Wakili Musa Kwikima (1939 – 2020) Katibu Tume ya Waislam ya Mgogoro wa EAMWS, 1968

Mungu amlaze mahala pema peponi hawa wasio amini wakisikia tu majina ya hawa wazee chuki zao hushindwa kuzificha dhahiri

Sent using Jamii Forums mobile app
Madi...
Lakini hii ndiyo historia ya Tanganyika hatuwezi kuibadilisha.

Wamejaribu watu kuibadili na natokeo yake ndiyo haya tunayaona leo baada ya kuandikwa historia ya kweli.

Katika kujaribu kutengeneza lili lililoharibika ndiyo wasomi wa nchi hii wakaamua kukaa kitako na kuandika historia ya Mwalimu Nyerere kuanzia kuzaliwa kwake hadi anafika Dar es Salaam katika kitovu cha siasa za ukombozi.

Walipofika hapa Mwalimu kaja Dar es Salaam wakaja kufanya mahojiano nami na niliwapa Nyaraka za Sykes na picha za zamani za Mwalimu za wakati ule vilevile baadhi ya picha hizo kutoka katika kumbukumbu za akina Sykes kama nilivyozitumia katika kuandika kitabu cha Abdu Sykes.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu akujaalie maisha marefu yenye fanaka uzidi kutudadafulia mengi tusiyo yajua juu hawa wazeee wetu japo wasio amin wanachukia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi niliyepata kumsikia jaji Musa kwenye baraza maarufu Kigoma meza ya duara, miaka miwili iliyopita, alieleza mengi zaidi ya haya. Mengine yanatisha. Nae alipata kusema angeendelea kuhudumu angekuwa jaji mkuu. Umeeleza sahihi japo hujamaliza yote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngali...
Ungeeleza ulichosikia kutoka kwake sote tungenufaika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi alijuaje kama angekuwa jaji mkuu wote tunajua jaji mkuu huteuliwa na rais ni vigezo gani alifikiri yeye anavyo na wengine hawakuwa navyo
 
Mashaaah Mzee katika vitu ambavyo tunapindishwa nchini humu ni historia ya Tanganyika imefinywa sana Jazakhallah Ntakitafuta kitabu chako sheikh
 
Nafikiri utakubaliana na mimi linapokuja swala la uteuzi inategemeana na mapenzi ya anayeteua ndio maana wakati mwingine tunaona wako waliostahili kuteuliwa lakini hawateuliwi
Rod. ..
Umesema kweli lakini hiki ni kisa kingine kabisa kinaanza na mgogoro ukiokuwapo ndani ya TANU kati ya Nyerere na baadhi ya waliokuwa washirika wake wakati wa kupigania uhuru ukaishia kwa serikali kuivunja EAMWS na taasisi zingine kama Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Ukiujua undani wa mgogoro huu na nafasi ya Mussa Kwikima utaelewa kwa nini alikosa nafasi ile.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi siko kwenye mgogoro nishawahi kukutana na marehemu akidai alipaswa kuteuliwa kuwa jaji mkuu nisichokubaliana naye yeye sio anayefanya teuzi Haruni Mahundi aliteuliwa kuwa mkui wa polisi wakati kulikuwa na mapolisi wengi wamemzidi vyeo sifa ya elimu lakini yeye akawapiku kwenye teuzi kuna vitu vingi wanaangalia sio usomi peke yake
 
Rod. ..
Siwezi kukulazimisha.

Mimi nimeandika historia yote kwa utafiti na iko paper, "Islam and Politics in Tanzania," (1989).

Paper hii inakamilisha sehemu ya mwisho ya kitabu changu, "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968)The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," London 1998.

Kuamini au kutoamini kitu ni khiyari ya mtu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi sijapinga historia wala utafiti kwa sababu mpaka umeileta hapa ni wazi umetumia muda mrefu na kuongea na watu mbalimbali na hata swali nalohoji sio maneno yako bali yametoka kwa mhusika nisichokubaliana naye ni hoja ya yeye kuteuliwa kuwa jaji mkuu labda kama teuzi angekuwa anafanya yeye binafsi
 
Rod...
Nami ninachueleza ni kuwa kama si mgogoro ule Mussa Kwikima angepata ile kazi na Sheikh Hassan bin Ameir asingekamatwa na kufukuzwa Tanganyika na BAKWATA isingekuwapo na mambo chungu nzima yangekuwa tofauti.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi alijuaje kama angekuwa jaji mkuu wote tunajua jaji mkuu huteuliwa na rais ni vigezo gani alifikiri yeye anavyo na wengine hawakuwa navyo
Suala la alijuaje au alifikiri ni masuala ya dhana, kiukweli watu kama kina barnabas sammata, Joseph warioba au butiku wengeweza kukusaidia gonjwa lako la chuki lakini zaidi ni kuwa huyu bwana (Mungu Amlaze mahala pema) Aliitumikia nchi kwa uzalendo wake wote ndio ukaona hata akateuliwa mara mbili kuwa Jaji, hizi habari maskini angepaswa kuziandika kuondoa mkanganganyiko kwa hawa wajinga
 
Sijui unamjuaje ila mimi navyomjua ni kwa namna nyingine usinilazimishe nikubaliane na mawazo yako mara nyingi mtu akifariki ni hekima ukanyamaza ukamwache apambane na mola kwani kwa imani zetu yeye ndiye anaona zaidi ya kile tunachokiona sisi
 
Kwikima ndie alikuwa hakimu mkazi wa kwanza muafrika, kwikima ndie alikuwa kabidhi wasii wa kwanza muafrika lakini kama haitoshi ndie mtanganyika wa kwanza kupendekezwa na
Sijui unamjuaje ila mimi navyomjua ni kwa namna nyingine usinilazimishe nikubaliane na mawazo yako mara nyingi mtu akifariki ni hekima ukanyamaza ukamwache apambane na mola kwani kwa imani zetu yeye ndiye anaona zaidi ya kile tunachokiona sisi
Mimi kaka yangu mihayo (judge) alimlea kwenye taaluma ya sheria, lakini kwa ufupi kwikima alikuwa ni mtu wa carible yake ilikuwa ukimshuhudia mahakamani akiunguruma utafurahi, usichoke kujifunza lakini ukitaka kuujua unguli wa yule mnyamwezi funua judgements zake au kutana na mzee mihayo atakusimulia
 
Kwikima amefanya mengi huenda wewe ulikuwa mtoto au hujazaliwa, hao ndio ma pioneer wa sheria ya Tanganyika, unaweza usimpite hata mtu mzima mmoja wa umri wa kuanzia miaka 60 katika fani ya sheria ashindwe kukueleza umaridadi wa kwikima, bwana mkapa alikuwa akimuita mnyamwezi mbishi.

Kwikima ndio hakimu mkazi wa kwanza mtanganyika, kwikima ndio kabidhi wasii wa kwanza mtanganyika, kwikima ndio pendekezo la kwanza la Philip Telford Georges (aliyekuwa Jaji mkuu baada ya uhuru akitokea visiwa vya Trinidad and Tobago) kwenda kwa mwl julius ili awe Jaji mkuu, itoshe tu kukwambia wapo wazee wengi walioifanyia hii nchi makubwa hutokuja kuwasikia, Mola Ampumzishe kwa Amani Advocate kwikima
 
Bwana Mohamed Said Waambie hawa mabwana wakafunue EAST AFRICA LAW REPORTS wazisome judgment za yule nguli wa sheria, inaonyesha ni watoto wa juzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…