Wakati wapiga kura jimboni kwake wakimkana mchana kweupe tena mbele ya rais, Job Ndugai kuburuzwa kortini June 3 2020

Wakati wapiga kura jimboni kwake wakimkana mchana kweupe tena mbele ya rais, Job Ndugai kuburuzwa kortini June 3 2020

Mtu kati.

Ni moja ya wiki stressful sana kwa Job Ndugai.

Wakati huko jimboni kwake Kongwa wapiga kura wake wakimkana mbele ya mwenyekiti wa chama chake Magufuli, huku kuna wananchi wengine wanamburuza kortini.

Kesi hii inatarajiwa kuanza kusikilizwa tarehe 3 June 2020 katika Mahakama Kuu kwa mujibu wa taarifa hii hapa chini.

Kuteswa (siyo kutesa mind you) kwa zamu..... unaweza kusema hivyo!


Huyo mgogo wacha ashitakiwe, kwa kweli kiburi cha madaraka kimemzidi mno!
 
Hili ni jukwaa huru Mkubwa....

Ina maana humu JF kila member ni aidha CCM ama CHADEMA, right?

Kama unadhani hivyo, nakuhakikishia kuwa, HAUKO SAHIHI kwa 1,500,000%....!!

Kuna watu tuko kinyume na serikali hii na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na John Pombe Magufuli mwenyewe lakini hutatukuta CHADEMA, ACT Wazalendo ama chama chote cha siasa....!!

Grow up mkubwa, acha kuishi ktk UTUMWA na VIFUNGO vya vyama vya siasa....

Penda nchi yako tu, baasi.....!!

Kuwa mzalendo wa nchi yako tu, baasi.....!!

Kumpenda "mtu kiongozi fulani "ama "serikali", it's just an option" isiyo na ulazima wowote....

Serikali na vyama hivi vya siasa vitapita, lakini nchi yako ndiyo hii hii milele, haitapita.....haibadiliki...

Mfano leo hii itokee vyama vyote vya siasa vyote vife, nchi na watu wake yenyewe itakuwapo tu, haitakufa...

Hata ikitokea leo serikali ambayo kwa sasa inaongozwa na John Pombe chini ya CCM, ikalewa POMBE, ikajikwaa na kufa....nchi ya Tanzania na watu wake, itakuwepo tu, haitakufa....!!

Kitakachofanyika ni kutafuta namna nyingine ya kujitawala na kuindesha nchi yetu, yet, maisha yakaendelea bila matatizo yoyote...!!
Kwamba pombe alafu nani alewe pombe mbona sijaelewa mkuu hiyo kauli yako ?[emoji1787][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna nadharia mbili hapa!kwanza 1,kesi hii itamuondolea uhalali wa kuteuliwa na chama kuwa mgombea!2:Atashinda kesi kutokana na nafasi yake na ateuliwe tena kuwa mgombe!!!chagua moja kati ya mawili hapo juu!!
 
Kamtendea mabaya Sana Lissu eti ajui halipo,wakati the same Mukono ajulikani alipo huku wananchi wake wakikosa uwakilishi the same as kwa Lissu still ajafukuzwa
 
Badala ya kuwawaza wapiga kura wake eti anawaza jinsi ya kumshughulikia Lissu anastuka miaka 5 hii hakuna hata choo alichojenga.
 
Wakati mwingine Mungu humshitaki mtu kwa kuwatumia wanadamu
Nadhani nyote hamjui kusoma aliyeshtakiwa ni Job Ndugai au ni Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tofautisha personality na Taasisi. Mnadanganyana.
 
Nadhani nyote hamjui kusoma aliyeshtakiwa ni Job Ndugai au ni Spika wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tofautisha personality na Taasisi. Mnadanganyana.
Mtu mmoja anaweza akawa na majina mengi but hakumaanishi ni watu tofauti.Dr Mbunge Mchungaji mama lkn ni yuleyule
 
Back
Top Bottom