Wakili Boniface Mwabukusi: Hatutaruhusu Mzanzibari kufanya mambo ya ovyo kwenye Mali za Tanganyika

Wakili Boniface Mwabukusi: Hatutaruhusu Mzanzibari kufanya mambo ya ovyo kwenye Mali za Tanganyika

Tanganyika ni nchi kama ilivyo Zanzibar,hatutaruhusu Mzanzibari kufanya mambo ya hovyo kwenye Mali za Tanganyika,kama ambavyo Mtanganyika hawezi kufanya mambo ya hovyo kwenye Mali za Zanzibar" Wakili Boniface Mwabukusi

Aisee

Wanasemaga mbuyu ulianza kama mchicha!

Mungu atutangulie ktk hili tutavuka salama

Mungu iongoze Tanzania, Mungu Ilinde Tanzania. #TanzaGiza!
Asanteni watangulizi wa JamiiForums.
The leaders of 2morro
 
WAKILI BONIFACE MWABUKUSI;KAMA HAMTATUSIKILIZA,TUTAZUNGUMZA LUGHA MTAKAYOTUSIKILIZA,HATUTARUHUSU MZANZIBARI KUFANYA MAMBO YA HOVYO KWENYE MALI ZA TANGANYIKA.

"Wazee wangu wa Mbeya nipo hapa kuwahakikishia Tanganyika hailiwi tena,tutafuatilia hatua kwa hatua kwenye mikataba ya Mali zote za Tanganyika" Wakili Boniface Mwabukusi

"Mkataba unatakiwa ujisimamie na ujitetee,ila watu wanautetea bila "baseline" za data na facts kwenye mkataba huo,hakuna research wala data, mkataba hauna data ambazo ni measured kisayansi watu wanacheza na maneno tu ambayo hayapo kwenye mkataba" Wakili Boniface Mwabukusi

"Mkataba wa bandari ni batili, chochote kilichofanywa nje ya sheria na nje ya katiba kirekebishwe" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Tanganyika ni nchi kama ilivyo Zanzibar,hatutaruhusu Mzanzibari kufanya mambo ya hovyo kwenye Mali za Tanganyika,kama ambavyo Mtanganyika hawezi kufanya mambo ya hovyo kwenye Mali za Zanzibar" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Ndoa ya Tanganyika na Zanzibar ilikuwa ndoa ya utotoni sasa tumekua tunataka tuongee tukubaliane Mali za Tanganyika ziwe chini ya Mtanganyika na Mali za Zanzibar ziwe chini ya Mzanzibari" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Waziri Mkuu alitudanganya kuhusu kifo cha Hayati Rais John Pombe Magufuli na hajawahi kuomba radhi,na leo anatudanganya kuhusu mkataba wa bandari,akae pembeni kumsaidia Rais" Wakili Boniface Mwabukusi

"Waziri Mkuu atujibu,sheria sura 449 na sheria sura 450 kuhusu Ulinzi wa rasilimali za nchi na kuhusu ushughulikiwaji wa vifungu vyenye utata walizifuata,je vipengele vya mkataba wa bandari vinaoana na vipengele hivi vya sheria yetu" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Waziri Mkuu atujibu,kwa nini bunge linataka kubadili sheria sasa hivi ziendane na mkataba huu wa bandari" Wakili Boniface Mwabukusi

"Tuliibinafsisha Tanesco kwa Net Solution tulipata faida gani na leo Tanesco ya nani? Tulileta watu TRL wakaishia kubeba vichwa vya treni kurudi navyo India,tulifanya hivyo hivyo kwa NBC kuuzwa bei ya kutupwa,na leo mnatuambia mna muujiza kwenye kuibinafsisha bandari" Wakili Boniface Mwabukusi

"Kama mkataba ni sahihi,Waziri Mkuu anatuambiaje tukusanye maoni,nani anakusanya maoni,yaende wapi,ya nini? kama mkataba tayari umeshapita" Wakili Boniface Mwabukusi

"Wakati nchi yetu ina Kiongozi mwenye element za Uzalendo watu fulani hawakuonekana kabisa,sasa hivi wamerudi wanatukana hadi Mahakama, Watanzania angalieni walioko nyuma ya huu mkataba"Wakili Boniface Mwabukusi.

"Kila uovu juu ya Tanganyika tutaukabili kwa jina lake na kila muovu tutamkabili kwa jinsi anavyokuja,hii ni nchi yetu hatutamuchia mtu mwingine aitetee" Wakili Boniface Mwabukusi

"Mabadiliko ya sheria yanayokwenda kufanyika ni matusi kwa Tanganyika,narudia tena Tanganyika ni nchi kama ilivyo Zanzibar" Wakili Boniface Mwabukusi.

"Tunatoa onyo kwa Kiongozi mwingine kudhani anaweza kuingia mikataba ya kuuza nchi akabaki salama,wasituchezee" Wakili Boniface Mwabukusi

"Tunawaomba Watanzania wa dini zote,Waislamu, Wakristo,Wachungaji na Mashehe na WA jadi,tufunge tarehe 14,15,16 kuomba mapenzi ya Mungu yakafanyike kwa Tanganyika na Tanzania,ahsanteni sana"Wakili Boniface Mwabukusi
KAULI YAKE NI JINAI TOSHA KABISA,HIZI NI KAULI ZA KUWAGAWA WATANZANIA NA KUHATARISHA MUUNGANO WETU NI ZA KUKEMEWA NA KULAANIWA IKIBIDI NA ADHABU YA KIFUNGO JUU,INFLICT,UCHOCHEZI,.
 
Umeamua kutoona mema ya CCM na ni mengi hivyo sina uwezo wa kubadilisha maoni yako mkuu cassavaleaves
Steven,

Kila ni kikaa na kutafakari mema ya CCM nashindwa kuyaona! CCM imetengeneza jamii ya Watanzania kuwa ya Kinafiki, uoga, kujipendekeza kwa wakubwa! Kuabudu viongozi, na kila mtu kujali tumbo lake!

Hali ya unafiki ni kubwa mno kwa Watanzania! Angalia maofisini, mnafanya kikao cha kawaida cha wafanyakazi, unauliza nani ana swali au nyongeza yoyote ile, unaona watu wako kimya! Ngoja watoke mlangoni! Manung'uniko, malalamishi chini chini, unabakia kujiuliza mbona hamkutoa madukuduki yenu kikaoni! Watanzania ni waoga mno kutoa mawazo yao! Tuliofanya kazi na Wakenya, Wanageria au watu wa West Africa na South Africa wako huru kutoa mawazo yao! Sio Mtanzania! Culture hiyo imejengwa na CCM! Kumuogopa Mkuu!

CCM imetengeneza Culture ya ulaji wa mali ya umma na ufujaji! Ni kama jadi kwa Watanzania! Mtu akipata kazi kubwa unasikia, kapata ulaji, na waharibifu wakubwa wa mali ya umma Tanzania, ukiondoa CCM yenyewe ni serikali ya CCM, tuliofanya na watendaji wa serikali , wakubwa kwa wadogo ni walafi wakubwa! Posho! Posho! (Per Diem) Mkutano mdogo wa kiofisi lazima kuwe na posho! Kitu hakiendi bila bahasha! Hili ni janga kubwa mno ambalo CCM imetujengea!

Janga jingine kubwa ni rushwa! .......Steven nisaidie kuyaoona hayo mema ya CCM unayoyazungumza!
 
Ndio imeshakuwa hivyo mkuu cassava, mengi unayoandika ni malalamiko ni kilio chako binafsi ukiwa sehemu umekaa na simu yako ya mkononi, na hayupo wa kukusaidia.

Punguza malalamiko binafsi yakabili maisha kama yanavyotakiwa kukabiliwa. Unakuwa ni wale wale walalamikaji na waliaji wa mitandaoni.

Wakati wewe unaongelea benevolent dictactor wapo wanaoziona fursa nyingi za kibiashara na wanazitumia kikamilifu.

Wewe piga siasa wenzako wanapiga kazi ili wajiingizie kipato.

Steven!

"Wakati wewe unaongelea benevolent dictactor wapo wanaoziona fursa nyingi za kibiashara na wanazitumia kikamilifu."

Ukijikomba kwa "Benevolent dictator" na mfumo wake utakosa fursa kweli! Umepofua macho yako! Kila kukicha Rostam Aziz na watu kama hao wanaingia Ikulu, unadhani wanakwenda kunywa kahawa? Ni kweli kina Rostam Aziz na kundi lao wanazitumia kikamilifu!
 
Wakili Mwabukusi hapo amezidisha ukali wa maneno na matamshi yake, tena sana. Mpaka roho imenistuka dah!!!

Hata viongozi wa vyama vya upinzani kina Tundu Lissu, Freeman Mbowe, Zitto Zuberi Kabwe, Yuda Iskarioti (Prof Lipumba) hawajawahi kutoa matamshi makali kiasi hicho!

Sisi wengine kila kukicha tunaitoa kasoro Serikali, Mawaziri na CCM kwa maamuzi wanayofanya, tokea enzi za mwendazake. Kila siku tunavurugana nao mitandaoni... Ila hatujawahi kuthubutu kufikia kutoa maneno makali na yenye ukakasi kiasi hicho!

Mungu iongoze Tanzania, Mungu Ilinde Tanzania. #TanzaGiza!
Wewe ni msaliti wa Tanganyika. Upi ukakasi wa maneno ya Mwabukusi?
 
"ashukuliwe" ndiyo nini kwenye heading hapo? Au mnaandika kwa lafdhi ya Kiarabu?
 
Hatari sana…….Wazanzibari wamelikoroga lazima walinywe
Hivi kama uwekezaji wa Bandari una faida kwa mkataba huu kwnn wasiwape DP WORLD bandari za Zanzibar?
 
Duuh....
Safi kwa kuanza kuelewa kinachopigiwa kelele.
Serikali imeshindwa vipi kuajiri hao wataalamu wa mataifa mengine yenyewe?
Huoni kuwa serikali imeshindwa kutuongoza nayo pia inapaswa ibinafishwe?
Serikali legelege ,haina uhalali wa kuwepo kuwepo kama inashindwa kusimamia kikamilifu eneo dogo tu la bandari , hiyo kampuni yenye watu wa kimafia wataiweza wapi .au ni yale mambo kila kitu SAA100 atakiona ikulu kama alivyosema
 
Hii article imejisimamia!
Inasomeka na inaeleweka kuanzia makao makuu ya akili na Uzalendo.

Kwamba kila nchi ijisimamie.

Hii ina Maanisha Zanzibar inaye Rais, Tanganyika haijafanya Uchaguzi.

Kipindi kigumu sana hiki.

Katiba Mbovu.

Rais akifia Madarakani yapaswa baada ya kipindi kifupi kama 90 days ufanyike uchaguzi, Makamu wa Rais anayekaimu ndani ya hizi siku 90 asiruhusiwe kugombea ndani ya awamu hiyo ya aliyefia madarakani, aruhusiwe kugombea awamu inayofuata baada ya ile ya kufiwa kwa democracy kama kawaida ya ndani ya vyama vyao vya siasa, na anayekaimu nafasi ya rais aliyeaga dunia ndani ya hizo siku 90 asiruhusiwe kufanya mabadiliko ya nyadhifa zozote ndani ya utawala uliokuwepo.
Na asiwe na ruhusa ya kusaini mikataba ya uwekezaji au ya aina yoyote mpaka uchaguzi.
Atumike kutuvusha tu.

Tusiwe taifa lenye maono hopeless kabisa kiasi hiki.
Or
Otherwise nafasi ya Makamu wa Rais wa nchi yetu kwa fursa yake ilivyo inaendelea kuwa ni hatari ya wazi kabisa kwa Rais mchaguliwa.
Naunga mkono hoja..
Inaboa sana kuongozwa na mtu ambaye hamkumchagua.
Kingine haya uliyopendekeza itakuwa ni njia nzuri sana ya kumlinda Rais aliyechaguliwa na watu ili hata makamu wake akiingiwa na tamaa ya madaraka, akate tamaa ya kufanya chochote kumdhuru kwa sababu kwa kufanya hivyo, hataweza kuchukua nafasi ya Rais, isipokuwa kwa ajili ya kulivusha tu Taifa kwa kipindi hicho cha mpito.
Ahsante sana kwa maoni mazuri Mkuu.
 
"Maliasili zetu Watanzania zinachukuliwa bure haya ni maajabu,sitaruhusu hilo" Hayati Rais John Pombe Magufuli.
 

Attachments

  • VID-20230715-WA0734.mp4
    9.5 MB
Kwa hiyo taratibu zinafanya adanganye hata kwenye nyumba ya Ibada! Nimekwambia CCM inaondoa hata hofu ya Mungu! Huyu mwingine anadangamya kuhusu Tenda ambayo ambayo wanaijua wao tu!

Steven, huwa siamini mambo ya ushirikina! Lakini ukiiangalia CCM KWA KINA unaweza kuamini kuna ushirikina unaopumbaza akili za watu!

Huwa nashangaa walioko kwenye fani ya ualimu Tanzania, hivi huwa wanawezeje kufundisha Muundo wa Muungano ambao haungii hata kichwani! Maana Muungano wetu ni kama fumbo la Imani! Haulezeki! Na huwa najiuliza watoto wa Kitanzania wanajua mfumo wetu wa Siasa kweli? Maana hujui tunafuata mfumo wa Kibepari/Ujamaa/Social Democratic......Maana Nyerere alianza na Siasa ya Ujamaa.....na Magufuli akaondoka Fascism!Mungu asingelihurumia taifa hili tulikuwa tumezaa Fashisti mwingine Africa. Mfumo wa siasa ndani ya CCM unamtegemea Raisi! Sasa hivi Samia haijulikani anafanya nini! Hiyo ndio CCM! Lazima ujiondoe akili!
Unayo haki ya mawazo huru mkuu cassava. JPM hakuwa fascist. Alikuta taifa la wapigaji na akaamua alichangamshe.

Hakuna fascist anayeweza kujenga SGR kama ilivyojengwa na kuelekea kumalizika.

Hakuna dikteta anayeweza kupambana mpaka bwawa la Mwalimu Nyerere limekamilika na kwenda kuongeza umeme kwenye gridi ya taifa.

Hakuna dikteta mwenye uwezo wa kufufua shirika la ndege na linapaa katika ushindani wa kidunia kwa kasi, hayupo mbabe wa aina hiyo.

Tunadhani ni dikteta kwa sababu wengi wetu tulizoea kubembelezana katika kila hatua ya uongozi wa nchi, tumezoea mno kupiga domo na kudhani wenzetu na wao wanaendekeza ujinga huu wa demokrasia zinazopitiliza kama sisi.

Muungano wetu sio fumbo la imani, mkuu usiikejeli imani katoliki hata kama wewe sio mkatoliki.

Muungono wetu umejikita kwenye utu wa mtu na hauwezi kukwepa mantiki ya muungano wakati wowote ule wa maisha yako. Usiwasikilize hawa wapumbavu wanaozungumzia Utanganyika katika afrika mashariki ambayo Sudan ya kusini inataka kuwa sehemu yake pia.

Usiwasikilize hawa wapumbavu wanaojiita watanganyika wakati Congo anaingia kwa kasi kuwa sehemu ya jumuiya ya afrika mashariki na kati.
 
Steven,

Kila ni kikaa na kutafakari mema ya CCM nashindwa kuyaona! CCM imetengeneza jamii ya Watanzania kuwa ya Kinafiki, uoga, kujipendekeza kwa wakubwa! Kuabudu viongozi, na kila mtu kujali tumbo lake!

Hali ya unafiki ni kubwa mno kwa Watanzania! Angalia maofisini, mnafanya kikao cha kawaida cha wafanyakazi, unauliza nani ana swali au nyongeza yoyote ile, unaona watu wako kimya! Ngoja watoke mlangoni! Manung'uniko, malalamishi chini chini, unabakia kujiuliza mbona hamkutoa madukuduki yenu kikaoni! Watanzania ni waoga mno kutoa mawazo yao! Tuliofanya kazi na Wakenya, Wanageria au watu wa West Africa na South Africa wako huru kutoa mawazo yao! Sio Mtanzania! Culture hiyo imejengwa na CCM! Kumuogopa Mkuu!

CCM imetengeneza Culture ya ulaji wa mali ya umma na ufujaji! Ni kama jadi kwa Watanzania! Mtu akipata kazi kubwa unasikia, kapata ulaji, na waharibifu wakubwa wa mali ya umma Tanzania, ukiondoa CCM yenyewe ni serikali ya CCM, tuliofanya na watendaji wa serikali , wakubwa kwa wadogo ni walafi wakubwa! Posho! Posho! (Per Diem) Mkutano mdogo wa kiofisi lazima kuwe na posho! Kitu hakiendi bila bahasha! Hili ni janga kubwa mno ambalo CCM imetujengea!

Janga jingine kubwa ni rushwa! .......Steven nisaidie kuyaoona hayo mema ya CCM unayoyazungumza!
Tatizo letu kubwa ni elimu tu. Mengi yanayoendelea katika mijadala ya mitandaoni ni ushahidi wa upungufu wa elimu tulionao.

Mengi yanayohusu bandari ni ukosefu tu wa elimu ya kisasa. Ushahidi ni namna wanasheria walivyoweza kujibu hoja zote zilizoletwa kuhusu bandari siku walipofanya mkutano na waandishi wa habari.

Tusichezee elimu, kwa kufanya hivyo tunazalisha wajinga wengi sana, wanaoweza kudanganywa kwa hoja nyepesi za mtu mwenye nia mbaya.

Culture ya ulaji hata hao CHADEMA wanayo. Hata huo upinzani kwa ujumla umejaa hiyo culture.

Mengi unayoandika ni malalamiko tu, ni hisia zako japo unaruhusiwa kuwa nazo.
 
Steven!

"Wakati wewe unaongelea benevolent dictactor wapo wanaoziona fursa nyingi za kibiashara na wanazitumia kikamilifu."

Ukijikomba kwa "Benevolent dictator" na mfumo wake utakosa fursa kweli! Umepofua macho yako! Kila kukicha Rostam Aziz na watu kama hao wanaingia Ikulu, unadhani wanakwenda kunywa kahawa? Ni kweli kina Rostam Aziz na kundi lao wanazitumia kikamilifu!
Mkuu unalialia sana. Huyo dikteta ndio kiongozi wako na huna mwingine sasa unafanyaje ili uweze kuishi?.

Nenda kapige kura siku ya uchaguzi uweze kuchagua unayemtaka. Kulalamika hapa JF bila ya kutafuta suluhisho katika sanduku la kura ni kupoteza muda tu.

Unaishia kuwa mwanaharakati fulani mwenye hasira muda wote.
 
Tatizo letu kubwa ni elimu tu. Mengi yanayoendelea katika mijadala ya mitandaoni ni ushahidi wa upungufu wa elimu tulionao.

Mengi yanayohusu bandari ni ukosefu tu wa elimu ya kisasa. Ushahidi ni namna wanasheria walivyoweza kujibu hoja zote zilizoletwa kuhusu bandari siku walipofanya mkutano na waandishi wa habari.

Tusichezee elimu, kwa kufanya hivyo tunazalisha wajinga wengi sana, wanaoweza kudanganywa kwa hoja nyepesi za mtu mwenye nia mbaya.

Culture ya ulaji hata hao CHADEMA wanayo. Hata huo upinzani kwa ujumla umejaa hiyo culture.

Mengi unayoandika ni malalamiko tu, ni hisia zako japo unaruhusiwa kuwa naz

Usiniingize Chadema kwa nguvu!...Sina kadi yoyote ya Chama chochote Tanzania.....Ni Mtanzania naipenda Tanzania.....Hayo mawazo zuzu kila anayetoa hoja dhidi ya CCM ni Chadema ndio ujinga wa wana CCM!
 
Mkuu unalialia sana. Huyo dikteta ndio kiongozi wako na huna mwingine sasa unafanyaje ili uweze kuishi?.

Nenda kapige kura siku ya uchaguzi uweze kuchagua unayemtaka. Kulalamika hapa JF bila ya kutafuta suluhisho katika sanduku la kura ni kupoteza muda tu.

Unaishia kuwa mwanaharakati fulani mwenye hasira muda wote.
Naona unashindwa kunielewa na hutanilewa! Sijahishi Tanzania hata siku moja kwa Hisani ya CCM! Akili za Watanzania wengi CCM ndio Baba, CCM ndio Mama....CCM ndio "mungu"
 
anachokitafta atakipata. soon atajua maana ya amri jeshi mkuu inamaana gani. ngoja aendelee kufurahisha genge. his days are numbered.

Hata wewe hauwezi kuepuka kifo.

Jaribu kuficha upumbavu wako kwenye mambo muhimu ya nchi
 
Back
Top Bottom