupanda bei, Serikali imelipia ndege mpya tano kuimarisha ATCL

Wakati vitu vinazidi kupanda bei, Serikali imelipia ndege mpya tano kuimarisha ATCL

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali imeendelea kuliimarisha Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ili liweze kutoa huduma bora ya usafiri wa anga ndani na nje ya nchi ambapo amebainisha kuwa serikali imefanya malipo ya awali ya ununuzi wa ndege tano.

Japo hawajasema ni lini wamefanya malipo ya ndege hizo, ni muhimu kujiuliza ni kwa nini serikali haijataja mpango wake wa kupunguza ongezeko la bei lililopo ambalo linaongeza ugumu wa maisha.

Ndege mpya kati ya hizo, ndege moja ni aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, ndege mbili aina ya Boeing 737-9, ndege moja aina ya De Havilland Dash 8-Q400, na ndege moja ya mizigo aina ya Boeing 767-300F hivyo kuifanya serikali kuwa na jumla ya ndege mpya 16.

Yes, ni jambo jema kuwa na shirika thabiti la ndege, Je ni sahihi kwa muda huu?
 
Tungejenga uchumi wa ndani kwanza kwa kuwekeza kwa wananchi wa kati na wa chini kupitia mikopo yenye riba nafuu, iki kuanzisha viwanda, kilimo cha kisasa, ujasiriamali, kuboresha mishahara ya wafanyakazi, kuimarisha miundombinu ya barabara, maji, umeme, nk.

Hii mambo ya kununua midege inayo zalisha hasara kila mwaka, ili tu kutafuta umaarufu wa kisiasa! Haikubaliki hata kidogo.
 
Yani kodi zetu zinateketea hivihivi? Yani kwa iyo hela wangeweza kununua hizi vi cassena vipya za kutosha single engine kama zile za kumwagilia pembejeo na pesticides kwenye mashamba makubwa
 
The only easiest and quickest technic to steal public funds ni kufanya procurement kwakuwa utapata payback tofauti na kuboresha maisha ya wananchi kwasababu hawatakupa payback
 
Tungejenga uchumi wa ndani kwanza kwa kuwekeza kwa wananchi wa kati na wa chini kupitia mikopo yenye riba nafuu,
Sawa kabisa Mkuu, lakini hawatakubaliana nawe kwasababu wananchi hawatoi 10% kwa mtoa fedha, hivyo njia rahisi kutuibia ni kwenda kufanya manunuzi
 
The only easiest and quickest technic to steal public funds ni kufanya procurement kwakuwa utapata payback tofauti na kuboresha maisha ya wananchi kwasababu hawatakupa payback
Hizi nondo unazoshusha itakuwa lazima tu una jiwe la mlimani
 
Mwendazake aliacha amesaini mikataba migumu na mibovu na viwanda vya mabeberu vya kutengeneza ndege.

Hakuna namna lazima watekeleze manunuzi ndiyo legacy za mwendazake.

Sent from my SM-J320H using JamiiForums mobile app
 
Badala ya kuwekeza kwenye kilimo wao wanawekeza kwenye mambo ya kipuuzi ambayo hainufaishi nchi kisa tu kuna wanachofaidi wao kama wao.

Hii nchi ina haki ya kuwa masikini na itaendelea kuwa hivyo kadri tutakavyo endelea kuwa na watu kama hawa tulionao kama viongozi. Bure kabisa.
 
The only easiest and quickest technic to steal public funds ni kufanya procurement kwakuwa utapata payback tofauti na kuboresha maisha ya wananchi kwasababu hawatakupa payback
Kudos , thats very deep!
Na kwa kuwa mwendazake aliasisi mfumo haramu wa manunuzi bila kupata baraka ya bunge , ni wazi sasa wamenogewa .
Now viongozi are busy advertising how many new airplanes are added into the atcl fleets regadless hasara zinazopatikana huko.
 
Back
Top Bottom