Wakili Mwabukusi: IGP hatukuogopi, upo hapo kikatiba na kisheria, ukitaka siasa vua magwanda njoo jukwaani

Hakuna mahali kaacha kutumia neno Tanganyika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa atakuwa mgonjwa huyu so tuliambiwa aliishiwa nguvu akawa mnyonge mpaka wenzake wakatoa maombi ili atolewe kumnusuru na kifo...
Mliambiwa na nani kaishiwa nguvu?au na wewe ni polisi uchwara?kawaambie wamkamate tena sasa,mbona wamemwamchia kwa dhamana kwa kosa ambalo halina dhamana,ni sheria ya wapi hio? Na bado Mdude kasema maandamano yataanzia nyumbani kwa IGP,kajipangeni upya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna mahali kaacha kutumia neno Tanganyika

Sent using Jamii Forums mobile app
na leo pia nmeona anazungumza na Wana kijiji kule kwny kimondo anawashauri polisi wakiwafuata wasipigane wala kugombana nao, na wakitaka kuwavalisha pingu wasibishe waende ndani nae atakuja kuwatoa …huu ndio uzalendo
kaitazame kwa Malisa hiyo clip

kaacha zile za kuhamasisha watu kuvamia vitu vya Polisi na kufanya fujo
 
Sijui huwa hawasomi au kufanya kazi kwa maelekezo kutoka juu ndio sababu?maana sheria ziko wazi kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi inahitaji watu kama Wakili Mwabukusi kwa kila Mkoa, mbona serikali ingenyooka sana. It's a time yatupasa tuamke Watanzania.
 
Kuna wakati anaongea kama wakili na kuna wakati anaongea kama mwanasiaisa kwahio angalia anazungumza kama nani muda huo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wakati anaongea kama wakili na kuna wakati anaongea kama mwanasiaisa kwahio angalia anazungumza kama nani muda huo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mahabusu kusikie hivyo hivyo

Ukiongea kama Mwanasiasa ndio uchochee ghasia?
Wewe pia kelele utakavyo sema Ccm wezi, sijui Rais hafai utaachwa , ila ukihamasisha fujo watu wanaruka na Wewe

Mdude mara ngapi anamtukana Rais na hakuna anaeshughulika nae, lete fujo ufanyiwe fujo
 
Mwaarabu anasubir muda tu aanze kazi
 
Kama amechochea ghasia mbona yupo nje?kwanini asihukumiwe na sheria zipo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ccm hawataki katiba mpya ili waendelee kuwa na nguvu ya kuendesha majeshi kwa maslahi binafsi ya kichama,
Mkuu wa wilaya kapewa mamlaka ya kuamuru kamati ya ulinzi ya wilaya na ikatii bila kuuliza chochote

Sasa kwa namna hiyo mambo kama haya hayawezi kuisha ni lazima tuambiane ukweli, vyama viondolewe nguvu ya kutoa maelekezo kwa jeshi la polisi, na jesh lijisimamie kwa mujibu wa sheria na awajibishwe mmoja mmoja pindi anaposhindwa kutekeleza sheria.

Hizi kauli za maelekezo kutoka juu zitaisha, bila hivyo miaka million hakuna kitakacho badilika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…