Wakili wa Fei Toto asema wamepokea hukumu lakini Fei hana mpango wa kurudi Yanga

Wakili wa Fei Toto asema wamepokea hukumu lakini Fei hana mpango wa kurudi Yanga

Feisal Salumu mpaka sasa hivi hana mpango wa kurudi na kuichezea Yanga na msimamo wake ni uleule kwamba anataka kuendelea kupinga hayo maamuzi kwa sababu anaona hayakumtendea haki…[emoji817][emoji818]
 
Hahaha Fei tushamalizana nae ,TFF washamaliza kazi ,kama anakimbilia CAS ajiandae kulipa 2m kufungua kesi na pili akae benchi muda wote mpaka kesi iishe ,tatu akishindwa aandae 230m kuilipa yanga.

Endeleeni kumdanganya huyo Fei wenu mtampoteza.

Ushahidi wa Azam upo DUBAI ,Boss wa azam aliyemlipia ticket,hotel na trainer.
Kama alilipa milioni 112 unafikiri 2m itamshinda
 
Wakili Salum Nduruma ambaye anamuwakilisha mchezaji Feisal Salum katika mgogoro wake wa kimkataba dhidi ya Yanga amesema wamepokea nakala ya maamuzi ya Kamati na mteja wake hana mpango wa kurejea Yanga kuendelea kuichezea timu hiyo.

“Feisal Salumu mpaka sasa hivi hana mpango wa kurudi na kuichezea Yanga na msimamo wake ni uleule kwamba anataka kuendelea kupinga hayo maamuzi kwa sababu anaona hayakumtendea haki… njia iko nyeupe kwenda CAS,” amesema na kuongeza:

“Hukumu tuliyopewa haina tofauti na kile kilichotolewa wiki iliyopita na Kamati. Tunataka kuwaandikia FIFA kuwaelezea mazingira yote yalivyokuwa ili kama inawezekana wakati Fei anaendelea na rufaa aweze kusajiliwa katika dirisha moja."
Nimeipenda hio kauli ni kauli kisusio kwa wanaojielewa kisheria
 
Back
Top Bottom