Wakenya wazidi kumtamani Magufuli, wamtaka Uhuru Kenya kujifunza toka kwake kupambana na Corona

Una hakika? Ushawahi hata kusafiri nje ya mipaka ya Tz? Halafu kama huna uwezo wa Kutafuta hela usisumbue watu humu, huo ni ujinga wako usitusemee.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika watu waliochanganyika sana, wewe upo. Katika maelezo yako umeonyesha kutokupendezwa na kitendo cha Magufuli kutozuia nyumba za ibada, wewe ungependa azuie watu kwenda kumuomba Mungu, wakati unajua fika kwamba Mungu aneamrisha watu kuzidisha maombi katika kipindi kigumu kama hiki, sasa kati ya Magufuli na wewe ni nani anayekwenda kinyuma na matakwa ya Mungu?.

Katika kudhihirisha upoyoyo wako, umemalizia kwa kumuomba Mungu aweze kutusaidia, Mungu huyohuyo ambaye Magufuli anamuheshimu na kutii amri yake ya kuwataka binadamu wasiache kumuabudu hata katika mazingira magumu kiasi gani, Mungu ambaye wewe unashabikia watu kuzikimbia nyumba zake eti kwa kuogopa ugonjwa, mwisho unamuomba huyohuyo Mungu atulinde. Umechanganyikiwa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
neno muhimu katika hoja yangu ni MKUSANYIKO na si MAOMBI. Ila umeamua kuchagua maneno ili kudhihirisha kuwa wewe ni "mwerevu" sana. Kitendo chako cha kuleta maneno ya kashfa kuitana mapoyoyo ni dhahiri ukomo wa fikra zako ndipo unapogota hapo sasa sidhani kama kuna lolote mtu yeyote anaweza sema na wewe ukaelewa. Jifunze kujibu kwa hoja ndugu na si kebehi, si kila mchangiaji hapa ni mwanasiasa ama mkaa kijiweni ambao anakuja hapa kwa ubishani ili mradi uonekane tu unabishana. Kila la heri Bwana Mwerevu acha nikae pembeni na kuchanganyikiwa kwangu pamoja na upoyoyo wangu.
 
Magufuli amakua kituko cha dunia kila nchi inamshangaa kua 'adamant' kiasi hicho......sisi wtznia tutadharauliwa sana kua na Raisi wa nanma hiyo na Bunge kibogoyo, kwa karne hi, kua na Raisi kama hayha Jame au Idi Amini, ni hatari sana kwa Raisi mwenye elimu ya phd.......I doubt his academic credentials

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kwa hapa umeandika ujinga asee!!! Cha umuhimu tumshukuru tu Mungu nchi yetu huu ugonjwa haujaenea kwa kiasi kikubwa. Hakuna mkakati wa maana uliochukuliwa zaidi ya kuambiwa tupige kazi.
Mikakati aliyotumia ndio iliyofanya hadi leo Tanzania ina wagonjwa 14, hakuna vifo na maambukizi yanaongezeka kwa kasi ndogo sana, " Work in silence, let success be your noise".

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Idadi Tanzania imefikia 19, ninajua bado utasema tunaficha, au hizi data sio sahihi hadi pale Tanzania itakapokua na wagonjwa wengi zaidi ya Kenya, kuanzia hapo ndio data za Tanzania zitakubalika kwa wakenya. Sijawahi kuona jamii yenye wivu na roho mbaya kama wakenya, hamkubali kushindwa.

Katika ukabila pia mnasema Tanzania inaficha data, kwamba Tanzania kuna ukabila kuliko Kenya, rushwa hivyo hivyo mnasema Tanzania haisemi ukweli. Failed state kabisa.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bahati mbaya sana hata wakimtamani huyu jamaa yetu hawezi kufanya kazi kwenye nchi yenye katiba kama ya Kenya.
 
Kila mtu anamtukana wa kwake hadi marrkani wanamtukana trump .inabid duniani tulete utaratibu wa kuswipe mataifa .yaan unamkamata mkenya mmoja mnajaza form yeye anakuja tz ww unaenda kenya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kweli watu wanapambana na virus [emoji3083] kwa kuweka maji kila mahali wakati chafya zetu na vikohoo viko nje nje
Sasa huko Zimbabwe wamewekwa lockdown kila sehemu imefungwa kabisa kwa muda wa wiki 3 watu wanalia wanasema watakufa na njaa
Hali yao tunajua na leo wamefungiwa ndani daa tuwaombee ndugu zetu huko maana hiyo ni death sentence kabisa


Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…