TANZIA Wakili mtetezi wa ICTR Prof. Jwani Mwaikusa auawa Tanzania

TANZIA Wakili mtetezi wa ICTR Prof. Jwani Mwaikusa auawa Tanzania

Mwapachu mourns Mwaikusa

THE East African Community (EAC) Secretary General, Ambassador Juma Mwapachu, has sent condolences...

...said that much as there could be criminal elements in the society, Prof Mwaikusa’s tragic killing may not be a manifestation or reflection of such type of behaviour.

"Evidently, we live in an age and time when we cannot be too rational about these situations. If anything, we are challenged, as individual members of society, as a country and more ardently, as a state, to be more focused about the nature and character of our society; the social stratification that is reinforcing due to the huge gulf between wealth and poverty and the sense of despair that seems to engulf a large section of our society," he said.



By DAILY NEWS Reporter, 18th July 2010 @ 12:03
??????????
 
Sijasoma posts zote hapa lakini najiuliza swali moja .............oh sorry RIP Professor na wote uliotangulia nao kupitia njia hii ya kikatili..............
Kunasehemu nimesoma maelezo ya mtoto wa kwanza wa marehemu, Baraka Mwaikusa akisema kuwa alipotoka kwenda kumsaidia baba yake katika eneo la tukio aliwakuta hao wauwaji na kuwauliza kwa nini wamemuua baba yake, nao wakamjibu kuwa wamemuua kwa kuwa alikuwa mbishi na wakamwuliza kama naye anataka wamuue na kisha akachapwa vibao na kuamriwa akimbie huku akisindikizwa na mawe!!! Nina maswali mawili tu kama habari hii ni ya kweli
1. Je wauaji hao walikuwa wamefunika nyuso zao? kama hapana Baraka anawezakuwatambua akiwaona? au kulikuwa na giza? (assume nyumba haina taa ya nje sehemu ya kuegeshea magari)
2. Kwa jambazi ambaye tayari ameua wamewezaje kusita kumwuua Baraka ambaye amekuja karibu kabisa na kufanya mahojiano nao ya kwa nini wamemuua baba yake?
3. Reflex action ya Baraka ni ya ajabu kwa kweli (kwangu mimi) maana kwa kawaida katika tukio kama hili nilitegemea Baraka angejificha kabisa uvunguni kwani hakuwa anajua kama wataishia tu kumwuua baba yake au wataingia na ndani kuwaangamiza na wao sembuse kutoka nje na kuwafuata?? Inanikumbusha wale watu 17 waliouwawa Musoma ambapo watoto wadogo tu walikimbilia uvunguni kujificha pamoja na kuwa hawakuwa wakijua madhara ya tukio lililokuwa mbele yao)

Unless mtu anihakikishie kuwa habari hizi hapa Picha na maelezo ya tukio la msiba wa Prof. Mwaikusa - wavuti)
ni za uzushi.
 
Manajamiione,pia nashangazwa kama walimwua huyo mpwa wake na jirani kwa hofu ya kutambuliwa na wakamfukuza tu huyo kijana wake,habari zinachanganya sana,kijana huyo ilishasemwa pia kwamba alidai wauwaji hao hawakuchukua kitu,na sasa kuna taarifa walichukua brief case,pia kulikuwa na taarifa kwamba walimsachi marehemu mifukoni,sasa sijui walioshuhudia tukio ni wangapi?
 
Kagame ana hasira sana. Na nadhani hasira zake hazitaisha habi awarestishe in peace wale wote aliopambana nao kipindi kile cha genocide.
 
hahaha tuko...hiki ni kile kikosi cha kagame cha kuua wapinzani wake nje ya nchi...saivi kakutana na raisi mjeshi!!!JK hahahahaha!!!!!!
 
sura hii mbaya sana kwa serikari yetu na wanywarwanda ndio wamejikita sana; rejea kauli ya mtikila kuhusu kagame
 



Habari nilizozipata zinasema Prof. Mwaikusa Mwalimu wa Sheria na Mwanasheria aliyebobea wa Chuo Kikuu cha DSM amefariki dunia baada ya kuvamiwa na watu wanaosemekana kuwa ni majambazi alipokuwa akirejea nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo.

Prof. Mwaikusa pia alikuwa rafiki wa mahakama ambaye alitetea vizuri hoja alizowakilisha kuhusu mgombea binafsi. mwenye data zaidi atujuze. rip prof.mwaikusa.
---


Wakili mwandamizi wa utetezi nchini Tanzania wa mahakama inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa inayoshughulikia kesi za washukiwa wa mauaji ya kimbari ya Rwanda amepigwa risasi na kufa nje ya nyumba yake mjini Dar es Salaam.

Profesa Jwani Mwaikusa, ambaye pia alikuwa mkufunzi katika chuo kikuu cha Dar es Salaam, aliuawa wakati akitaka kuingia nyumbani kwake nje kidogo ya mji huo.

Polisi wanasema mpwa wake pamoja na jirani yake waliuawa pia.

Imearifiwa kuwa wahalifu hao walilipekua gari la marehemu na kuondoka na mkoba wake wa kazi pamoja na hati kadhaa.

Bw Mwaikusa alikuwa wakili mtetezi wa mfanyabiashara wa Rwanda Yussuf Munyakazi anayekabiliwa na tuhuma za kuhusika katika mauaji ya kimbari kwenye mahakama ya kimataifa mjini Arusha.

Wakati akimtetea, alifanikiwa kuzuia Munyakazi asirejeshwe nchini Rwanda, kwa hoja kuwa asingeweza kutendewa haki na mahakama za huko.

Gazeti la Citizen nchini Tanzania limesema kumekuwepo na ongezeko la matukio ya uhalifu mjini Dar es Salaam katika siku za hivi karibuni.

Watu watano wameuawa kwa risasi na wahalifu wenye silaha katika kipindi cha miezi mwili iliyopita.
---

Viongozi na Wanasiasa wengine waliowahi kupigwa riasasi
- Utata kifo cha hayati Abeid Karume

- DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

- Simulizi: Kisa na Mkasa wa Mauaji ya Jenerali Imran Kombe (Mkurugenzi Mstaafu wa Idara ya Usalama wa Taifa-TISS)

- TANZIA - John Mwankenja auawa kwa risasi

- Dr. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

- TANZIA - Waziri Salome Mbatia afariki dunia, maswali yaibuka!

- Iringa: Mwandishi Mwangosi auawa katika vurugu kati ya Polisi na CHADEMA

- Maandamano ya CHADEMA: Aqulina Akwilini Mwanafunzi wa mwaka wa kwanza NIT apigwa risasi na kufariki; Polisi wakiri kuhusika

- Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka ashambuliwa kwa risasi na Watu wasiojulikana

- Askari polisi aliyepigwa risasi na majambazi Tanga afariki

RIP Prof
 
Mmh! Hii inatisha jamani, sasa hao majambazi walifanikiwa kuchukua kitu? au ilikuwa ni chuki tu?
Nina wasiwasi kama kweli ni majambazi, sasa kwanini waue mtoto na jirani pia!!
Mungu tusaidie.
Alikuwa anatetea kesi nyingi za genocide Rwanda!
 
Back
Top Bottom