"Wakati watu wanalia kuhusu kikokotoo nilikuwa naona kawaida, sasa nimeona ukali wake" Mtumishi aliyeambulia 10M baada ya kustaafu miaka 33 Magereza

Mkuu kwa ng'ombe gharama zitamzidia maana kuna dawa na matunzo mengine yatararua hicho kidogo alichonacho arudi mavumbini alipotoka mapema bora boda ambayo akishanunua akapata vijana wake wa mkataba yeye ni kusebu 70k kila wiki
Mkuu hiyo 70k ni mauzo kwa ujumla hiyo piki piki Una mshauri anunue atakua na faida ya 21k tu kwa wiki . Kwa sababu faida ya boda kwa siku ni elf 3 kama na mia moja hivi
 
Huu ni zaid ya umasikini hii tuite ufukara ..
Serikali kwenye hili inakosea sana.
Wezi/majambazi wachache waliopo serikalini wanaoijinufaisha kwa mali za umma wanawachokoza wabunge wajinga kwa miswada kandamizi ili waipitishe kuwa sheria ije iwaumize wananchi/watumishi kwa faida yao.Mkiiuliza serikali inawajibu wao hawahusiki kabisa muwalaumu wabonge/wabunge wenu.
 
Mara nyingi tunajiona tuko salama, tunafikiri mabadiliko, kanuni, sheria za kigandamizi zinazofanywa na watawala hazituhusu sisi hasa hawa watumishi wa uma; watu wa magereza, wanajeshi, maaskari police, watumishi wa almashauri, walimu, mahakimu n.k.
Ukiwa kijana unajiona kuwa kikokotoo kina husu wazee tu😂😂😂
 
Kwa kupata kwake kiinua mgongo cha shilingi milioni 20 kabla hiyo Saccos yao haijakata milioni 10 ya Deni lake, inaonesha huyo Afisa hakuwahi kufikisha mshahara wa milioni 1 Kwa Mwezi 🙌

Kwa mshahara huo na kama utakuwa na familia ya watoto 4 unaweza ukashindwa hata kujenga nyumba ya kuishi.

Afisa amekumbuka kuanza kuwekeza (kununua shamba aanze kulima) baada ya kustaafu Utumishi 🙌

Suala la kikokotoo vyema lingefanyiwa marekebisho, Bora kutumia kikokotoo cha zamani tu
 
Serikali ya babu imekuwa ya kinyonyaji sana.tukatae kutawaliwa na wakimbizi kutoka Nchi ya nje ya zanzibar.wakimbizi wanakuja kutuhujumu ustawi wa taifa letu la tanganyika.kwa Nini kokokotoo hakiwahusu wa Zanzibar?
 
Noma sana. Tatizo la manjagu ni kuchekeweshwa kuingia kwenye permanent and pensionable!


Poleni makopolo, sajini na staff sajini. Wengi hamtatoboa 25m
 
Ila kapata ndogo sana kuna commissioner wa magereza namjua miaka minne nyuma alipata 200mil. Ka sikosei, Sasa huyo yake hata kama imekatwa sijui imekatwa ngapi mbona ndogo sana hiyo 20 kabla ya kukata 10 ya mkopo?

Miaka hiyo yote hakuwa hata na mil 100? Kikokotoo alikatwa mil 80? Na zinapelekwa wapi? Vip zile za kila mwezi?
 
Unapata kulingana na mshahara wako. Commissioner boss mkubwa huyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…