Wakili Mwabukusi: IGP hatukuogopi, upo hapo kikatiba na kisheria, ukitaka siasa vua magwanda njoo jukwaani

Wakili Mwabukusi: IGP hatukuogopi, upo hapo kikatiba na kisheria, ukitaka siasa vua magwanda njoo jukwaani

Duuh! Huyu Mwamba Huyu. Apewe Maua Yake Ayanuse Mapema.

Maana Naona Si Muda Mrefu Wanaweza Wakamzima. Na Kama akishinda Battle Ya Chama Na Serikali Kwa Kweli Atastahili Kupewa Position Kubwa Hapa Tz Miaka Ijayo Kama Reward Ya Uzalendo Wake.
hawawez mzima kuna macho ya raia kwny hili , mpk ss nchi inampasuko na waliobakia kuiunga mkono serikali , wataanza iunga waunga mkono wakosoaji kama wakimuua huyo mwamba
 
hawawez mzima kuna macho ya raia kwny hili , mpk ss nchi inampasuko na waliobakia kuiunga mkono serikali , wataanza iunga waunga mkono wakosoaji kama wakimuua huyo mwamba
Katika issue ya bandari, tusipochagua kuwa kama Mwabukusi na wenzie, tujiandae kuwa watumwa kwenye Nchi yetu!!

Mimi sitokubali asilani, wewe je?
 
Kabisa,anaongea kimamlaka sana

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii ni kawaida ukanda ule,akiongea ukimsikiliza utasema Ghost anaongea.
Sio yeye tu.
Wengi ni koo za Machifu waliwafurumusha hata Wajerumani miaka ya Ukoloni.
Hata kuongea tu kawaida akianza utatamani ukimbie.
Ni sauti zina mamlaka ndani yake.
Iwe kwa mke,mzazi au nani ni hayo hayo.
Mwabukusi ni watu wa kaliba hiyo.
We sikiliza point zake zaidi.
Kufoka ni kawaida kabisa kwa Wanyaki.
Na ukileta ubishi vichwa,makofi,ngumi vitakuhusu.
Fikiria hapo angekua na mtu anayemlalamikia jirani.
 
Hii ni kawaida ukanda ule,akiongea ukimsikiliza utasema Ghost anaongea.
Sio yeye tu.
Wengi ni koo za Machifu waliwafurumusha hata Wajerumani miaka ya Ukoloni.
Hata kuongea tu kawaida akianza utatamani ukimbie.
Ni sauti zina mamlaka ndani yake.
Iwe kwa mke,mzazi au nani ni hayo hayo.
Mwabukusi ni watu wa kaliba hiyo.
We sikiliza point zake zaidi.
Kufoka ni kawaida kabisa kwa Wanyaki.
Na ukileta ubishi vichwa,makofi,ngumi vitakuhusu.
Fikiria hapo angekua na mtu anayemlalamikia jirani.
[emoji3]Aisee kweli,ukiangalia hio video unaona hata Mbatia kuna muda kama anamshangaa hivi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanachokifanya sasa wanapanda mbegu ya ujasiri hata wakifa wataibuka wengi zaidi,nani alijua angeibuka Mwabukusi?wengi hatukuwahi kumsikia,Kina Lissu tayari walishapanda mbegu haifi, ndio hizi zinaibuka leo
Umeongea point saaana, cheki Lissu mwenyewe imebidi apoe kwanza maana moto wa jamaa ni mkali mnoo
 
Baada ya kutoka Mahabusu kaacha kutumia neno Tanganyika …karudi kutumia neno Tanzania na sasa Dr Samia Suluhu Hassan anamtambua kama Rais sio Mwanamke kutoka Zanzibar

Wakufunzi wa Jela za Tanzania ni mahiri sana kuelimisha watu ndani ya muda mfupi
 
Jamaa atakuwa mgonjwa huyu so tuliambiwa aliishiwa nguvu akawa mnyonge mpaka wenzake wakatoa maombi ili atolewe kumnusuru na kifo?
Sasa ametoka ameanza mbwembwe!! Mngeniachia nchi hii niongoze hata wiki mbili tu niwaweke kwenye mstari hawa wakina kajhujhumele.

Eti wamenipa dhamana nimekataa Mara hooo! nimeshtakiwa kosa la uhaini Mara sijui kosa langu!
Hivi kweli hawa hawaelewi wajibu wa Polisi ni kukamata SUSPECTS mwenye kutamka kwamba ingredient zimetimia ni Mahakama ambayo amekuwa akikataa maamuzi yake.
Nchi hii bado sheria zinaruhusu kumzuia suspect na anaweza kupewa dhamana sasa Polisi wamekosea nini?
 
Wakuu,

Akihojiwa na waandishi wa habari siku chache baada ya kuachiliwa na polisi kwa dhamana, wakili Mwabukusi amenukuliwa akisema."

Nataka nimwambie wazi IGP hatukuogopi, upo hapo kikatiba na kisheria, ukitaka siasa vua magwanda,toka kwenye bunduki njoo jukwaani." Hoja zetu za kisiasa anajibu kwa bunduki akiwa nyuma ya ofisi za umma, amevaa magwanda ya kiaskari? Alisema.

Aache watujibu, tunauliza maswali ya kitaaluma.

Pia amekemea Viongozi waliojigeuza miungu watu, nanukuu;

"Nchi hii kuna watu wamejigeuza miungu watu, wao na familia zao wanataka kugeuza watanganyika kama ngo'mbe wao zizini, watuswage kwenda machungani na kuturudisha muda wanaotaka. Nataka kuwaambia kama walifikiri sisi ni makondoo tumeshageuka kuwa wanambuzi wakorofi na tumeshanyanyua mkia kama ngiri na hawatatufuga tena.

Wanajificha kwenye kichaka mara waseme mapinduzi,sijui uhaini,mara waseme udini, kote huko ni kukwepa kuwajibika, sasa wanataka kupeleka sheria ya hovyo bungeni ili kujusfy IGA, na hii tunawaambia wabunge that luxury is long gone, na kwa sababu tulishaenda Mahakamani na mahakama ikasema haina uwezo wa kuingilia mambo ya bunge, hatutaenda mahakamani tena, tutatumia nguvu ya umma kuleta uwajibikaji, we will not go to court again, we do not have that time.

Ajabu,wanang'ang'ana na sisi tunaodiclose ubovu wa mkataba wanayaacha majizi na majitu yaliyolileta hapa taifa, yanakula na kutafuta vitumbua kwenye ofisi za umma, halafu unakimbizana na bonafide person ambaye anakwambia kuna shida mahali?

Kwahio ndugu zangu narudia kusema tena,IGA ni uvamizi wa taifa letu kiuchumi, bandari ni lango kwa taifa letu, bandari ni urithi tuliopewa na Mungu. Hatuwezi kuwa taifa la ubwege kiasi hiki, mbuga za wanyama tumewapa wageni, nenda kule,unaingia unaambiwa 'now you are entering the United Arab Kingdom' ndani ya nchi?

Tizama mahoteli yanayojengwa Ngorongoro pale,huku wamasai wakifurushwa kama wanyama kutoka kwenye ardhi yao,leo unataka kuniambia Mwarabu ndio ana Ikolojia ya Ngorongoro kuliko Mmasai? That is stupid aspect.

Halafu tukisema,watu wanasema wachochezi. Jamani hili taifa ni kwa ajili yetu,sisi hatujawekwa hapa kuwa watumwa na watwana wa wageni, tuna haki ya kufaidi fursa za kijamii, kiuchumi na kimaendeleo pamoja na kuzimiliki.

Kwahio, ndugu zetu mtuelewe, IGA sio nchi kwahio kuupinga haiwezi kuwa uhaini, IGA ni limkataba korokocho lililookotwa huko kizembe, watu wakafanya copy and paste wakifiri sisi ni mazuzu, tumelikataa."

Mwongozo huu ulikiukwa sana na mamlaka husika badala ya kuufuata wakaongozwa na chuki binafsi kuwakamata hao jamaa bila kuwa na ushahidi mkononi hivyo wahusika kwa majina yao wanatakiwa kushitakiwa kwenye vyombo vya shsria, umma na Mwenye Enzi Mungu aliye Hai afanye uamuzi ulio halali na katika uwanja ulio sawa kisheria.
 

Attachments

Back
Top Bottom