Wakazi wa Nairobi wanatumia malimao kujikinga na Corona

Wakazi wa Nairobi wanatumia malimao kujikinga na Corona

luangalila

JF-Expert Member
Joined
Jan 12, 2014
Posts
6,346
Reaction score
6,928
Pamoja na baadhi ya Wakenya kuwadhihaki majirani zao Tanzania kwa kutumia njia asili za kujikinga na corona mfano matumizi ya malimao, kujifukiza, sasa taarifa ikufikie wakazi wa Nairobi wameanza kutumia njia asili kujikinga na Covid hivyo kupelekea tunda la LIMAO (LEMON) kuadimika na kupanda bei maradufu.

 
Aipate MK254 kwenye file lake please maana ni mbishi! hata kwa sayansi yetu waafrica haiamini hata kidogo. Yeye anaamini Wazungu tu
Anaisoma namba ss iv ananunua limao kwa Ksh 20 mpaka 30.
 
Hehehe mnachekesha, limau nimekua natumia kila siku asubuhi kabla kula chochote kwa miaka kadhaa sasa hata kabla corona haijaja. Kawaida mimi kwa mafua huwa simezi vidonge na kunywa dawa, na sio mimi tu, huku Kenya tunafahamika sana kwenye kuzingatia sana masuala ya afya.

Nimewaambia mara kadhaa sasa kwamba tukiamua kuficha corona kama nyie inafichika tu, maana hadi sasa miezi yote hii hatujafa wengi, hiki kitu kwa namna moja au nyingine hakikuja na nia ya kutugaragaza Waafrika.

Tatizo ni kwamba Kenya hatuwezi kufuata namna ya mnavyofanya mambo huko ya kiujamaa, ambapo watu milioni 60 mnashikiliwa akili na kiongozi, hata wataalam wote hawana la kusema, sisi tumefundishwa kuhoji, huku rais hawezi akaamka mara moja na kufoka foka kwamba corona imeisha na kuchimba mikwara hataki kuiskia ikitajwa, na kuifanya corona iwe kama gonjwa la aibu kwamba mtu akiumwa inabidi kuwa siri ya ndani.

Wakenya tunaweza tukamvuruga rais Uhuru hadi atamani kuihama nchi, sisi tunataka tuhabarishwe hali kama ilivyo, takwimu zitolewe, tupimwe na tuendelee kuchukua tahadhari. Hili ni tatizo la kisayansi haliwezi kutoweka kwa matamko au hasira za rais.
 
hakuna jipyaa apooo kwani miaka yote malimau hayapo kitaa? ebooo!.....
ila uswahilini ndio kumeanza kutisha mazeee dah...wananchi wameanza kushiriki ngono zembe bila kutumia mipira ya kondomu huku wakijiaminisha kuwa watayashinda magonjwa ya zinaaa na ukimwii!😂 kama walivoishinda deptivo la koronaaa...#tujifukizeee!!
 
Pamoja na baadhi ya Wakenya kuwadhihaki majirani zao Tanzania kwa kutumia njia asili za kujikinga na corona mfano matumizi ya malimao, kujifukiza, sasa taarifa ikufikie wakazi wa Nairobi wameanza kutumia njia asili kujikinga na Covid hivyo kupelekea tunda la LIMAO (LEMON) kuadimika na kupanda bei maradufu.

Wapumbavu wakubwa hawa wamesababisha limao sasa hivi limefikaTsh 700
 
Anaisoma namba ss iv ananunua limao kwa Ksh 20 mpaka 30.
Kenya wana maisha magumu sana. Yaani limao moja ni tsh 430 hadi 640 wakati sisi fungu moja lenye limao zaidi ya tano zilizoshiba ni ksh 47 tu.

Aisee, fursa hiyo, tuwapelekeee wajitibu na corona
 
Yaani wao hadi limao wanapata Tanzania? Sasa kenya wanalima vitu gani?
 
Kenya wana maisha magumu sana. Yaani limao moja ni tsh 430 hadi 640 wakati sisi fungu moja lenye limao zaidi ya tano zilizoshiba ni ksh 47 tu.

Aisee, fursa hiyo, tuwapelekeee wajitibu na corona
Nataman sana kujua nyanya kule wananunua bei gan
 
Pamoja na baadhi ya Wakenya kuwadhihaki majirani zao Tanzania kwa kutumia njia asili za kujikinga na corona mfano matumizi ya malimao, kujifukiza, sasa taarifa ikufikie wakazi wa Nairobi wameanza kutumia njia asili kujikinga na Covid hivyo kupelekea tunda la LIMAO (LEMON) kuadimika na kupanda bei maradufu.


Wamechelewa sana hawa majirani zetu , wanywe pia chai ya tangawizi na michaichai.
 
Back
Top Bottom