wakati wa ujauzito,naombeni msaada

wakati wa ujauzito,naombeni msaada

Mtende

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2010
Posts
6,385
Reaction score
7,332
jf dotors naombani msaada
dada yangu alipata ijauzito lakini mimba ilipokua na wiki mbili ghafle alianza kupata period then alipoenda hospitali akaambiwa mimba imeharibika akasafishwa. baada ya muda alipata tena ujauzito pia hali kama ile ile ya mwanzo ikatokea mimba ikaharibika.baada ya kusafishwa alienda hospitali kufanya chekup na aliambiwa kwamba kizazi kipo sawa na hana tatizo lolote

alienda kwenye hospitali nyingine akafanyiwa vipimo dokta akamwambia kwamba ana kifafa ha mimba ambacho kinasukuma mimba na kusababisha itoke

sasa she is in onfusion haelewi afanye nini, kama kuna wataalamu humu naomba mnijuze haya mabo,au kama kuna mtu anamfahamu dokta yeyote ambaye ni bingwa wa mambo hayo please anijuze nitampataje, na je hili tatizo litatibikaje? nahitaji msaada wenu
 
mh kuhusu kifafa cha mimba sijui, ila kuhusu sbb za mimba kutoka ziko nyingi sana, lbd nikuulize baada ya mimba ya kwanza kutoka alivyosafishwa alitumia dawa yoyote? Na je ilichukua mda gani kupata mimba ya 2 baada ya ile ya kwanza kutoka?
 
kifafa cha mimba mara nyingi huanza kujitokeza baada ya 1st trimester (mimba zaidi wiki 12), hivyo sidhani kama ndio sababu yake ya kutoka kwake kwa mimba. Ushauri ni kuwa aanze mapema kabisa (pale tu akikosa siku zake) antenatal clinic ambapo ataonana na madaktari bingwa wa kina mama afanyiwe uchunguzi na kupewa ushauri mapema kabisa
 
jf dotors naombani msaada
dada yangu alipata ijauzito lakini mimba ilipokua na wiki mbili ghafle alianza kupata period then alipoenda hospitali akaambiwa mimba imeharibika akasafishwa. baada ya muda alipata tena ujauzito pia hali kama ile ile ya mwanzo ikatokea mimba ikaharibika.baada ya kusafishwa alienda hospitali kufanya chekup na aliambiwa kwamba kizazi kipo sawa na hana tatizo lolote

alienda kwenye hospitali nyingine akafanyiwa vipimo dokta akamwambia kwamba ana kifafa ha mimba ambacho kinasukuma mimba na kusababisha itoke

sasa she is in onfusion haelewi afanye nini, kama kuna wataalamu humu naomba mnijuze haya mabo,au kama kuna mtu anamfahamu dokta yeyote ambaye ni bingwa wa mambo hayo please anijuze nitampataje, na je hili tatizo litatibikaje? nahitaji msaada wenu

Poleni kwa matatizo.

Katika hayo uliyoelezea hapo sioni kabisa dalili yeyote ya kifafa cha mimba. Hicho si kifafa cha mimba. Pia kifafa cha mimba hakisukumi mimba na kusabibisha itoke. Huyo daktari (kama kweli aliambiwa na daktari) hajui kifafa cha mimba ni nini!

Kama livyokuambia Futota hapo juu, Kifafa cha mimba mara nyimngi huanza baada ya miezi mi3 ya kwanza ya mimba (First Trimester), na huanza kwa presha ya damu kuwa juu (Pregnancy Induced Hypertension) ambayo inaweza kumbatana na miguu kuvimba kupita kiasi (mara nyingine mpaka uso uvimba asubuhi) na kutoa protini kwenye mkojo. Kwa kawaida kina mama wanaohudhuria kliniki ya wajawazito (ANC) huwa wanachekiwa hivi vitu vyote vitatu hivyo ni rahisi kugundua kuwa mama yuko kwenye risk ya kifafa cha mimba (Eclampsia).

Tafadhali mwambie dada akafanyiwe uchunguzi na daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake (Gynaecologist) kabla ya kupata mimba, na aanze ANC mapema pindi apatapo ujauzito.
 
baada ya mimba ya kwanza kutoka na kusafishwa dokta alimpa ntibiotics za kuzuia infections na alipata mimba ya pili baada ya miezi mitatu
 
Poleni kwa matatizo.

Katika hayo uliyoelezea hapo sioni kabisa dalili yeyote ya kifafa cha mimba. Hicho si kifafa cha mimba. Pia kifafa cha mimba hakisukumi mimba na kusabibisha itoke. Huyo daktari (kama kweli aliambiwa na daktari) hajui kifafa cha mimba ni nini!

Kama livyokuambia Futota hapo juu, Kifafa cha mimba mara nyimngi huanza baada ya miezi mi3 ya kwanza ya mimba (First Trimester), na huanza kwa presha ya damu kuwa juu (Pregnancy Induced Hypertension) ambayo inaweza kumbatana na miguu kuvimba kupita kiasi (mara nyingine mpaka uso uvimba asubuhi) na kutoa protini kwenye mkojo. Kwa kawaida kina mama wanaohudhuria kliniki ya wajawazito (ANC) huwa wanachekiwa hivi vitu vyote vitatu hivyo ni rahisi kugundua kuwa mama yuko kwenye risk ya kifafa cha mimba (Eclampsia).

Tafadhali mwambie dada akafanyiwe uchunguzi na daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake (Gynaecologist) kabla ya kupata mimba, na aanze ANC mapema pindi apatapo ujauzito.

asante sana kwa useful advice,hivi dikta mzuri ambaye ni bingwa wa mambo haya naweza kumpata wapi tafadhali nisaidieni maana tumezunguka kila dokta anatupa majibu tofauti so hatuelewi which is which
 
Poleni kwa matatizo.

Katika hayo uliyoelezea hapo sioni kabisa dalili yeyote ya kifafa cha mimba. Hicho si kifafa cha mimba. Pia kifafa cha mimba hakisukumi mimba na kusabibisha itoke. Huyo daktari (kama kweli aliambiwa na daktari) hajui kifafa cha mimba ni nini!

Kama livyokuambia Futota hapo juu, Kifafa cha mimba mara nyimngi huanza baada ya miezi mi3 ya kwanza ya mimba (First Trimester), na huanza kwa presha ya damu kuwa juu (Pregnancy Induced Hypertension) ambayo inaweza kumbatana na miguu kuvimba kupita kiasi (mara nyingine mpaka uso uvimba asubuhi) na kutoa protini kwenye mkojo. Kwa kawaida kina mama wanaohudhuria kliniki ya wajawazito (ANC) huwa wanachekiwa hivi vitu vyote vitatu hivyo ni rahisi kugundua kuwa mama yuko kwenye risk ya kifafa cha mimba (Eclampsia).

Tafadhali mwambie dada akafanyiwe uchunguzi na daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake (Gynaecologist) kabla ya kupata mimba, na aanze ANC mapema pindi apatapo ujauzito.

Maelezo mazuri, naomba kuongezea machache, presha wakati wa ujauzito (pregnancy induced hypertension) hutokea baada ya wiki 20 na endapo mama atakuwa na presha kabla ya hapo hiyo huitwa chronic hypertension,na kuvimba miguu kwa sasa haitumiki kama kigezo cha kifafa cha mimba.
Kama wachangiaji walivyosema ni vizuri kufanya uchunguzi kwa mabingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi kabla na baada ya kupata ujauzito.
 
Maelezo mazuri, naomba kuongezea machache, presha wakati wa ujauzito (pregnancy induced hypertension) hutokea baada ya wiki 20 na endapo mama atakuwa na presha kabla ya hapo hiyo huitwa chronic hypertension,na kuvimba miguu kwa sasa haitumiki kama kigezo cha kifafa cha mimba.
Kama wachangiaji walivyosema ni vizuri kufanya uchunguzi kwa mabingwa wa magonjwa ya wanawake na uzazi kabla na baada ya kupata ujauzito.

asante sana be blessed maana nilikua na wasiwasi sana
 
Damu ya Yesu ni dawa tosha! Kimbilia kwake kwan yy ndiye daktar bingwa wa mabingwa wote! Atafute wa2mish wa Mungu wamwekee mkono nae atapona au hata yy akiamin afunge na kuomba kwa ajil ya hlo.
 
Damu ya Yesu ni dawa tosha! Kimbilia kwake kwan yy ndiye daktar bingwa wa mabingwa wote! Atafute wa2mish wa Mungu wamwekee mkono nae atapona au hata yy akiamin afunge na kuomba kwa ajil ya hlo.
Wewe unatupeleka Samunge...Wengi wameangamia Loliondo kwa akili hizi!
 
Damu ya Yesu ni dawa tosha! Kimbilia kwake kwan yy ndiye daktar bingwa wa mabingwa wote! Atafute wa2mish wa Mungu wamwekee mkono nae atapona au hata yy akiamin afunge na kuomba kwa ajil ya hlo.


that totaly tue
 
Back
Top Bottom