Wakenya wanataka fainali ya AFCON 2027 ifanyike kwao

PureView zeiss

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2016
Posts
10,786
Reaction score
35,916
Wakenya wanataka fainali ya AFCON 2027 ifanyikiwe kwao. Rais Ruto ameliagiza Jeshi pamoja na Wizara ya Michezo wajenge uwanja wenye hadhi ya Kimataifa unaobeba watu 60,000 jijini Nairobi tena Ukamilike ndani ya Miaka 2 tu. Tanzania inabidi tuchangamke, fainali ichezewe kwa Mkapa.

Sisi wabongo tukiwa bado kwenye usingizi wa pono wa siasa michezoni pamoja na UJINGA wa akina Haji manara na akina Baba levo wenzetu wakenya wameshatoka usingizini Toka SAA 11 alfajiri. Wakenya wanajua dunia nzima itasimama kuangalia fainali pale Nairobi...

Wizara yetu ya michezo imejipanga vipi na haya mashindano ya AFCON 2027 au bado tunawasubiri wahamasishaji wa soka akina mwijaku?
 
Kuhost hiyo michezo kwa nchi masikini ni gharama zisizo na kipaumbele chochote.

Ni muhimu ku host kama sehemu ya reciprocity diplomacy, huwezi kuwa hosted na wengine kila siku bila ku host, lakini si kitu cha kupigania.

It is more about prestige than profit if you do the cost benefit analysis.
 
Mkuu nadhani kutakuwa na Faida kubwa kuweza ku-host hayo mashindano hasa kupitia

Biashara za hotel/Lodge
Migahawa
Transportation

Japo ni vyema tusi-inject fedha nyingi kujenga miundombinu mipya rather than kuboresha iliyopo
 
Mkuu nadhani kutakuwa na Faida kubwa kuweza ku-host hayo mashindano hasa kupitia

Biashara za hotel/Lodge
Migahawa
Transportation

Japo ni vyema tusi-inject fedha nyingi kujenga miundombinu mipya rather than kuboresha iliyopo
Hakuna lolote. Labda kama u host kwa kujibana na kutia aibu.

Fuatilia mashindano ya Olympic wanavyopata hasara almost everytime.

Kabla ya kuhesabu gharama za ujenzi, Ivory Coast wametumia zaidi ya dola za Kimarekani bilioni moja kuandaa AFCON 2023.

Je, nchi yenye matatizo mengi kama Tanzania ni sawa itumie hela zote hizo ku host michezo?
 
Hivi lile kapu wanalolipitisha umeshawahi kuchangia hata 100? Au haujui kwamba kuna kapu la kuchangia?
 
sio kwa wakati huu ambao pira la bongo limekuwa vibaya mno hao caf hawakuchagui sababu unamaghorofa mengi wanaangalia sehemu watayopata faida na kwa hilo hapa bongo tunaongoza kupenda mpira.

Kuna watu mataifa mbalimbali watasafiri sababu ya simba na yangu tu..

Pia rais wa sasa nae anatua ujasusi wa kiuchumi.
Wakenya Wasahau.
 
Tatizo ni wabahili sana, hawanunui tiketi za kuingia uwanjani.
Wanasababisha hasara kubwa
 
Ndiyo maana AFCON ya 2027 zinaandaa Nchi 3 za Kenya/Tanzania/Uganda

Kwa kuwa na cost sharing itasaidia ku-cut off mzigo wa gharama.

Japo naona una hoja Mkuu

Vyema wataalamu wa Uchumi waingie Kazini waje na paper baada ya kufanya tathmini ya kina
 
Hauoni kama ni sehemu ya kujitangaza ulimwenguni? Wakenya sio wajinga Hadi wapiganie fainali ipigwe Nairobi kwasababu wanajua nchi Yao itaweka history na kuongeza thamani ya utalii..
Zile nguvu zilizotumika kwenye royal tour zingeenda huku
 
Wizara yetu ya michezo imejipanga vipi na haya mashindano ya AFCON 2027 au bado tunawasubiri wahamasishaji wa soka akina mwijaku?

WANAZINGUA.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Sawa tuu,ufunguzi ukifanyika Tzn hakuna shida pia japo sidhani kama CAF watapeleka fainali Kenya Kwa sababu Tzn Ina mashabiki wengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…