Kwanza kabisa siungi mkono stereotypes za kwamba "Wachaga hivi, Wapare vile" ni uvivu wa kufikiri na ubaguzi tu.
Mama Anna Mkapa (née Maro) ni Mchaga, halina ubishi, naifahamu familia yao mpaka kaka yake Dr. Maro aliyekuwa na hospitali kariakoo na kuvamiwa na majambazi miaka kadhaa iliyopita, na mkewe Dr. Maro Violeta Maro aliyekuwa kiongozi wa chama cha netiboli Tanzania. Watoto wake huyu kaka yake ni kina Brian na Peter Maro. Mmoja wa wadogo zake Mama Anna Mkapa ni Ernest Maro. Nawajua personally tangu Mkapa anakaa Mfaume Rd karibu na Olympio Primary School tulivyokuwa tunaenda party kwake tukiwa wadogo, enzi hizo alikuwa Waziri wa utamaduni kama sikosei, sie wadogo.
Contrary to common belief, Mama ana kwa kiasi kikubwa kaingizwa mkenge na Ben, na wala si kweli kwamba Ben kashawishiwa na Mama Anna, Ben ni policy wonk aliye steal show ya Mzee Ibrahim Kaduma mbele ya Nyerere na Henry Kissinger mpaka kumfanya Nyerere ampe wizara nyeti kutoka uhariri wa Daily News,Ben si kichwa cha kushawishiwa na mke kirahisi rahisi, hususan kama mke mwenyewe ni type ya Mama Anna. Mama Anna anapewa mzigo mzito kuliko anavyostahili.
Kosa lake (Mama Anna) pekee lilikuwa kukubali kurudi kwa Ben kwa heshima ya ombi maalum la msuluhishi wao Mwalimu Nyerere mwaka 1995 wakati Nyerere anamuandaa Mkapa kwa urais na Mama Anna alipokuwa amekwishachoka visa vya Benjamin William Mkapa.Kutoka hapo alikuwa anasainishwa mambo mengi kwa minajili ya mfumodume tu.
Benjamin William Mkapa is no Ali Hassan Mwinyi.