Wakenya wametupiga bao sana kwenye uwekezaji nchini

Wakenya wametupiga bao sana kwenye uwekezaji nchini

Watu wengine wa ajabu sana. Huku tunahimiza nchi za nje wake kuwekeza. Wakija (Kenya) mnasema tumepigwa. Mbona hamsemi hivyo kuhusu uwekezaji wa UK, South Africa au Mauritius? Magufuli aliharibu sana ajili za watu!
Wakenya mbwembwe tu hakuna kitu wanaishi maisha magumu kupita kiasi nusu ya ardhi yenye rutuba inamilikiwa na familia ya kenyata, hapo nairobi wanamiliki msitu mkubwa sana walipojenga kiwanda cha maziwa, hyo familia inamililki mahoteli, mabenki, kampuni za bima, shule, viwanda, mashamba, redio, tv stations, etc, uchumi wa kenya unamilikiwa na asilimia 0.5 ya wakenya wengi wao wakiwa ni wanasiasa, asilimia inayobaki ni mafukara wa kutupwa.
 
Mkuu makampuni mengi ni ya uchochoroni, ambayo Yana fahamika hayazidi ata 50, anaweweseka na makampuni ya kulipa watu laki na nusu ahahahahahaha
Na nikwambie ukweli mtupu mkuu wangu 'ielewemitaa', shida inaanzia kwenye vikampuni hivyo vya mfukoni.

Hivi ni vikampuni vya wakubwa huko huko Kenya.

Hivi vikampuni vya mfukoni vinawapa shida wao kwelikweli, vinasumbua sana katika mambo ya rushwa wanaiita "tenderpreneur" huko kwao.

Vikampuni hivi ndivyo wanavyovitumia wakubwa walio serikalini na kwenye mashirika yao kufisadi hela ya serikali na misaada inayotolewa nchini humo.

Ukisikia 'scandal' zinazohusiana na uagizaji wa mahindi kwa mfano, kila mwaka nchi hiyo inapokumbwa na njaa, ni vikampuni hivyo ndio vinara wa kuvuruga taratibu zote za manunuzi ya kawaida. Ni hivyo hivyo na uagizaji wa sukari, kama ilivyokuwa mwaka juzi, hata tukapiga marufuku/tukaongeza ushuru kwa bidhaa zao zinazozalishwa kutokana na sukari, kama biskuti, icecream na pipi,n.k.; lakini wakalalamika kama watoto wadogo.

Juzi tu hapa, miezi michache iliyopita, wakapata misaada toka nje kupambana na COVID-19, wakubwa hawakuchelewa na vikampuni vyao, wakakwapua misaada hiyo kwa tenda magumashi zilizofanyika KEMSA (shirika lao la kununua na kusambaza vifaa vya tiba)

Ulishamsikia Gavana wao wa Kirinyaga, aliyewahi kuwa waziri wa vijana na ambaye sasa ni Gavana wa Kirinyaga Binti mzuri mzuri wa Kikuyu - Anne Waiguru. Yeye kasambaratisha mfuko wa kuwahudumia vijana akiwa waziri, na hakuna lolote lililofanyika.

Hii ni mifano michache tu ya hawa watu na vikampuni vyao wanavyovileta hapa.

Hatari iliyopo kwetu, wanaleta tabia zao hizi hapahapa, ndiyo maana sasa unawasikia akina Muhongo na wenzake huko Bungeni wakipiga kelele juu ya umeme wa gesi.

Tuwe waangalifu sana. Mambo haya yalishaanza kuota mizizi wakati wa Kikwete; inawezekana sasa wakaanzia walipoachia waliposambaratishwa na Marehemu Mgufuli.
 
Tumeyataka Wacha Watunyooshe
Na sasa watafikisha makampuni 1,000+

Watajaa kama Wachina.
Waje tu, watupatie hata kazi za ulinzi na kusafisha ofisi na kuwaoshea magari

Maana sisi tumezubaa tu.
🤣🤣🤣
 
Wale mamilionea Mia tano aliowazalisha Jiwe wapelekwe Kenya wakawekeze .
Wakuu

Kenya ina jumla ya kampuni 529 zinazoendesha shughuli zake nchini Tanzania ambapo zimewekeza Dola za Marekani Bilioni 1.7 na zimeajiri watu 56,260.

Tanzania sisi sasa tuna kampuni 30 tu. Je, tumekwama wapi kama Nchi?

Nini kifanyike? Waalimu, Wahudumu katika hoteli nyingi ni Wakenya. Wapi wizara zetu na wale watoa maamuzi wanaweka mkakati wa pamoja juu ya hili?
 
Kuhusu wakenya kutuzidi WATANZANIA ni kwa sababu sisi hatuna juhudi za kuthubutu kuanza kitu, pia hotels nyingi wanawaajiri coz kiingereza chao lipo juu, pia elimu yetu haiandai watu kujitegemea kila anayemaliza chuo anataka kuajiriwa mahali hathubutu kujiongeza ili yeye aajiri watu na hii ni kutokana na kuwa hakuna policy nzuri kupromote watu kujiajiri

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Tumeyataka Wacha Watunyooshe
Na sasa watafikisha makampuni 1,000+

Watajaa kama Wachina.
Waje tu, watupatie hata kazi za ulinzi na kusafisha ofisi na kuwaoshea magari

Maana sisi tumezubaa tu.
Inaelekea umekata tamaa sana
 
Kuhusu wakenya kutuzidi WATANZANIA ni kwa sababu sisi hatuna juhudi za kuthubutu kuanza kitu, pia hotels nyingi wanawaajiri coz kiingereza chao lipo juu, pia elimu yetu haiandai watu kujitegemea kila anayemaliza chuo anataka kuajiriwa mahali hathubutu kujiongeza ili yeye aajiri watu na hii ni kutokana na kuwa hakuna policy nzuri kupromote watu kujiajiri

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Kiingereza siyo issue kabisa....Seema sisi ni wavivu kwa Kila kitu...
 
Sisi fedha za umma zinanunua ndege lakini zinaitwa ndege za Lipumba, je mashabiki wa Mbowe watafurahia, ubinafsi wa kipumbavu unatutafuna mkuu
Kwenye mambo ambayo yako serious inabidi nawe uwe serious katika kuchangia mada. Haileti maana kama utachangia hoja kama mtoto wa darasa la tatu. Utaonaje ajabu kuwa nchi haiwezi endelea kama watu ambao wanategemewa kama wewe mawazo yenu ni ya kiumasikini wa akili?
 
Kwenye mambao ambayo yako serious inabidi nawe uwe serious katika kuchangia mada. Haileti maana kama utachangia hoja kama mtoto wa darasa la tatu. Utaonaje ajabu kuwa nchi haiwezi endelea kama watu ambao wanategemewa kama wewe mawazo yenu ni ya kiumasikini wa akili?
Mpuuzi wewe, acha kuishi kwa dada ako siku moja utafungwa pampasi wewe.
 
Uwekezaji wa Kenya nchini Tanzania umeleta ajira 51,000 kwa Watanzania

Uwekezaji wa Tanzania nchini Kenya umewapa ajira 2100.

Kenya ni msaada Kenya ni rafiki mkubwa wa kiuchumi kwa Tanzania.
 
Tanzania iliamua kuweka rehani uchumi wake ili kuwakomboa ndugu zetu wa Uganda waliokuwa wakipitia kipindi cha mateso na ukatili wa kutisha chini ya dikteta Idd Amin Dada.

Kenya waliogopa hata kumgusa Amin.
 
Wkaenyawanavipaji vingisana kuliko TZ
Sisi tumeweka Siasa za maji taka mbele.
Watanzania ni wajuwaji sana ,lakini kielimu tupo chini mno.
Hata hivyi ,hizo biashara zinazosifiwa ni za Wakenya mnajuwa ni wakenya wa jamii ganiwaliowekeza zaidi?
Mii nadhani Wahindi na pengine Wasomali,
sisi Waswahili tunasubiri Vibarua tuu.
Mitaji yetu midogo , Business management zetu ni Poor.
Mswahili kabakia mtu wa Kutumwa tuu na Kulipwaga mishahara.
Inawezekana elimu yetu ndiyo imetufikisha hapa na kuua vipaji vyetu. Nyerere na ujamaa wake pamoja na CCM yake wameua elimu na sioni ni lini tutainuka kielimu.
 
Tanzania iliamua kuweka rehani uchumi wake ili kuwakomboa ndugu zetu wa Uganda waliokuwa wakipitia kipindi cha mateso na ukatili wa kutisha chini ya dikteta Idd Amin Dada.

Kenya waliogopa hata kumgusa Amin.
Sijaelewa nini lengo la mchango wako. Nachojua mimi ni kwamba Nduli Idi Amin Dada alivamia kasakazini mwa nchi yetu huko Kagera na kuchukua sehemu ya nchi yetu kinguvu. Hicho ndicho kilicho sababisha hata sisi kuchukua jukumu la kumtoa.

Hayo mambo ya kumng'oa yeye kutoka nchini kwake hiyo ilitokana na wauganda ambao wengi walikuwa wakimbizi kwetu na walitu support kwenye hiyo vita. Ndiyo maana ilikuwa rahisi na sisi kushirikiana nao.

Haya mambo ya kuweka rehani uchumi wetu, hiyo naona ni issue nyingine.
 
Mpuuzi wewe, acha kuishi kwa dada ako siku moja utafungwa pampasi wewe.
Kuna dada yangu yeyote yule unayemjua ambaye mimi naishi kwake? Nikikuambia kuwa mimi sina dada utaniamini au utanikatalia?

Sishangai hoja zako, huo ni uthibitisho tosha kuwa wewe ni kiumbe wa aina gani? Huna uwezo wa kuchangia hoja ukaeleweka.
 
Wkaenyawanavipaji vingisana kuliko TZ
Sisi tumeweka Siasa za maji taka mbele.
Watanzania ni wajuwaji sana ,lakini kielimu tupo chini mno.
Hata hivyi ,hizo biashara zinazosifiwa ni za Wakenya mnajuwa ni wakenya wa jamii ganiwaliowekeza zaidi?
Mii nadhani Wahindi na pengine Wasomali,
sisi Waswahili tunasubiri Vibarua tuu.
Mitaji yetu midogo , Business management zetu ni Poor.
Mswahili kabakia mtu wa Kutumwa tuu na Kulipwaga mishahara.
"tumeweka siasa majitaka mbele" our current situation hapa nchini. kila kitu siasa
 
Inaelekea umekata tamaa sana
Hapana Wala Sijakata Tamaa,
Hivi Ni lini watanzania watajiamini? Wakenya wanatoa ajira 50+ kwani lazima na Sisi tutoe ajira kama wao? Yaani miaka hii karibu sitini hatuna cha ku-offer tukashindana. dah! This mentality is damning![emoji848]

Si fufanye utafiti tuone nini twaweza kushindana ambacho wao hawana wajameni? Kila nikifiria hii inaniumiza kweli.

Miaka hii yote hatuna kitu unique kama nchi cha kushindana mpaka tufanye kama wao? Wachumi wetu na wataalam wetu mko wapi?

Amsheni kizazi hiki jamani. Mpaka Mwalimu arejee akute bado tunaimba historia tuuu. Hatuwezi kutumia mazingira chotara ya kiuchumi kujiendeleza na Kushindana na Hawa Wakenya??
 
Watanzania tujifariji? unaota tukiamua ku compete wakenya watatafuta pa kujificha.Wakenya wakibisha wamuulize Akamba bus service ambaye kenya ndio giant namba moja kwenye usafiri wa mabasi Alijaribu kuleta mabasi ya route ya kenya Tanania alipigwa mateke na Wenye mabasi watanzania wenye mabasi ya Tanzania kwenda kenya akina Dar express nk hadi akafunga ofisi akarudi kwao kenya kwa kushindwa competition.

Hadi leo mabasi ya watanzania ndi yanatamba route ya Tanzania kwenda kenya na kurudi.Wakenya walikimbia mbio

Shahidi Akamba Bus service wa Kenya
ww umetoa mfano wa mabasi ambao ni small portion sana. ni ndogo sana.
what about nyanja zingine? biashara zingine?
 
Kuna dada yangu yeyote yule unayemjua ambaye mimi naishi kwake? Nikikuambia kuwa mimi sina dada utaniamini au utanikatalia?

Sishangai hoja zako, huo ni uthibitisho tosha kuwa wewe ni kiumbe wa aina gani? Huna uwezo wa kuchangia hoja ukaeleweka.
Hoja huo ujinga wako
 
Back
Top Bottom