hahah eti atachagua Kenya kusomea Kiswahili huko ambako mtu akiugua mnasema amegonjeka basi katika watu kumi ni mmoja tu ndugu yangu ....Suala la kuteka soko ni ishu ya muda , muda utaongea tu usiwe na haraka .Baadaye watu watajua tu ukweli maana uongo hupanda lift bali ukweli hupanda ngazi .
Suala la elimu bora ya madaktari duniani inafahamika India ,sasa nashangaa hizo porojo unazitoa wapi wakati Kenya kwenye ramani ya dunia haifahamiki . Na kama suala la English bora Uganda wanawazidi mbali kama unabisha ingia google utafute nchi zenye kuongea kiingereza kizuri Afrika utapewa orodha kutoka katika vyanzo vinavyoaminika. Lakini wao hawana kelele kama majirani zetu fulani
Mhaya mtu akiugua anatamka kwa kiswahili '' huyu mutu arumwa'' sabuni anaita Sambundi! sasa ni wapi utaelewa kirahisi? ukilinganisha na kugonjeka? Mkuu TZ naijua sana kuliko unavoijua weye! yaani huko tunaingia na kutoka. sema unatokea Mkoa gani nikupe data? Kuna shule Tanzania zinaongea Vilugha tupu! nazijua nimeziishi. km Kiribho, Kongore, shule za msingi .
Kuhusu soko lako!! usijidanganye Muda utaongea lini? semi za kizamani zinakumaliza, eti ''Aliyeko juu mngoje chini'', ni wa kizamani. mpandie hukohuko, mmalizane, sijui ''subira yavuta heri '' wee lini itavuta heri na mimi nina njaa?! utapata madonda ya tumbo bure, wakati unaugulia wenzako wanapiga ndefu! utawapata wapi? unajipa Moyo!
Mtaka cha uvunguni sharti ainame? unajua Muhindi alijibu vipi? ''sharti nyanyua Matanda!''
Sijui semi km ''Harakaharaka haina baraka'' ni tamathali za semi za kikoloni! ili mnyonywe vizuri!! yeye mbona ana haraka ya kwenda mwezini? Nashangaa wewe bado unazikumbatia. Kiburi chetu cha mafanikio ya ngome ya kiswahili Africa, ni sawa na gwaride la Chipukizi jeuri ya chama cha Mapinduzi,wakati uleee! ile siyo dhambi, Dua la kuku halimpati mwewe!
Jeuri/ kibri akishushwi na mtu au watu, zaidi ya Al asma al husna Lit, Allah! Subhaan Wataalh! na tunajua mbinu za kuongea naye atupandishe ngazi za mafanikio! tuna jeuri kwa Lugha yetu! Africa. TZ haina hati milki ya Kiswahili. huo ni ubinafsi uliopitiliza. km hujui Kiswahili ni Kibantu, huna uelewa, au ulisoma st Kayumba- Bongo, (kwanza nini maana ya Bantu nakuuliza) kuna maneno ktk Lugha zote Africa isipokuwa chache sana.
Mfano wa-Sotho wana maneno ya kiswahili km ''Ebwana wee!'' ''tuliza Ghwana!'' mnyongeni, ''Mughaka-(linasadifu kikurya) , Xhosa Baba wanaita Tata, wazanaki wanaita ivoivo, hapo Bongo km wewe mlivo wabinafsi na uelewa mdogo mnaona ni neno lenu! mta taka wayatamke mnavotaka nyie! kugonjeka ni neno la kikamba, linarandana na kiswahili. tuja hapo kwenu neno ''Chogo'' latumika zanzibar tu, wakuja- Mtwara na Moro, MKanja bhuro- Bukoba,
Elimu Bora tunaongelea EAC na Africa, siyo India kwa magabachori wako huko, fungua akili . neno porojo ni hoja hafifu sana iso mashiko! kuteka soko Duniani siyo kazi ndogo kijana, mtangoja sana, tumepitia mitihani mingi, Mashalah! tunauzoefu, njooni mjifunze mpige bao! hamtaki! Oooh!! sisi kenya hatujui kiswahili fasaha! tuwafanyeje sasa?
Mmepata Rais mzuri but still watanzania mna mnanga eti mara hajui Kiingereza! mara kiswahili hajui! Km mimi muongo muulize Barakoa ni nini? angalia thread humu!! ni wazi mlio wengi mna kitamani! ila uwezo! hata wewe unajifanya hamnazo tu lkn moyoni.., angalia wenzako wanavoikubali Kenya wanajibu hoja kwa ufasaha! wewe ptyuuu!
Mkuu Kujua Lugha ya Adui yako zaidi yake, ni sheria ya vita, sisi tunaenda sambamba ili asije kutuangamiza kirahisi, asikutete, si mna JKT huko wewe ulikimbia? na Watanzania mmeingizwa chaka hadharani mara kibao sababu ya ujuaji km huu,
Meridia BIAO iko wapi? DECI, Mv Buttrfly viko wapi? Bandari ya Bagamoyo, RIchmond,nk uliza wakubwa zako ilikuwaje? Mlipigwa za chembe mchana kweupeee! Bazee mkuje kenya yetu hakuna Matata! sisi hata kiswahili cha Congo. SA tunakikubali na tunakitumia, wamekubali usharika, nyie cha Kenya mnakinanga! eti mnajivunia utanzania haya bana!