Wakili Msomi, Naibu Spika, Mhadhiri Mwandamizi na Daktari wa Falsafa wa Sheria, Tulia Ackson awa tishio kwa Spika Job Ndugai

..Dr.Tulia anajiandaa kugombea Uraisi.

..mashindano ya ngoma, riadha, na misaada inayotolewa na taasisi yake, lengo ni kugombea Uraisi.

..Na Dr.Tulia alikuwa ni chaguo la mwendazake kati ya wanasiasa ambao angependa wamrithi.
Kumbe ndivyo ilikuwa!
 
Watu wajiandae kuchapwa bakora 2025πŸ˜‚
 
Kumbe ndivyo ilikuwa!

..Magufuli alimuamini sana Dr.Tulia.

..alitaka awe Spika mwaka 2015 akitokea ktk nafasi ya Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

..Magufuli hakumtaka Ndugai, alitaka Spika atokane na wabunge aliowateua, na chaguo lilikuwa Dr.Tulia.
 
Pamoja simkubali Ndugai na matamshi yake Ila Tulia nae hakubaliki hata kwa kulumangia.

Tuendelee na mjadala.
 
Achana na mzee wa Galilaya ambaye ameshamuona mkee wa........mubashara.
 
Tukiweka ushabiki pembeni,Mimi Ndugai simpendi kabisa,
Lakini alichoongea kina mantiki,
Swali kwanini mawakili hujitambulisha kama"wakili msomi fulani bin fulan"(learned friend),huu utamaduni ulitokea UK kwa maelezo ya Spika,je una maana yeyote katika kuonyesha weredi wa hao mawakili?
Je mtu asipotambulishwa kwa cheo Cha kielimu alichonacho,Kuna mfanya ujuzi wake upotee?au ni njia ya kuji boost tu,na kujionyesha upo tofauti na wengine?!
Maana hivi vyeo na title,zipo kwenye CV,na Kuna sehemu inabidi uzionyeshe ama kwenye usahili,au kutafuta tender kukuza profile ya kampuni yako,sasa Kuna haja gani ya kutumia hivyo vyeo kwenye public?ukisema mi ni wakili msomi,muhandisi,Dokta,muhasibu kwa watu wengi hawaoni chochote zaidi ya Swaga.
Wacha sifa zikufate,mfano Watu kama Diamond,Kiba,Dangote,Mzee Mengi,Bakheresa,Mo,Shabiby wakijatambulisha tu majina yao,watu wote watajua Hawa ni kina nani na wamefanya na wanafanya nini?
Sasa ukisema Mimi wakili msomi! Then ??!!!so what!!!?
 
Mkuu wewe Achana nae hajui asemalo. Anachanganya mambo. Kuna Spika na Naibu Spika.
Wewe ndio unampotosha mwenzio spika sio lazima awe mbunge bali naibu spika lazima awe mbunge hata Mzee Msekwa mwaka 2000 alistaafu ubunge lakini aligombea uspika na akashinda akawa spika.
 
Kuwa mawakili wa aina mbili
1. Uwakili kwa desturi na utamaduni (customary & cultural legal agent-doesn't hold a practice licence)
2.Uwakili wa kusomea (learned counsel/advocate-holds a practice licence)

Hiyo sifa hawakujipachika wenyewe ila mfumo wa kisheria ndio uliweka tofauti hiyo kwa kuzingatia matokeo ya kazi waifanyayo inahitaji kuongozwa kwa maadili, taratibu, kanuni na sheria. Kusomea sheria pekee hakukufanyi uitwe wakili msomi mpaka upitie shule ya sheria.

Halikadhalika wahandisi, madaktari, wahasibu na wapelelezi wenye taaluma wana leseni ya utendaji kazi hiyo (cerified licence-class A, B &C na inahuishwa kila mwaka kwa kukipia tozo stahiki .

Kwa hiyo kama mtu kweli amesomea hiyo taaluma ya sheria na ana weledi baada ya kuhakikiwa na kupitishwa shule ya sheria basi wako sawa. Acheni wivu. Kama miongoni mwa mawakili hawatekelezi majukumu yao kwa uadilifu basi hao ni mapungufu binafsi sio taaluma husika
 

Hivi wakili Msomi maana yake ni nini? πŸ˜‚ kuwa mawakili ambao sio wasomi?
 

Hakuna uwakili wa desturi mnajaribu kujitengenezea vimajina tu. Hao wa desturi nani kasema wanaitwa mawakili. Kama ni hivyo kila kitu kina destruri πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Hata asipogombea bado anaweza akashinda kiti cha ubunge.
Tulia Ackson aliingia kwa mtindo up huo!
Mw3nda zake alimchomoa toka UDSM kwa kumteua Mbunge na akawa amependekezwa kuwa Naibu wa Spika!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…