Wakili Boniface Mwabukusi aitikia wito wa Jeshi la Polisi, afika kituoni

Wakili Boniface Mwabukusi aitikia wito wa Jeshi la Polisi, afika kituoni

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Wakili Boniface Mwabukusi ambaye ni mmoja wa mawakili wanaowawakilisha walalamikaji kwenye kesi ya kupinga mkataba wa bandari iliyofunguliwa mkoani Mbeya, ameitikia wito wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya baada ya kuitwa (kwa njia ya simu na maandishi) na polisi siku chache zilizopita.Haijajulikana bado kwamba Wakili Mwabukusi anayeongoza jopo la wenzake kuwatetea walalamikaji kwenye kesi hiyo anahojiwa kuhusu nini hasa.
F0-v7G_XgAEdhKw.jpg
 
Wakili Boniface Mwabukusi ambaye ni mmoja wa mawakili wanaowawakilisha walalamikaji kwenye kesi ya kupinga mkataba wa bandari iliyofunguliwa mkoani Mbeya, ameitikia wito wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya baada ya kuitwa (kwa njia ya simu na maandishi) na polisi siku chache zilizopita.Haijajulikana bado kwamba Wakili Mwabukusi anayeongoza jopo la wenzake kuwatetea walalamikaji kwenye kesi hiyo anahojiwa kuhusu nini hasa.
Sawa,mtuletee mrejesho
 
Tunaamini polisi ni sehemu salama kwa raia na Mali zao.

Tunaamini atakuwa salama salimini.
 
Polisi wasumbufu tu.

Hawajui sheria, wanamuita wakili kumuhoji kwasababu amefuata sheria.
 
Maoni yako ni yapi kwenye DP World?
1. Ule ni Mkataba (Nakubaliana na matamshi ya Spika pale Bungeni)

2. Mkataba una mapungufu ya wazi, hasa kwenye vifungu vinavyozungumzia maslahi na ukomo.

3. Serikali inapaswa kuzijibu hoja za wadau na kufanya jambo kabla ya kuendelea na mchakato

4. Sauti za wakosoaji pamoja na wanaounga mkono zisipuuzwe

5. Nchi yetu sasa inaelekea pazuri: wananchi wanakuwa na uthubutu wa kukataa, kwa hoja na sheria, hadharani kuhusu maamuzi au mchakato wa kiserikali. Kinachotakiwa ni kutumika kwa lugha ya staha tu.

6. Naunga mkono uwekezaji pale Bandarini. Lakini, kama taifa, tunapaswa kuwa makini kwa kila kifungu/kipengele cha mikataba ya uwekezaji tutakayoingia.

7. A document is self-speaking. Tunapaswa kuisikia sauti inayozungumzwa na Mkataba wa DP World bila kubishana nayo.
 
1. Ule ni Mkataba (Nakubaliana na matamshi ya Spika pale Bungeni)

2. Mkataba una mapungufu ya wazi, hasa kwenye vifungu vinavyozungumzia maslahi na ukomo.

3. Serikali inapaswa kuzijibu hoja za wadau na kufanya jambo kabla ya kuendelea na mchakato

4. Sauti za wakosoaji pamoja na wanaounga mkono zisipuuzwe

5. Nchi yetu sasa inaelekea pazuri: wananchi wanakuwa na uthubutu wa kukataa, kwa hoja na sheria, hadharani kuhusu maamuzi au mchakato wa kiserikali. Kinachotakiwa ni kutumika kwa lugha ya staha tu.

6. Naunga mkono uwekezaji pale Bandarini. Lakini, kama taifa, tunapaswa kuwa makini kwa kila kifungu/kipengele cha mikataba ya uwekezaji tutakayoingia.

7. A document is self-speaking. Tunapaswa kuisikia sauti inayozungumzwa na Mkataba wa DP World bila kubishana nayo.
Dalili zote ni kuwa Hawa watashupaza shingo. Tunafanyaje?
 
1. Ule ni Mkataba (Nakubaliana na matamshi ya Spika pale Bungeni)

2. Mkataba una mapungufu ya wazi, hasa kwenye vifungu vinavyozungumzia maslahi na ukomo.

3. Serikali inapaswa kuzijibu hoja za wadau na kufanya jambo kabla ya kuendelea na mchakato

4. Sauti za wakosoaji pamoja na wanaounga mkono zisipuuzwe

5. Nchi yetu sasa inaelekea pazuri: wananchi wanakuwa na uthubutu wa kukataa, kwa hoja na sheria, hadharani kuhusu maamuzi au mchakato wa kiserikali. Kinachotakiwa ni kutumika kwa lugha ya staha tu.

6. Naunga mkono uwekezaji pale Bandarini. Lakini, kama taifa, tunapaswa kuwa makini kwa kila kifungu/kipengele cha mikataba ya uwekezaji tutakayoingia.

7. A document is self-speaking. Tunapaswa kuisikia sauti inayozungumzwa na Mkataba wa DP World bila kubishana nayo.
Wewe mwanasheria, hoja zako namba 2 na 4 huoni kama zinakinzana?

Nina wasiwasi hizi hoja zako ume copy & paste somewhere!.

Huwezi kusema sauti za wanaounga mkono ule ubovu zisipuuzwe [hoja # 4], ikiwa umeshakiri mkataba una mapungufu ya wazi { hoja #2} sasa unataka sauti zinazounga mkono ule ubovu zichukuliwe zipelekwe wapi?!
 
Kwa hiyo baada ya Nshalla Ni Mwakabusu.
Bado Shivji, Ulimwengu, Mzee Butiku, Askofu Bagonza, Askofu Munga, Adam Malima, etc.
Mbona kina Kitenge na Zembwela hawaitwi polisi?

Watalia na kusaga Sana.
 
Wakili Boniface Mwabukusi ambaye ni mmoja wa mawakili wanaowawakilisha walalamikaji kwenye kesi ya kupinga mkataba wa bandari iliyofunguliwa mkoani Mbeya, ameitikia wito wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya baada ya kuitwa (kwa njia ya simu na maandishi) na polisi siku chache zilizopita.Haijajulikana bado kwamba Wakili Mwabukusi anayeongoza jopo la wenzake kuwatetea walalamikaji kwenye kesi hiyo anahojiwa kuhusu nini hasa.
Mungu mbariki Mwabukusi .
 
Wewe mwanasheria, hoja zako namba 2 na 4 huoni kama zinakinzana?

Nina wasiwasi hizi hoja zako ume copy & paste somewhere!.

Huwezi kusema sauti za wanaounga mkono ule ubovu zisipuuzwe [hoja # 4], ikiwa umeshakiri mkataba una mapungufu ya wazi { hoja #2} sasa unataka sauti zinazounga mkono ule ubovu zichukuliwe zipelekwe wapi?!
Kuna umuhimu wa kutukana?
Kuna umuhimu wa kumshirikisha Mayalla?
Kama huna hoja zaidi ya matusi, Soma za wenzio na ukae kwa kutulia.
 
Back
Top Bottom