Wakazi wa Dar kufaidi TAWA-Weekend bash ya kula Nyama Pori zilizochomwa

Wakazi wa Dar kufaidi TAWA-Weekend bash ya kula Nyama Pori zilizochomwa

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
590
Reaction score
807
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Meja. Gen. (Mstaafu) Hamis Semfuko, ameyasema hayo Mkoani Dar Es Salaam 10 Septemba 2022 alipokuwa aliongea na Wanahabari kwenye hifadhi ya pori la akiba la Pande (Pande game reserve).

Amesema Wakazi wa Dar Es Salaam na Tanzania kwa Ujumla Wajiandaye kurudisha Furaha yao kwani TAWA inawaletea Burudani ya "TAWA-Weekend bash" ambapo Watu Watakunywa, Watakula Nyama Pori Watacheza na kufanya Utalii wa ndani kwa Wakati mmoja.

Pori la Akiba Pande ambalo lipo Mkoani Dar Es Salaam kuna vivutio vingi kama:

1.Mimea ya aina tatu ambayo inapatikana Pande pekee dunia nzima

2.Mbega weupe na weusi yaani Black and White Colobus Monkeys.

3.Bonde (Crater) iliyojaa uoto wa asili ndani yake

Shughuli za kitalii zinazofanyika ni pamoja na
1.Camping
2. Kuna sehemu za kukimbi na kutembea
3.Bird watching
4. Utalii wa Picha
5.Kuendesha Baiskeli nk.

TAWA-Weekend bash itawafanya watu wafaidi yote hayo kwani itakuwa ni kitu kinachoendelea kila Wkend.

Kiongozi huyo alikuwa ni mgeni mualikwa kwenye mkutano wa TAWA na wahariri wa vyombo vya habari ikiwa ni jitihada za taasisi hiyo kuendelea kutoa uwelewa wa shughuli mbalimbali Wanazozifanya kwa Watanzania.

 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Meja. Gen. (Mstaafu) Hamis Semfuko, ameyasema hayo Mkoani Dar Es Salaam 10 Septemba 2022 alipokuwa aliongea na Wanahabari kwenye hifadhi ya pori la akiba la Pande (Pande game reserve)...
Hilo pori lipo sehemu gani hapa Dar.
 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Meja. Gen. (Mstaafu) Hamis Semfuko, ameyasema hayo Mkoani Dar Es Salaam 10 Septemba 2022 alipokuwa aliongea na Wanahabari kwenye hifadhi ya pori la akiba la Pande (Pande game reserve)...
Nakumbuka Hamis Kigwangala aliandaa wiki ya Utamaduni wa Mtanzania pale Kijiji cha Makumbusho, akatuahidi kutakuwa na nyama choma ya pofu, swala, nyati na nyama ya mamba.

Alileta kilo hamsini tu za nyati, wakagawiwa wakubwa zikaisha. Haya manenomaneno ya viongozi wa CCM sio ya kuyaamini hata kidogo
 
Back
Top Bottom