Tlaatlaah
JF-Expert Member
- May 18, 2023
- 24,665
- 25,388
without sory JošNigga please!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
without sory JošNigga please!
nimekuelekeza jinsi mambo yalivyo, unataka kuleta mambo ya agano la kale hapa. shauri yako kama hutaki kuchukua hiyo, baki hivyo hivyo maana hakuna namna nyingine šJibu swali, mbunge anapitia kikotoo kama huyo mstaafu wa magereza? Swali hili nimeuliza baada ya wewe kusema kila mstqafu anapitia utaratibu HUO.
CCM wakikuona umekwepa msala wa PAYEE.Thank,
Nilijua CCM ni wezi tangu 2005,nikahapa sitalipa Kodi ya PAYE, namshukuru Mungu,
Niliona Bora nijiajiri kuliko kuibiwa
TuliambiwPXMara nyingi tunajiona tuko salama, tunafikiri mabadiliko, kanuni, sheria za kigandamizi zinazofanywa na watawala hazituhusu sisi hasa hawa watumishi wa uma; watu wa magereza, wanajeshi, maaskari police, watumishi wa almashauri, walimu, mahakimu n.k.
Hutashangaa kusikia kada hizi zikikemea wanaopinga kikokotoo kipya, hutashangaa kusikia wakiwapinga na kuwabeza wanaotaka katiba mpya, hutashangaa wakiwabeza wanaowauliza watawala dhalimu maswali magumu na ya msingi kuhusu kubinafsishwa kwa bandari zetu zote na baadhi ya misitu na hifadhi za wanyama. Kinyume utawasikia wakisema hao wana wivu, hawa ni wapinga serikali, hawa hawana akili, wametumwa na mabeberu, hakika watatuhalibia amani na upendo wa nchi yetu
Sasa leo yamemkuta aliyekuwa mtumishi wa Magereza ndugu Shamte (56) staff Surgent alipojikuta akiambulia kiinua mgongo (malipo ya pension ya kustaafu) cha shilingi 21 millioni badala ya shilingi 55 millioni aliyotarajia baada ya kuitumikia serikali kwa miaka zaidi ya 33.Mstaafu huyo aliyasema hayo baada ya kutembelea ofisi za Magazeti ya mwananchi juzi.
"Najiona mfungwa mtarajiwa baada ya kubakia na shillingi 10 millioni kwani shillingi 10 millioni nyingine zimekatwa baada ya kuwa nilikopa chama cha ushirika wa Akiba na Mikopo cha watumishi wa Jeshi la Magereza" alitoa masikitiko yake bwana Shamte akitumia mfano wa mateso ya watu aliokuwa akiwachunga kila siku wakati akifanya kazi gerezani, kwani anajua machungu ya kuwa mfungwa. "Nilitegemea nikanunue shamba la kulima mazao niweze kujisitili baada ya kustaafu sasa haiwezekani, sioni mbele maisha yatakuwaje" bwana Shamte akitoa sentensi kuashiria kukata tamaa ya maisha
"Wewe ndugu, utaratibu wa malipo ya pensheni halipi CGP, waziri husika au katibu mkuu, utalipwa kulingana na michango yako" hayo ndiyo majibu ya kifupi na kukatisha tamaa aliyopewa mtumishi mstaafu ndugu Shamte kutoka kwa wakuu wake baada ya kupata ujumbe wa kiasi atakacholipwa.
Swali la kujiuliza ni, je ? tuko akina Shamte wangapi? akina shamte ambao tunakubali kila kitu watawala wanachopitisha kwa manufaa yao, akina shamte tunaokuwa wa kwanza kuwanyooshea vidole wale wachache wenye akili timamu na uthubutu wa kuhoji haya mabadiliko dhalimu kwa niaba na manufaa yetu, utasikia hawana akili hao, utasikia wamechanganyikiwa hao, nakwambia utasikia wametumwa na wazungu , mabeberu. Wengi wetu tunafikili madhara ya sheria dhalimu , mabadiliko kandamizi haya hayatuhusu sisi, yanawahusu wale tu wanaolalamika.
Hakika bwana shamte amekumbuka shuka wakati kunakucha , amekumbuka jinsi alivyokuwa akiwadharau waliokuwa wakipinga kikokotoo kipya na pengine alishiriki kuwahadhibu walipopelekwa gerezani alikokuwa akifanya kazi, hakika alimalizia kwa kutubu na kusema "Wakati watu wanalia kuhusu kikokotoo nilikuwa naona kawaida,sasa nimeona ukali wake.
Swali la msingi ni, Je...? wewe na mimi tumejifunza nini katika kisa mkasa hiki cha mstaafu Shamte?
Mkuu yaani uliajiriwa ukatumikia miaka kibao siku ya kustaafu hukupata kitu?Si Bora hata huyo kapata m10 yake. Wengine hata Senti hatukupewa na tunaambiwa tutafute ajira as if wanajua malengo yangu.
Nigga brain is dead and rotten.Nigga please!
Hela ya kila mwezi (pension) unaipata kwa miaka 12 tu kisha inakoma.Hiki ndo kinaendelea tanzania hii?
Kwa hiyo ile ya kila mwezi nusu mshahara wa mstaafu haipo tena? Mbona maumivu.
Mimi niliachaga ualimu nikaenda kusoma kitu nilichokuwa napenda, ingawa nilisota mitaani ila sikuwahi kujuta kuacha ualimu, nilikuwa nauchukia kumbe bora niliuacha.
Mama yangu aliumia sana mimi kuacha ualimu eti nimekosa mshahara wa kila mwezi, eti walimu wanajenga mapema eti itakuwaje?
Nikamwambia mama wewe omba niwe hai, wakati ukifika nitakuwa nakutumia hela bila kusubiri mwisho wa mwezi, na ndivyo ilivyo kwa sasa baada ya msoto wa miaka kama 8.
Wakati nikiwa mwalimu kila mwezi nikifata mshahara nanunua mazagazaga, namtumia mama basi ilikuwa furaha yake kila mwezi mazaga zaga yakishushwa barabarani, basi mashoga zako wanamuonea wivu.
Nilipo acha kazi aliumia eti koz niliyo soma sitopataga kazi nani atamuhudumia? Ni kweli baada ya chuo sikupata kazi.
Yaani kwa ufupi nilipo acha kazi nikaenda kusoma kozi nyingine mshahara ukakatwa, mateso yakaanza ahaaa shoga yangu mama yangu anaumia balaa.
Mungu hana choyo jpm (rip) akatumbua wenye vyeti feki, wenye vyeti halali tukaanza kuwa na dhamani, hata private, ndo kazi ikapatikana, ambayo ni uhuru na ninacho kipata sio kusubiri kikokotoo.
Shoga yangu sasa nyumbani tukiwa tunapiga stori anasema dah waalimu wana maden dah, ila wana mikopo nabaki nacheka, mimi hela ya kusubiri kila mwezi siiwezi.
Hicho kikokotoo kitanikuta nikiwa hai? Kula hela yako ukiwa hai.
Hapana mkuu inakoma ukifa kwa PSSSF.Hela ya kila mwezi (pension) unaipata kwa miaka 12 tu kisha inakoma.
Hongera kwa kujiongeza. Tanzania pagumu kwa wengi na neema kwa wachache at the cost of many.
Mfuko ni mmoja.Hapana mkuu inakoma ukifa kwa PSSSF.
Hii kauli naikumbuka sana...Si Bora hata huyo kapata m10 yake. Wengine hata Senti hatukupewa na tunaambiwa tutafute ajira as if wanajua malengo yangu.
Mimi ni mstaafu.Mfuko ni mmoja.
Mimi naongea sio stori ya kijiweni. Ndugu yangu aliyestaafu kaambiwa wanalipwa kwa miaka 15 tu.
Commissioner general of prisonCGP kirefu chake nini?
protocal na viapo kwenye swala la maisha yako binafsi... yani uumie na familia iteseke utuliee kisa protocal na viapo ningekuwa mwajiriwa wa serekali lazima ningekuja kuacha kazi nisingekubali kustafu kwenye uzee huku mustakabari wa maisha yangu upo ktk mfumo wa watu furani never.HIVI nyie mnaowasema askari,mnazijua protocal na viapo vyao?au mnajisemea tu...brabrabra
Wa miaka ya nyuma haiwahusu. Imeanza kwa waliostaafu kuanzia mwaka wa fedha mpya. Lakini kwa ninavyojua siasa za nchi hii, si ajabu akaja rais mwingine akafuta au huyuhuyu akafuta miaka ya usoni kisha wakaitumia kama political campaign.Mimi ni mstaafu.
Na wako waliostaafu kabla yangu wanalipwa, nitafuatilia na pia kwa wenzangu
Ili nilete majibu ya kina, ila hii kikotoo ni kibaya sana. Tungejua wanapata kiasi gani kila mwezi pia sababu tumeambiwa, watapata hela nyingi.
Nitafuatilia miaka 60 +15 naona 75 hapokati wengi tunarudisha namba.
Kwa ushauri wangu bora ustaafu miaka 55 unakuwa na nguvu kidogo. Miaka 60 hata upewe 600m akili na mwili umechoka majukumu na hela unawakabidhi ndugu ns watu wengine wakufanyie miradi kinschofuata ni stress tu na kufa mapema.
Ndiyo hivyo mkuu.TuliambiwPX
Mkuu yaani uliajiriwa ukatumikia miaka kibao siku ya kustaafu hukupata kitu?