TANZIA Wakili mtetezi wa ICTR Prof. Jwani Mwaikusa auawa Tanzania

??????????
 
Sijasoma posts zote hapa lakini najiuliza swali moja .............oh sorry RIP Professor na wote uliotangulia nao kupitia njia hii ya kikatili..............
Kunasehemu nimesoma maelezo ya mtoto wa kwanza wa marehemu, Baraka Mwaikusa akisema kuwa alipotoka kwenda kumsaidia baba yake katika eneo la tukio aliwakuta hao wauwaji na kuwauliza kwa nini wamemuua baba yake, nao wakamjibu kuwa wamemuua kwa kuwa alikuwa mbishi na wakamwuliza kama naye anataka wamuue na kisha akachapwa vibao na kuamriwa akimbie huku akisindikizwa na mawe!!! Nina maswali mawili tu kama habari hii ni ya kweli
1. Je wauaji hao walikuwa wamefunika nyuso zao? kama hapana Baraka anawezakuwatambua akiwaona? au kulikuwa na giza? (assume nyumba haina taa ya nje sehemu ya kuegeshea magari)
2. Kwa jambazi ambaye tayari ameua wamewezaje kusita kumwuua Baraka ambaye amekuja karibu kabisa na kufanya mahojiano nao ya kwa nini wamemuua baba yake?
3. Reflex action ya Baraka ni ya ajabu kwa kweli (kwangu mimi) maana kwa kawaida katika tukio kama hili nilitegemea Baraka angejificha kabisa uvunguni kwani hakuwa anajua kama wataishia tu kumwuua baba yake au wataingia na ndani kuwaangamiza na wao sembuse kutoka nje na kuwafuata?? Inanikumbusha wale watu 17 waliouwawa Musoma ambapo watoto wadogo tu walikimbilia uvunguni kujificha pamoja na kuwa hawakuwa wakijua madhara ya tukio lililokuwa mbele yao)

Unless mtu anihakikishie kuwa habari hizi hapa Picha na maelezo ya tukio la msiba wa Prof. Mwaikusa - wavuti)
ni za uzushi.
 
Manajamiione,pia nashangazwa kama walimwua huyo mpwa wake na jirani kwa hofu ya kutambuliwa na wakamfukuza tu huyo kijana wake,habari zinachanganya sana,kijana huyo ilishasemwa pia kwamba alidai wauwaji hao hawakuchukua kitu,na sasa kuna taarifa walichukua brief case,pia kulikuwa na taarifa kwamba walimsachi marehemu mifukoni,sasa sijui walioshuhudia tukio ni wangapi?
 
Kagame ana hasira sana. Na nadhani hasira zake hazitaisha habi awarestishe in peace wale wote aliopambana nao kipindi kile cha genocide.
 
hahaha tuko...hiki ni kile kikosi cha kagame cha kuua wapinzani wake nje ya nchi...saivi kakutana na raisi mjeshi!!!JK hahahahaha!!!!!!
 
sura hii mbaya sana kwa serikari yetu na wanywarwanda ndio wamejikita sana; rejea kauli ya mtikila kuhusu kagame
 
Niliwahi kusikia tetesi kuwa Rais Kagame kahusika na mauaji haya.
 
RIP Prof
 
Mmh! Hii inatisha jamani, sasa hao majambazi walifanikiwa kuchukua kitu? au ilikuwa ni chuki tu?
Nina wasiwasi kama kweli ni majambazi, sasa kwanini waue mtoto na jirani pia!!
Mungu tusaidie.
Alikuwa anatetea kesi nyingi za genocide Rwanda!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…