Wakazi wa Mbezi kwa Msuguli, Kibanda cha Mkaa, Mbezi Mwisho… tuna wiki mbili tunapata maji machafu ya bomba

Wakazi wa Mbezi kwa Msuguli, Kibanda cha Mkaa, Mbezi Mwisho… tuna wiki mbili tunapata maji machafu ya bomba

NBica

Member
Joined
Sep 13, 2010
Posts
39
Reaction score
36
2f5feeaa-3342-4b96-827c-a0be6689f6b8.jpeg
Uchafu wa Maji ya Bomba kwa Wakazi wa Mbezi kwa Msuguli, Kibanda cha Mkaa, Mbezi Mwisho Kwa Yusuph na Mbezi Mazulu.

Sisi wakazi wa maeneo ya Kimara kwa Msuguli, Kibanda cha Mkaa, Mbezi Mwisho Kwa Yusuph, na Mbezi Mazulu tunakumbwa na changamoto kubwa ya maji machafu kutoka kwenye mabomba.

Kwa takribani wiki mbili sasa, tumekuwa tukipata maji yenye tope badala ya maji safi na salama.
c152c5a6-24ed-443f-a981-323e7dad22d0.jpeg

Hali hii ni hatari kwa afya zetu kwani maji haya yanaweza kusababisha magonjwa ya tumbo, ngozi na hata maambukizi mengine ya bakteria.

Tunaiomba mamlaka husika (DAWASA au wahusika wa usambazaji wa maji) kuchukua hatua za haraka kutatua tatizo hili na kuhakikisha tunapata maji safi na salama kwa matumizi ya nyumbani.

Tunaomba mamlaka zitupatie taarifa rasmi kuhusu chanzo cha tatizo hili na hatua zinazochukuliwa ili kurejesha huduma ya maji safi kwa wakazi wa maeneo haya.

 
Nyinyi mnapata maji? Sisi uku mbezi mtaa wa muungano hatujayaona mwaka mzima sasa
 
Back
Top Bottom