Wakili Msomi Pascal Mayalla, umemsikia Prof. Shivji? Bado unatuita watanzania Wajinga?

Pascal hafai kuwa na verified ID maana anabaki kuwa mtu wa kuongea kinafiki ili ajikombekombe huenda akakumbukwa kwenye teuzi, mimi hata kusoma comments zake naona ni kupoteza muda tu.​
 
Paskali mayalla ni takataka kabisa,hata maandiko yake huwa siyasomi kbs.yamejaa unafiki wa hari ya juu.
 
Sasa hao maprof si ndio wametufikisha hapa tulipo nchi masikini wajifunze au wao tunawapima na wale maprof wenzao wa kipindi kama chao waliokuwa nchi za vietnam ,singapore na south korea wa huko ndio kipimo chao,ila wao kwa sasa hawana nafasi ni fikra zilizopitwa kwa kweli zilipendwa tutajifunza nini kwao kwenye dunia ya utengemano wao bado ni conservative wakati tunahitaji modernisation na economic liberalisation tunahitaji mitaji ije ,technology na knowledge za kisasa zije through foreign investment tunataka makampuni makubwa yaifanye Dar es salaam hub ya business operation zao ili pia wananchi na raia na sekta binafsi wawe ndio engine kuu za kuendesha na kuumiliki uchumi na kukuza kipato binafsi na pato la nchi na sio states tena yaani states ikamue kodi,iweke sera, na kuweka uwanja sawia kwa watu kufanya biashara nchi inafunguka.
 
JPM ndio alileta shida hii huku jamii F, baada ya kuwapiga marufuku mitaani wapinzania wakahamia huku japo sio kitu kibaya. Nina shida moja tu hawataki mtu yoyote awe na mawazo tofauti na wao wataanza kushambulia mtu badala ya hoja, sasa Pascal kaingiaje hapa, Prof Issa katoa maoni yake lakini anajibika sana tena sana lakini kwakuwa kaongea wanachopenda kusikia basi anatukuzwa lakini angekuja na hoja ya kuunga mkono tu angetukanwa na sio kama Issa angeitwa ponjoro na uhakika 100%. Ana hoja mbili dhaifu sana eti hatutajuwa nini kinaingia nini kinatoka yaani export and import huyu mzee hajui operating port haina uhusiano na kutoza kodi za kiforodha, TRA wapo na ndio itabaki kazi yao 100%. Pia hakuna usiri katika export na import dunia hii ya sasa ni kama airport wanaoshusha mizigo na kupakia sio serikali private ila TRA wapo wanafanya kazi zao. Hoja yake nyingine oohh nishati na madini sensitivity ningependa kujuwa usensitivity gani anaongea hapa? Madini yanachimbwa na private na Gas soon private mbona haongei huko. Hoja nyingine dhaifu eti kwanini tusiajiri expats management kamili, hivi kasahahu Voda walitaka kuajiri director tu zilipigwa kelele humu kwani hakuna wa Tanzania na vibali wakakataa kutoa na hii ni private company, issue sio management ya nje kampuni inakuwa na uwekezaji wa vifaa na tech hizi kampuni zinanunua programs kwa bei kubwa na zinalipia millions yearly zina set up training centres za kisasa ndio unaona ufanisi. Kumbuka hizi kampuni zinazouza program za kisasa za kuendesha zina charge pesa ndefu na pia baada ya muda unaambiwa ni absolute unahitaji system mpyaa, haya mambo hayaji kwa bahati kuna huge investment nyuma ya pazia. Mimi nataka kujuwa wapingaji, wao wanapinga uwekezaji au wanapinga mkataba haujakaa vizuri. Huyu Prof anapinga uwekezaji, wako wanasema mkataba mbovu na wako hatutaki DP sasa shida ni wapi ni kama hawaeleweki.
 




"Wakili Msomi" nani Huyo? "Paschal"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…