Wakili Boniface Mwabukusi: Hatutaruhusu Mzanzibari kufanya mambo ya ovyo kwenye Mali za Tanganyika

Wakili Boniface Mwabukusi: Hatutaruhusu Mzanzibari kufanya mambo ya ovyo kwenye Mali za Tanganyika

Ni vuguvugu la muda tu. Huwa yanakuja na kupita.

Leo limepita, hasa kwa watu wanaongalia hatua mbili mbele yao! Wasioweza kuona kesho ! Mnashindwa kabisa kuziona nyufa katika sera zenu, na hata Muungano! Siasa za CCM ni kushiba leo! Kumridhisa Rais! Sheria mlizozitunga wenyewe kwa kupiga makofi Pwaa...Pwaa..! Leo mnazifunja kwa takwa la Rais kupitisha anachokitaka!......Akiondoka hata DP World itakua hati hati!.....Hii mentality ya " Huwa yanakuja na kupita" Italicheza taifa hili mduara wa muda mrefu! Inasikitisha sana!
 
Ni busara ipi hasa! Katiba inakuruhusu kutoa maoni yako! Wewe Kuunga mkono DP World mimi kuikataa, Ni busara ipi hiyo unayoisema! Kuwa Raisi ni kuiheshimu katiba! Hivyo kuiheshimu katiba ni kuwa na busara!

Akili za Watanzania na usomi wao unatia mashaka mno!
Ukitaka kujua kuendesha nchi ni busara tazama mataifa yanayoingia vitani ndani afrika hii hii.

Hekima ukiiona kwa mwenzako ni nyepesi sana lakini kuitekeleza kama anavyoitekeleza ndio mtihani mgumu unapoanzia.
 
Leo limepita, hasa kwa watu wanaongalia hatua mbili mbele yao! Wasioweza kuona kesho ! Mnashindwa kabisa kuziona nyufa katika sera zenu, na hata Muungano! Siasa za CCM ni kushiba leo! Kumridhisa Rais! Sheria mlizozitunga wenyewe kwa kupiga makofi Pwaa...Pwaa..! Leo mnazifunja kwa takwa la Rais kupitisha anachokitaka!......Akiondoka hata DP World itakua hati hati!.....Hii mentality ya " Huwa yanakuja na kupita" Italicheza taifa hili mduara wa muda mrefu! Inasikitisha sana!
Mfumo wa CCM upo tangu miaka hiyo ya sabini, sio chama legelege kama baadhi yetu tunavyodhania.
 
Kimejifunza ujasusi huko Russia miaka ile ya Marehemu Paul Sozigwa, uzoefu wa kutosha tu.

Umenichekesha...halafu Sozigwa akafa Maskini!......Uzoefu upi huo! Manipulation of the masses....Rais anayesema ukichagua Wapinzani sileti Maendeleo! Wafanyabisaha wanaogopa kubambikiwa kodi au kunyimwa leseni! Ndio unaita uzoefu! Bila hata aibu......Kweli ikokazi.
 
anachokitafta atakipata. soon atajua maana ya amri jeshi mkuu inamaana gani. ngoja aendelee kufurahisha genge. his days are numbered.

Mwenyewe anajiita wakili msomi.

Tumemuuliza atuonyeshe kipengele japo kimoja kwenye mkataba kinachosema kuwa ardhi hii imeuzwa au bandari imeuzwa,anadhani kuongea Kwa kupayuka na kuvuja jasho basi ndiyo kueleweka.

Yeye anadhani kuongoza nchi ni kama kuuza parachichi hapo mwanjelwa.
 
Umenichekesha...halafu Sozigwa akafa Maskini!......Uzoefu upi huo! Manipulation of the masses....Rais anayesema ukichagua Wapinzani sileti Maendeleo! Wafanyabisaha wanaogopa kubambikiwa kodi au kunyimwa leseni! Ndio unaita uzoefu! Bila hata aibu......Kweli ikokazi.

Teh teh teh

Na mkichagua chadema musahau maendeleo kabisa shenzy.
 
Umenichekesha...halafu Sozigwa akafa Maskini!......Uzoefu upi huo! Manipulation of the masses....Rais anayesema ukichagua Wapinzani sileti Maendeleo! Wafanyabisaha wanaogopa kubambikiwa kodi au kunyimwa leseni! Ndio unaita uzoefu! Bila hata aibu......Kweli ikokazi.
Hata akija rais mwanademokrasia bado kulalamika hakuishi!, lakini cha muhimu ni uhai.
 
Hata akija rais mwanademokrasia bado kulalamika hakuishi!, lakini cha muhimu ni uhai.

Unaona yaliyompata Sozigwa? Hiyo ndio CCM...

Paulo Sozigwa, aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwa Katibu wa Rais Julius Kambarage Nyerere, anakabiliwa na hali ngumu kimaisha.

Sozigwa, ambaye kwa sasa anaumwa ugonjwa wa kupoteza kumbukumbu (Alzheimer), anaishi kwa kudra za Mwenyezi Mungu, akisaidiwa na familia yake na wasamaria wema.

Kutaabika huko kumechangiwa na kutopata malipo ya kiinua mgongo na pensheni, kwa kile kinachoelezwa kwamba ni kutokuwapo kumbukumbu zake za kiutumishi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ofisi Binafsi ya Rais hadi serikalini ambako aliwahi kuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Habari na Utalii.

Katika mahojiano maalumu yaliyofanywa na JAMHURI nyumbani kwake Magomeni Mapipa, Dar es Salaam, mke wa Sozigwa, Monica Kuga, anasema hali yao uchumi ni mbaya kiasi cha kumfanya amtunze mumewe kwa misaada kutoka kwa jamaa na watu waliomfahamu vizuri enzi za utendaji kazi wake.

Wakati Mama Kuga akisema kinachowataabisha ni kukosekana kwa mafao na pensheni, baadhi ya watu waliozungumza na JAMHURI wanasema, kilichomponza mwanasiasa na mtangazaji huyo mahiri wa redio, ni kazi yake aliyoifanya akiwa katika Kamati ya Maadili ya CCM.
 
Uhai unapewa na Mwenyezi Mungu au Rais......au hata CCM.....Sijakuelewa ! na Sijakuelewa zaidi uliposema "Hata akija raisi Mwanademokrasia" Unakiri aliyepo sasa sio mwanademokrasia?
Huwa kuna mada za kulalamika na hofu nyingi wakati nchi inapoongozwa na mbabe.
 
Mfumo wa CCM upo tangu miaka hiyo ya sabini, sio chama legelege kama baadhi yetu tunavyodhania.

Steven,

Nadhani unaathiriwa na " Normalcy Bias" Mambo yatakua hivi hivi! Kama ilivyokuwa jana na juzi na kesho itakua hivyo hivyo! Miaka mingi mmetumia ujinga wa Watanzania, Tume ya Uchaguzi, Polisi, Jeshi nk! Itaendelea kuwa hivyo...... Labda hili kama kuna wenye akili CCM wanaweza kukaa na kutafakari! Lakini Sasa hivi yatatokea Maandamano ya kumpongeza mama! Kama miaka yote inavyofanyika.......Kwa mtu kama wewe inasikitisha unashindwa kuona hata "ulegelege" wa CCM!
DP imefichua ulegelege wa CCM....Imefichua udhaifu wa Muungano.......Haya yote yamekua dhahiri mno kwa watu wanaoona! Naamini hata ndani ya CCM hakuna wajinga wote....licha ya kutetea matumbo yao...kuna baadhi wanajua makosa yamefanyika wapi!
 
Steven,

Nadhani unaathiriwa na " Normalcy Bias" Mambo yatakua hivi hivi! Kama ilivyokuwa jana na juzi na kesho itakua hivyo hivyo! Miaka mingi mmetumia ujinga wa Watanzania, Tume ya Uchaguzi, Polisi, Jeshi nk! Itaendelea kuwa hivyo...... Labda hili kama kuna wenye akili CCM wanaweza kukaa na kutafakari! Lakini Sasa hivi yatatokea Maandamano ya kumpongeza mama! Kama miaka yote inavyofanyika.......Kwa mtu kama wewe inasikitisha unashindwa kuona hata "ulegelege" wa CCM!
DP imefichua ulegelege wa CCM....Imefichua udhaifu wa Muungano.......Haya yote yamekua dhahiri mno kwa watu wanaoona! Naamini hata ndani ya CCM hakuna wajinga wote....licha ya kutetea matumbo yao...kuna baadhi wanajua makosa yamefanyika wapi!
DP haijafichua ulegelege wa CCM, kumbuka wamesaini mikataba mingi yenye kufanana na huu na inafanya kazi mpaka muda huu.

Hizi siasa za vyama vingi zisikudanganye ukadhani kuna mabadiliko makubwa yanayotokea. Kumbuka SSH hana tofauti na Kikwete yaani awamu hii haina tofauti na ile ya nne.

Wangeweza kupita kimya kimya na maisha yakaendelea, kumbuka Samia kachukua pesa nyingi za EU na anaendelea kurudisha kuaminika kwetu kama taifa miongoni mwa taasisi hizi za kimataifa.

Awamu ya JPM ilizifungia vioo hizi taasisi na wao wakatususia masuala ya uendeshaji wa bajeti zetu, alipoingia Samia ikulu akabadili mwelekeo mzima kwanza kwa kumchagua yule Mama Mulamula pale mambo ya nje na pili kuibadilisha wizara nzima ya nje na masuala ya Royal Tour ili kuutambulisha msimamo mpya wa nchi kimataifa ni upi.

Usidhani kwamba CCM wamepoteza ushawishi humu ndani, wameamua kuiachia demokrasia ishamiri.
 
DP haijafichua ulegelege wa CCM, kumbuka wamesaini mikataba mingi yenye kufanana na huu na inafanya kazi mpaka muda huu.

Hizi siasa za vyama vingi zisikudanganye ukadhani kuna mabadiliko makubwa yanayotokea. Kumbuka SSH hana tofauti na Kikwete yaani awamu hii haina tofauti na ile ya nne.

Wangeweza kupita kimya kimya na maisha yakaendelea, kumbuka Samia kachukua pesa nyingi za EU na anaendelea kurudisha kuaminika kwetu kama taifa miongoni mwa taasisi hizi za kimataifa.

Awamu ya JPM ilizifungia vioo hizi taasisi na wao wakatususia masuala ya uendeshaji wa bajeti zetu, alipoingia Samia ikulu akabadili mwelekeo mzima kwanza kwa kumchagua yule Mama Mulamula pale mambo ya nje na pili kuibadilisha wizara nzima ya nje na masuala ya Royal Tour ili kuutambulisha msimamo mpya wa nchi kimataifa ni upi.

Usidhani kwamba CCM wamepoteza ushawishi humu ndani, wameamua kuiachia demokrasia ishamiri.

Hivi unadhani Wabunge wa CCM walikuwa wanajua wanapitisha nini isipokuwa kugonga Meza....! Mbona husemi pia wametuingiza katika mikataba mibovu iliyotuingizia hasara! Si mara moja! mara nyingi!
 
Hivi unadhani Wabunge wa CCM walikuwa wanajua wanapitisha nini isipokuwa kugonga Meza....! Mbona husemi pia wametuingiza katika mikataba mibovu iliyotuingizia hasara! Si mara moja! mara nyingi!
Usiisahau kuiongelea na ile mizuri waliyotuingiza na taifa mpaka kesho linaendelea kufaidika nayo.
 
Usiisahau kuiongelea na ile mizuri waliyotuingiza na taifa mpaka kesho linaendelea kufaidika nayo.

Steven, mingi ya mikataba ni kwenda mbele hatua nne na kurudi nyuma tena hatua tatu! Kwa Mtanzania wa kawaida sijaona lolote......nimezunguka sana vijijini.......Huwa nashindwa kuona kwa kina CCM imefanya nini kubadli mamilioni ya Watanzania wengi.....nadhani unajua pato la mtanzania kawaida! Ndio nikiri mimi sio kipofu kuna patches za hayo maendeleo unayoyasema hapa na pale.....lakini kwangu mimi miaka inavyokwenda CCM inazidi kuwa liability kwa Watanzania wengi.
 
DP haijafichua ulegelege wa CCM, kumbuka wamesaini mikataba mingi yenye kufanana na huu na inafanya kazi mpaka muda huu.

Hizi siasa za vyama vingi zisikudanganye ukadhani kuna mabadiliko makubwa yanayotokea. Kumbuka SSH hana tofauti na Kikwete yaani awamu hii haina tofauti na ile ya nne.

Wangeweza kupita kimya kimya na maisha yakaendelea, kumbuka Samia kachukua pesa nyingi za EU na anaendelea kurudisha kuaminika kwetu kama taifa miongoni mwa taasisi hizi za kimataifa.

Awamu ya JPM ilizifungia vioo hizi taasisi na wao wakatususia masuala ya uendeshaji wa bajeti zetu, alipoingia Samia ikulu akabadili mwelekeo mzima kwanza kwa kumchagua yule Mama Mulamula pale mambo ya nje na pili kuibadilisha wizara nzima ya nje na masuala ya Royal Tour ili kuutambulisha msimamo mpya wa nchi kimataifa ni upi.

Usidhani kwamba CCM wamepoteza ushawishi humu ndani, wameamua kuiachia demokrasia ishamiri.

Steven:

'Usidhani kwamba CCM imepoteza Ushawishi humu ndani"

Kama mna ushawishi mbona mnatumia mabavu mengi kuwepo madarakani! Fanyeni uchaguzi bila nguvu ya Polisi! Bila usimamizi wa ma DED, bila Tume ya Uchaguzi! Balozi Karume kaweka wazi...yamemkuta! Kama kweli mna ushawishi kama unavyosema, basi hamjiamini kabisa!
 
Steven:

'Usidhani kwamba CCM imepoteza Ushawishi humu ndani"

Kama mna ushawishi mbona mnatumia mabavu mengi kuwepo madarakani! Fanyeni uchaguzi bila nguvu ya Polisi! Bila usimamizi wa ma DED, bila Tume ya Uchaguzi! Balozi Karume kaweka wazi...yamemkuta! Kama kweli mna ushawishi kama unavyosema, basi hamjiamini kabisa!
Umeamua kutoona mema ya CCM na ni mengi hivyo sina uwezo wa kubadilisha maoni yako mkuu cassavaleaves.
 
Umeamua kutoona mema ya CCM na ni mengi hivyo sina uwezo wa kubadilisha maoni yako mkuu cassavaleaves.

Steven,

Tukubali kuto kubaliana kiungwana, napata shida mno kuyona haya mengi ambayo CCM imefanyia Tanzania! Maana hata uhuru uliletwa na TANU.....Hata misingi ya mshikamano wa kitaifa ni TANU.....CCM inashindwa hata kueleza ni mfumo gani wa Uchumi tunaoufuata......Kwao (CCM) kuwa madarakani, unaona wazi nchi inaongozwa na utashi wa Raisi aliyeko madarakani! Nguvu ya Raisi wa Tanzania ni kubwa mno! Kuliko Waziri Mkuu Wa Uingereza! Hata Raisi Wa Marekani! Seperation of power iko kwenye makaratasi tu!

CCM imetengeneza mfumo wa " Benevolent Dictator" Raisi wa Tanzania ni "mungu" hata sio nusu mungu! Inatisha sana kwa mtu anayejitambua! Ukitaka kufanikiwa katika nyanja nyingi lazima uiabudu system....au upate baraka za Raisi! Siutaki kabisa mfumo huo! Mawazo tofauti dhidi ya Raisi ni uhaini!

Hivyo nikutakie mema Steven, tukutane katika mada nyingine! Siwezi kubadili msimamo wako, na wewe pia sidhani unaweza kubadili msimamo wangu. SHUKRANI
 
Back
Top Bottom