Wakazi wa Ngorongoro, tunawakumbusha tu kwamba hata sisi wa maeneo mengine ya Tanzania, kama Kuna maslahi ya umma, tulihamishwa

Wakazi wa Ngorongoro, tunawakumbusha tu kwamba hata sisi wa maeneo mengine ya Tanzania, kama Kuna maslahi ya umma, tulihamishwa

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Hili sio jambo la ajabu, sasa hivi kuna watu wanapisha SGR, kuna watu wanahamishwa kupisha upanuzi wa barabara, ujenzi wa sekondari, vyuo vikuu, stendi ya magufuli watu waliipisha, stendi ya nyamhongolo mwanza, ujenzi wa migodi.

Upanuzi wa viwanja vya ndege Mwanza na DSM, watu waliipisha, ujenzi wa makao makuu Dodoma, watu wamepisha na wanafidiwa.

Hata nyie ni sehemu ya Tanzania, mnahamishwa na mnafidiwa. Hapo kuna maslahi ya umma.

The Land Act.
The Village Land Act.
Land Acquision Act.
Zinasema ardhi ni Mali ya umma wa Tanzania, sio Mali ya wamasai. Mdhamini ni Rais, Umma ukihitaji ardhi, basi anayenyanganywa anafidiwa.

Umma una maslahi na utalii, unawaondoa, na unawafidia.

Wagogo wangekataa kutoa ardhi, ikulu ya chamwino ingejengwa? Mloganzila Ile hospitali ingejengwa? Bugando Hospitali ingejengwa? Hii miji mikubwa inapimwa na kupendez kwa sababu wakazi wa asili walikubali kuachia ardhi.

Kwa mujibu wa sheria sisi ni wapangaji katika ardhi, ndio maana tunalipa Kodi ya ardhi Kila mwaka. Mmiliki wa ardhi ni umma, Rais ni mdhamini. Umma umeamua kuwapa eneo jingine.

Hizi hifadhi mnazosikia maeneo mengine ya nchi, sisi pia tulihamishwa, hata Bunda na Busega, Kuna kipande kidogo sana ambacho watahamishwa ili kupisha njia ya wanyama kunywa maji ndani ya ziwa Victoria.

Haiwezekani, Ngorongoro iwe kwa ajili ya wanyama! Binadamu watoke humo
20220610_203653.jpg
 
Umetaja kuhamishwa kupisha miradi ya maendeleo.

Hawa hawahamishwi kupisha mradi wa maendeleo.

Bali wanafukuzwa kupisha waarabu wa Oman wakawinde na kubeba wanyama hai.

Hiyo ndio tofauti iliyopo.
 
Umetaja kuhamishwa kupisha miradi ya maendeleo.

Hawa hawahamishwi kupisha mradi wa maendeleo.

Bali wanafukuzwa kupisha waarabu wa Oman wakawinde na kubeba wanyama hai.

Hiyo ndio tofauti iliyopo.
Sisiemu hoyeee
 
Umetaja kuhamishwa kupisha miradi ya maendeleo.

Hawa hawahamishwi kupisha mradi wa maendeleo.

Bali wanafukuzwa kupisha waarabu wa Oman wakawinde na kubeba wanyama hai.

Hiyo ndio tofauti iliyopo.
Nitashukuru kama utatoa uthibitisho kuwa wanahamishwa kupisha waarabu wakawinde. Hata hivyo naunga mkono wao kuhamishwa kwa maslahi ya wanyama na mbuga yao.
 
Umetaja kuhamishwa kupisha miradi ya maendeleo.

Hawa hawahamishwi kupisha mradi wa maendeleo.

Bali wanafukuzwa kupisha waarabu wa Oman wakawinde na kubeba wanyama hai.

Hiyo ndio tofauti iliyopo.
Hiyo ndio akili yako finyu tulivunjiwa nyumba zetu kupisha miundo mbinu na hao wamasai ni watanzania na ardhi ni mali ya serikali na lengo ni kutunza mbuga za wanyama kwa maslahi ya umma wahame tu kama wengine anavyohamishwa.
 
Hili sio jambo la ajabu, Sasa hivi Kuna watu wanapisha SGR, Kuna watu wanahamishwa kupisha upanuzi wa barabara, ujenzi wa sekondari, vyuo vikuu, stendi ya magufuli watu waliipisha, stendi ya nyamhongolo mwanza, ujenzi wa migodi. Upanuzi wa viwanja vya ndege mwanza na Dsm, watu waliipisha, ujenzi wa makao makuu Dodoma, watu wamepisha na wanafidiwa

Hata nyie ni sehemu ya Tanzania, mnahamishwa na mnafidiwa. Hapo Kuna maslahi ya umma.
Umesema vizuri, kuna mliohamishwa kupisha SGR, kuna waliohamishwa kupisha upanuzi wa barabara.

Sasa tuambieni, Wamasai wanampisha nani?
 
Umetaja kuhamishwa kupisha miradi ya maendeleo.

Hawa hawahamishwi kupisha mradi wa maendeleo.

Bali wanafukuzwa kupisha waarabu wa Oman wakawinde na kubeba wanyama hai.

Hiyo ndio tofauti iliyopo.
Unao ushahidi ukatuletea hapa?
 
Wamasai wanapisha shughuli za ustawi wa hifadhi wamekuwa wengi kwa idadi yao,nyumba ndani ya hifadhi na idadi ya mifugo ni kubwa katika eneo la ngorongoro,hao wamasai wamejengewa nyumba huko Handeni na pia watalipwa fidia za nyumba zao baada ya kuondoka,malori na mabasi watapelekewa kuwasafirisha wao,vitu vyao na mifigo yao.
 
Hii serikali imekuwa ya kisengerema sana.yaani wanathamini mwekezeji uchwara aje aanze kuwinda wanyama wetu.kumbe ile ziara ya royo to a Dubai ndio walikubaliana haya kuja kufukuza watu ili wanufaike waarabu.waananchi hatutakubali.lazima tukiwashe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wamasai wameshaamua Jambo lao. Wako tayari kufia juu ya ardhi yao kisha mkawachukue mkawazike Kyle mnakotaka kuwahamishia.

Taha wilaya hata moja iliyowahi hamishwa wakazi wake wote. Hayo uliyoyataja sijui kupisha migodi uwanja wa ndege Barabara nk ninsehemu ndogo sana kwenye Wilaya. Isitoshe wakazi wale walisogezwa tu na siyo kuwafukuza.
 
Hoja hii imeungwa mkono!
Serikali ya Tanzania ndiye mmiliki wa ardhi! Wengine hatuna uamuzi wa mwisho!

Na ukiamua imeamuliwa hata ziwekwe siasa za Aina gani watafanya jambo lao!
Kimara, sijui Kipawa, ilikuwa Lukobe huko Kilosa...Ihumwe...Songwe....Mvomero! Waathirika ni Sisi kwa ustawi wa jamii au hifadhi!
 
Mpaka muda huu, sjafahamu ni Kwa nini wa masaai wanahamishwa pahala ambapo wameishi miaka na miaka,

Nguvu kubwa inayotumika kuwahamisha ili kuwepo nini yaani

Maana tunaskia tuu wanapaswa kupisha, wanapisha ili kuwekwe nini ili hali wamekuwepo hapo miaka na miaka...? Kama ni mifugo, mpaka ilishazoeana na wanyama pori

Kuna nini?

Mleta mada umetaja vizuri, Luna watu walipisha ujenzi wa leri, viwanja vya ndege n.k

Si, walikuwa wakiambiwa wanapisha ili kuwekwe kitu Fulani!

Sasa huko umasaini, mbona hata wewe mleta Uzi hujabainisha hayo masilahi ya taifa zaidi ya kufurahia maumivu ya watanzania wenzako!?
 
Back
Top Bottom