Wakenya tushukuru Mungu kwa demokrasia yetu, watani wetu wamebanwa hadi wanalia toshaaa, wanakiri kwamba nchi yao sasa imekuwa 'Police State'

Wakenya tushukuru Mungu kwa demokrasia yetu, watani wetu wamebanwa hadi wanalia toshaaa, wanakiri kwamba nchi yao sasa imekuwa 'Police State'

Watanzania sijui tuna matatizo gani, kwahiyo hapa ndio umejibu hoja ya mleta mada. Kwa hali hii tutaendelea kuwa mikia miaka nenda rudi
Achana na hawa wakenya. Watatukoma aisee! Wanamtamani sana rais wetu. Uhulu Kenyatta na laila wameshindwa na nchi ndio wanakuja kujiriwaza hapa kwa folums zetu. Bule kabisa hii mikenya.
 
Hii nayo ni hatari, Civil Society Organisations Director's Forum ambayo ni mkusanyiko wa mashirika 65 ya kitanzania ya haki za kibinadamu na kidemokrasia limeamua kupaza sauti liwe liwalo. Wanalalamika na kulilia dunia kwa kile ambacho wanakiita 'Police State' ambayo mzee mtakatifu kule ikulu ameibuka nayo kwa kukandamiza kabisa upinzani, wanahabari na uhuru wa wananchi wake. Wanasema kwa mwendo huu wa kuminya demokrasia na uhuru wa wapinzani kuwa na vikao vyao, amani ya nchi inavurugwa huku katiba ikinajisiwa na viongozi wanaotawala. Matokeo yake ni wananchi wanaoishi kwa uoga na kujihisi kwamba hawapo huru kwenye nchi yao. Wameangazia sanasana kutupwa selo kwa miezi mitatu kwa kiongozi mmoja wa upinzani, Mr. Freeman Mbowe. Kunani watani wetu watanzania? Mnanikumbusha enzi za Nyayo Kenya. Mbona mmebadilika kiasi hiki? Tuliwajua kwa ustaarabu wenu ila sasa sivyo tena. https://www.africanews.com/2019/04/...n-groups-risks-undermining-peace-in-tanzania/
ni upumbavu wa watu wachache tu wanaojiita wapinzani
 
Nini JPM kaficha? Utawalawa wake ni wa uwazi sana, kila siku ana watumbua mawaziri, wakuu wa polisi nkt tena hadharani...Juzi tu kenyatta kaongea kuhusu mafisadi kwa ubabe....ilibidi afute accout zake zote za social media
Inaonekana huyu Kenyatta ni kipenzi cha watu. Rais wa afrika. Unampenda sana na ndio maana namuona kwa hiyo avatar yako akinywa kahawa moto.
 
Ni ujinga uliopitiliza kwa Mkenya kujiona hata ana chembe ya demokrasia. Watanzania na Wakenya hatujui na hatutakuja kujua demokrasia for one reason tu. Democracy is against our culture. Tutaipamba pamba lakini hiyo demokrasia haipo. Siku ikitokea mtoto wa familia ya Kiafrika akawa ana uhuru na haki ya kumjibu na kumtukana Baba na Mama yake ndipo hapo nitakubali demokrasia imeingia Afrika. Values na behavior za democracy zinakuwa embedded toka kwenye family level kwenda juu. Till then, potezeni pumzi zenu kwenye upumbavu unaitwa democracy ndani ya culture zetu za kiafrika.
Huelewi kabisa demokrasia ni nini wakati ipo wazi kabisa kwenye katiba yenu. Au mfalme mtakatifu alishaandika katiba yake mpya na bado hatujajua?
 
Maneno yako yamenivutia sana!
Umeandika kwa ufasaha!
Nashauri (kama kweli anatumia) bangi ihalalishwe maana Uhuru Kenyata pia anafaa kuwa Rais wa East Africa (kilimanjaro liwe jina la nchi hii mpya)
Na awe rais wa AFRICA Ndoto ya Nyerere, Kwame na Lumumba itimie.
Hapo ulipotaja cha Arusha ndio sasa umetia ukakasi. [emoji1] Ila freshi tu, nimekuelewa. Umoja wa taifa la Kenya kisiasa ndio itakuwa legacy kuu ya rais Uhuru Muigai Kenyatta, hilo nalo sio siri.
 
Ni kana kwamba demokrasia huliwa. Sisi watanzania hatubabaishwi na lolote. Haijalishi kama leadership tulio nayo ni autocratic. Tunalisha Africa nzima. Tuna miradi mingi kuliko nchi zote duniani. Hamna kiongozi afrika anayependwa kama rais wetu.most peace country in world. The only unite republican in universal.We ahead to Kenya.
Msituchezee nyie manyang'au we giants of Africa.
[emoji16][emoji16][emoji23][emoji23]...waah

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huelewi kabisa demokrasia ni nini wakati ipo wazi kabisa kwenye katiba yenu. Au mfalme mtakatifu alishaandika katiba yake mpya na bado hatujajua?
Hata katiba yenu imeainisha yote hayo lakini bado wanasiasa na wananchi wanazivunja bila kufikishwa mahakamani. Demokrasia kwa Waafrika ni foreign na it will always be foreign hadi vizazi kama viwili vipote.
 
Hata katiba yenu imeainisha yote hayo lakini bado wanasiasa na wananchi wanazivunja bila kufikishwa mahakamani. Demokrasia kwa Waafrika ni foreign na it will always be foreign hadi vizazi kama viwili vipote.
Mihimili yote mitatu Kenya ina uhuru wa kutimiza majukumu yao bila uoga au kushawishiwa. Mahakama zina hadhi na zinaheshimika. Bunge haliendeshwi kwa maagizo kutoka juu. Rais na serikali yake hawawezi wakadhubutu kuteua mazero brain kwasababu waloteuliwa wote lazima wafanyiwe usaili kwanza na wakubaliwe na kamati husika za bunge zote mbili. Raia nao wana uhuru wa kuwasilisha kesi bungeni, za kupinga uteuzi wowote wa rais au maamuzi yeyote ya bunge. Haya yote yanafanywa bila uoga wa kufatafatwa wala kutishiwa na yeyote yule hata awe rais au naibu wake. Bado hatujafikia malengo yetu kama taifa ila safari zote huanza kwa hatua moja. Tutafika tu, Inshaalah.
 
haya wakenya nyingine hii hapa,imagine hapo kenya jubilee ilazimishe primary school students kwenda kusafisha office zake then mtu wa ODM akataze mwanaye halafu district commisoner anaamrisha police wamkamate,hiyo ndiyo NEW TANZANIA najua hamuamini ila ni disaster kwa kifupi tumekatika tumegawanyika kama nchi kuna watoto wapendwa yaani ccm na step kids yaani opposition, ni mateso makubwa tribulation ndugu zetu ,kenya mnayo matatizo yenu tunajua ila sisi tunapoeleka itakuwa the worst tunaongozwa na kichaa a.k,a jiwe,hawezi kushindana hawezi ku argue,ni muoga wa challenges anapenda kusifiwa tu hadi hesabu za serikali anaficha hamtaki CAG sababu anafichua madudu,so far 1 billion dollars hazijulikani zimetumikaje
usafi.PNG
 
haya wakenya nyingine hii hapa,imagine hapo kenya jubilee ilazimishe primary school students kwenda kusafisha office zake then mtu wa ODM akataze mwanaye halafu district commisoner anaamrisha police wamkamate,hiyo ndiyo NEW TANZANIA najua hamuamini ila ni disaster kwa kifupi tumekatika tumegawanyika kama nchi kuna watoto wapendwa yaani ccm na step kids yaani opposition, ni mateso makubwa tribulation ndugu zetu ,kenya mnayo matatizo yenu tunajua ila sisi tunapoeleka itakuwa the worst tunaongozwa na kichaa a.k,a jiwe,hawezi kushindana hawezi ku argue,ni muoga wa challenges anapenda kusifiwa tu hadi hesabu za serikali anaficha hamtaki CAG sababu anafichua madudu,so far 1 billion dollars hazijulikani zimetumikaje
View attachment 1067271
Eti kuosha ofisi za CCM? Kwani kuna sheria ambayo inawalazimisha watu kukubali kuosha ofisi za CCM?
 
Hapo ulipotaja cha Arusha ndio sasa umetia ukakasi. [emoji1] Ila freshi tu, nimekuelewa. Umoja wa taifa la Kenya kisiasa ndio itakuwa legacy kuu ya rais Uhuru Muigai Kenyatta, hilo nalo sio siri.
Cha arusha ndio talk of the world! Au hukusikia ya home boy Obama? Au yab boss wa Tesla?

We support our brethren "Burning spear"
 
Boss umebofya hiyo link hapo na ukasoma taarifa yenyewe? Au umetangulia tu kutupia comment ya kishabik? Hii ni sifa mbaya sana kwa nchi yenu. Wakenya tumeishi kwenye hali kama hiyo ya 'police state' chini ya utawala wa rais mstaafu Daniel Arap Moi, almaarufu Nyayo. Usitamani kuyaona yale ambayo sisi tuliyashuhudia. Wazazi wetu wakivamiwa usiku wa manane na kuzabwa makofi, huku wakinyanyuliwa juu kwa juu na kutupwa kwenye landcruiser na kutawacha tukijiuliza kama ndio itakuwa siku yetu ya mwisho ya kuwaona kwa macho yetu mawili.
Hao walioandika ni tatizo la njaa ndo linawasumbua. Wameandika andiko, ili wapate hela lazima waandike hayo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom