Dabaga1998
JF-Expert Member
- Apr 10, 2016
- 994
- 502
Huko Kenya hakuna watanzania wanaofanya kazi
Waje tu wafanye kazi bila vibali tuache chuki na wivu tufanye kazi kwa bidii.
Nakuunga mkono 100%
hilo nalo nenoWoga, uvivu na ujinga ndio kila siku vinatufanya Watanzanzania kuwaogopa. Unaposema fursa za kazi walizoumbiwa Watanzania una hakika na hilo au ni hisia zako zimekutuma?
Wakenya waruhusiwe haraka sana kuja kufanya kazi na biashara, tutafaidika sana na uwepo wao ktk nyanja za elimu, afya na biashara. Fursa za kiuchumi na ajira zitaongezeka na sio kupungua kwa sababu wataleta mapinduzi ya kifkra na ki utendaji hivyo kuchochea ukuaji wa uzalisha na uchumi.
Kitu kimoja tu ni kuwa Wakenya (na wageni wengine wowote) wasipiwe fursa ya kununua na/au kumiliki ardhi. Jambo hilo liwe nje ya mada hiyo.
Mwisho lazima Watanzania tujifunze kuiga mambo mazuri na kukataa mabaya. Mfano vyama vyetu vya ushirika na hata nyingi ya SACCOs bado hazijaleta matokeo kama ambayo wenzetu Kenya wamekuwa wakifaidika. Sasa kwanini tusiige hata jambo dogo kama hilo? Kwa nini tunaona mabaya tu ilihali fursa ya mema ni kubwa zaidi???
Kwa heshima nyingi naomba Rais wetu Mh. John Magufuli ukubali fursa hiyo muhimu. Ikiwezekana ufute mara moja hilo zuio na tufanye kazi badala ya kushindana na kuwaona jirani zetu hao kama maadui.
Hawajui kula na kipofu.Kenyans are more educated and Agressive than Tanzanians.
Kuja kwao huku watakuwa na fursa nyingi zaidi kuajiriwa kuliko sisi.
Nisichopenda zaidi ni wabinafsi na wanatudharau sana watz.
Hapa sijaelewa. Kila kukicha humu jamvini kuna malalamiko ya ukosefu wa kazi kwa wasomi wetu. Kwamba ajira zimezuiwa.
Leo unakuja na stori za wakenya kuja kuchukua ajira hapa pasipo na ajira!!
Maswali yangu ni je.
Kama kweli wakenya wanatamani ajira za kwetu. Ni zipi hizo ambazo watanzania hawajaziona ama hawazitaki ama hawaziwezi?
Je. Kwanini watanzania nao wasiombe kwenda kenya kufanya kazi bila vibali?
Na je watanzania ni dhaifu kushindania kazi wakiwa nchini mwao. Nini tatizo?
Ndiyo sasa hao waafuta ajira mitandaoni waelimishwe wqende huko kenya.Kenya tayari ilishafuta malipo ya work permit kwa wananchi wote wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kwani kuna ubaya gani wa kuwaruhusu wakenya kufanya kazi bila vibali tz. Pengine hii ndiyo itakuwa dawa ya uvivu,kutokuwa na uaminifu, utegaji kazini. Sidhani kama kuzuia ni dawa mbona zamaini ilikuwa hivyo na hakukua na matatizo?Naomba ombi hili limfikie raisi wetu Mh. John Pombe Magufuli.
Kesho Jumatatu Raisi wetu ataanza ziara ya siku mbili ya kiserekali nchini Kenya na atatembelea viwanda mbalimbali ikiwemo kiwanda cha Maziwa cha Brokies Diaries kinachomilikiwa na Familia ya Mzee Kenyatta.Hio sio ishu kwetu kabisa.
Kuna habari za kuaminika Raisi wa Kenya Uhuru Kenyatta ana maombi makuu mawili kwa Raisi Magufuli.
Ombi la Kwanza
Raisi Kenyatta atawasilisha ombi la kuungwa mknono na Tanzania ili waweze kupata uenyekiti wa Africa Union Commission ambapo mwanamama na Waziri wa mambonyq nje wa Kenya Bi Aminq Mohamed anapigiwa chapuo achukue nafasi hiyo.Watanzania hatuna shida na ombi hili na tuko pamoja na Raisi wetu akiamua kuunga mkono jambp hili.
Ombi la Pili
Inasemakana Raisi Uhuru Kenyatta ataomba Tanzania ifute sheria zinazowataka raia wa kenya kuwa na vibali vya kufanya kazi hapa nchini yaani work permits.Hapa ndio kuna shida ikumbukwe tumekua na tatizo la wakenya kuja hapa nchini kuchukua fursa ambazo mungu aliwaumbia watanzania sasa kama Raisi Magufuli ataingia kwenye mtego huo basi sina shaka soko la ajira litavamiwa na wakenya ambao kila siku mate ya yanawatoka na ajira zetu.Najua raisi wetu wewe ni mtu wa kufanya maamuzi ya hapo kwa hapo ila kwa hili naomba usiingie kwenye mtego wa Uhuru Kenyatta.
Watanzania wenzangu naomba tupaze sauti na kuhakikishia ujumbe huu unamfikia Raisi wetu haraka iwezekenavyo tusambaze ujumbe huu whats app,twitter,facebook kila kona jamani.
[HASHTAG]#ChochondeMagufuli[/HASHTAG]
Ndiyo sasa hao waafuta ajira mitandaoni waelimishwe wqende huko kenya.