Wakati Watanzania takribani 50 wakiangamia huko Hanang na maelfu wakiachwa majeruhi, Rais wetu na Makamu wake hawako nchini

Rwebo

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2015
Posts
1,418
Reaction score
1,820
Hii ni hali ya hatari. Inabidi Rais akatize kile anachofanya huko Uarabuni aje asimamie mapambano ya uokoaji. Yeye kama Amir jeshi mku wa vikosi vya ulinzi na usalama inatakiwa awe mstari wa mbele akiwa katika ardhi ya Tanzania.

Rudi nyumbani mama utufute machozi kutuma Salaam za pole ukiwa ughaibuni si sawa Rais wangu. Huwa tunaona Marais wenzako wakikatiza ziara zao pindi patokeapo matatizo kama haya nchini mwao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…