Wakina Mdee wajipanga kukata rufaa. Je, Spika Tulia ataendelea kuwatambua kama wabunge?

Wakina Mdee wajipanga kukata rufaa. Je, Spika Tulia ataendelea kuwatambua kama wabunge?

Baada ya wabunge wa viti maalum wa Chadema kuangushwa mahakamani siku ya leo na kujipanga kukata rufaa kupinga hukumu hiyo, je Spika Tulia ataendelea kuwatambua kama wabunge kwa kigezo kuwa mchakato wa kisheria dhidi yao bado haujakamilika kwa kuwa rufaa wanayojipanga kuikata bado haijasikilizwa?

Kuweka kumbukumbu sawa tu hapa JF, ni kuwa Spika Tulia toka awali aliweka msimamo wa kuwatambua kama wabunge halali, Halima Mdee na wenzake kwa kuwa walikata rufaa kwenye baraza kuu la chama chao kupinga uamuzi wa kuvuliwa uanachama wa CHADEMA uliofanywa na kamati kuu.

Hata baada ya baraza kuu la CHADEMA kubariki uamuzi wa kamati kuu wa kuwavua uanachama wa CHADEMA bado spika Tulia alisema kuwa ataendelea kuwatambua wabunge hao kwa kuwa walimweleza kuwa wanajipanga kupinga uamuzi wa CHADEMA mahakamani.

Sababu kuu ya Spika Tulia anayoitumia ni kuwa, mchakato wa kisheria dhidi ya wabunge hao bado haujakamilika.

Sasa watanzania wanasubiria tena kusikia kauli ya Spika Tulia kuendelea kuwakumbatia wakina Mdee, tofauti na hapo Spika Tulia ataoneka ni mnafiki.
Yule njiti hana aibu kabisa
 
Usipotoshe.

Maombi yanapoondolewa kwa kuwa na makosa ya kisheria hukati rufaa bali unayarekebisha na kuyaleta upya.

Watakachofanya kina mdee ni kufanyia marekebisho maombi yao na kuyapeleka Mahakakani.

Kama wana nia ya kufaili upya itabidi wafanye hivyo bila kupoteza muda na kisha waombe stay order nyingine kabla Bunge halijafanya yake!
 
Usipotoshe.

Maombi yanapoondolewa kwa kuwa na makosa ya kisheria hukati rufaa bali unayarekebisha na kuyaleta upya.

Watakachofanya kina mdee ni kufanyia marekebisho maombi yao na kuyapeleka Mahakakani.
Na wakati huo wakisubiri wafanye marekebisho maamuzi ya mahakama yatakuwa yanaheshimiwa hivyo ni rasmi wamevuliwa ubunge.
 
Unaweka rufaa kwenye kitu gani?

Walikosea maombi yao hivyo hakuna cha kukatia rufaa pale, it's over.

Kama Spika akiamua kuwabeba tena basi sharti wapeleke maombi mengine upya, ambayo hata hivyo mwisho wa siku watashindwa tena, Chadema kama taasisi ina taratibu na sheria zake ambazo mahakama lazima iziheshimu.
 
Haya Mambo ya kina Halima Mdee yana turudisha nyuma sana ,Kwanza wanatumia pesa za wananchi kinyume na sheria ,pili tunatumia pesa kuendesha hizi kesi na Mwisho viongozi wa nchi hii pamoja na CHADEMA mnatufanya wananchi wajinga Sana .
Kosa la CHADEMA hapo ni nini?? Wewe hacha kupotosha, kosa hapa ni la tulia, kwan kigezo cha kuwabakisha bungeni tangu hawali hakikuwepo.

Nadhan mimi nauona mwisho wao covid19 hasa nikizingatia mahamuzi ya jana ya mahakama yametoka na matokeo ya maridhiano yanayoendelea kati ya samia/ CCM na CHADEMA
 
M
Ruge na Kiwanga nao vimeo tu. Kwa nini wasiwalete akina Rose Mayemba angalau wana viwango , uelewa na sio wachumba wa viongozi. Ruge ni mali ya mwenyekiti inajulikana wazi.
Mawazo ya kipumbavu.
 
Kwa kikao kile Cha ikulu nadhani Mama Samia aliridhia waangushwe mahakamani Ili mazungumzo ya katiba mpya yaendelee. Hakuna namna Mbowe angerudi mezani huku kina Mdee Bado wanadunda tu bungeni
Hata mm nilijua hilo, ukimya wa mbowe Kuna mkataba mzito wa utekelezaji uliowekwa, mmoja wao akikiuka hapo moto utawaka
 
Back
Top Bottom