Wakinamama wanaolea watoto bila baba (single mothers): Sababu, athari kwa mtoto, changamoto na mitazamo ya jamii

TAHADHARI



Ukitaka Kuoa Single Mother Hakikisha Umeona Kaburi La Baba Mtoto.


I'm Done.
 
We utakuwa umelishwa madawa amekuroga mkuu shtuka inamaana wanawake wameisha au
Kama limbwata limeweza kusurvive Ten yrs nitaenda kurenew mwenyewe kuliongezea mkataba sio kwa raha hizi ninazopata jamani,Sijui mnakwama wapi vijana wenzangu.!
 
Narudia tena kuoa single mother ni sawa na kubeba bomu la nyuklia wana pasha vipolo sana baba watoto zao labda uhakikishe baba mtoto kafa na mwili wake umeuona na umeshiriki kuweka udongo kaburini
Kwa hiyo Mna wawekea password single mother wasi olewe c et eeeh!!!
 
Narudia tena kuoa single mother ni sawa na kubeba bomu la nyuklia wana pasha vipolo sana baba watoto zao labda uhakikishe baba mtoto kafa na mwili wake umeuona na umeshiriki kuweka udongo kaburini
Kama uliemuoa haujaikuta bikra,unajisumbua tu kaka. kiporo kinapashwa tu tena muogope sana aliemtoa bikra.
 
Sasa alipata suprise gani kutoka kwako!
Yani bikra ukose, hata kuwa wa kwanza kumpa mimba nako umekosa!
 
Mwanamume kuzalisha hovyo nje ya ndoa ni jambo baya na la kukemewa. Mwanamke kuzalishwa hovyo nje ya ndoa ni jambo baya na la kukemewa. Mwanamume mwisho wa siku ndiye mwenye maamuzi ya kuoa ama kutokuoa, mwanamke hana maamuzi juu ya ndoa.

Tunaposema tuwalinde mabinti zetu nao wajitunze hatubahatishi. Wanawake ni waathirika wa moja kwa moja wa mahusiano yasiyofuata mpangilio. Uliona kilichotokea pale RC wa Dar alipoomba kukutana na waliozalishwa wakatelekezwa? Kuzalishwa na mwanamume ni kujitakia, kuolewa ni uamuzi wa mwanamume mwenyewe, mwanamke hana uamuzi kwa hilo.

Sasa kama mnadhani tusiwaelimishe wanawake madhara ya mapenzi kabla ya ndoa bali tuwazuie wanaume kutongoza kwa kuwa tu wakiwatongozeni hamuwezi kukataa basi sawa. Endeleeni kuwaasa binti zenu wajiweke target za kiwindwa na wakware kwa kisingizio cha kutafuta ndoa. Binti anapaswa kulindwa, ni kiimani na kibaiolojia kabisa. Mwanamume atawaka tamaa tu, mwanamke ataweka breki kuzuia tamaa ya mwanamume, ni maumbile. Kama hamtaki basi endeleeni kuzisaka mimba kitaa.
 
Nyenyere, Sijui kama tunaelewana,, sijasema tusiwaelimishe kabisa watoto wa kike bali nimesema tunawapoelimisha watoto wa kike tusisahau kuwaelimisha na watoto wa kiume yaani kwa kifupi ni kwamba tuwaelimishe watu wa jinsia zote..

Halafu mbona umeongea kana kwamba mwanaume kuwaka tamaa ni jambo jema au lililoruhusiwa?? Yaani bado tunarudi pale pale kwamba mwanaume kuwaka tamaa na kutongoza hovyo mnaona ni haki yake na siyo kosa lake ila labda nikuulize swali kwani dunia hii hakuna wanaume wanaojitunza??
 
Kuwaka tamaa kwa mwanamume ni sababu za kimaumbile, ukitambua hilo utaelewa ni kwa nini wanawake imewapasa kuacha kuwashawishi wananume kwa faida yao wenyewe. Mwanamke akitengeneza mazingira ya kumshawishi mwanamume ni rahisi kumdhibiti na ndivyo ilivyokuwa tangu kale.

Tatizo wanawake wameacha nafasi yao na kugeuka kuwanyooshea vidole wanaume, mambo ya chumbani wameyaleta mitaani na kuwasha tamaa za wanaume kwa makusudi. Wamewekeza kwenye kuteka hisia za wanaume, wakiwaonyesha maumbike yao, halafu wanawalaumu kwa kuwatongoza. Tafakari
 
Chanzo ni hii hii jamii ambayo inampangia mwanamke umri wa kuolewa na akifika umri huo hajaolewa inaanza kumnyooshea vidole sasa unadhani mwanamke wa aina hiyo atafanyaje??

Siku mkitambua ya kwamba ndoa inapangwa na Mungu na siyo wanadamu basi mtaacha kuwasimanga wanawake waliochelewa kuolewa na kuwaona hawafai kwenye jamii!!
 
Ni lugha za kujitetea. Jamii kumpangia mwanamke kuolewa hakupelekei aamue kuanza vitendo vya kikahaba. Mwanamke anayeanza vitendo hivyo hupunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kupata ndoa, hivyo si kweli kwamba jamii ndio inasababisha hayo.
 
Ni lugha za kujitetea. Jamii kumpangia mwanamke kuolewa hakupelekei aamue kuanza vitendo vya kikahaba. Mwanamke anayeanza vitendo hivyo hupunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kupata ndoa, hivyo si kweli kwamba jamii ndio inasababisha hayo.
Mkuu sijui unaishi kwenye jamii ya aina gani lakini ukijaribu kufuatilia vizuri utagundua kuwa hiki ninachokiandika ndiyo uhalisia uliopo hasa kwenye jamii za kiafrika.

Acheni kuwalazimisha wanawake waolewe mapema kama ambayo mnawaambia waache kuzaa bila ndoa halafu muone matokeo yake tatizo lenu hamtaki kubadili mbinu kila siku mnakazania mbinu moja tu hata kama imefeli kwanini msijaribu mbinu zote halafu muangalie ipi itazaa matunda.
 
Nahisi sijakuelewa, unamaanisha tatizo la single motjers ni ndoa za mapema? Pia mbona jamiii ya kisasa haina hozo mila za kuwaoza mabinti mapema na hicho ndicho mojawapo ya sababu za mabinti kuingia mapema kwenuye vitendo vya ngono!!

Angalia jamii za mijini kwa mfano, nani analazimisha mabinti waolewe mapema? Lakini huko ndiko kumejaa vitendo vya ukahaba na mimba zisizotarajiwa. Unadhani ni kwa nini? Tulitegemea katika jamii ambayo hairuhusu mimba za mapema kutakuwa na mabinti waliostaarabika wenye kujitambua thamani yao na haja ya kusubiri mpaka ndoa, lakini kinyume chake imefungulia milango ya ngono. Unadhani ni kwa nini?

Pia katika hilo jiulize ni kwa nini wazazi wa zamani hawakupenda mabinti wajikiste sana kwenye elimu. Hawakuwa na maana mbaya hata kidogo, kwao mtoto wa kike alikuwa mwenye thamani kubwa. Hivyo uangalizi na mafunzo yake kwa 90% yalitoka nyumbami kwa wazazi, kuliko kumtoa atumia 90% ya muda wake mbali na nyumbani ilipo shule yake halisi. Kijana wa kiume alihitaji kujifunza namna ya kuitunza familia ndio maana alisisitizwa asome, lakini leo mwanamke anafunzwa mbinu za kujitunza mwenyewe bila kumtegemea mume kwa sababu ni unyanyasaji wa kijinsia.

Mwanamke alipokubali kuwekwa daraja sawa na mwanamume katika majukumu ndipo mkanganyiko ulipoanzia, jamii ilivurugwa ikashindwa kumlinda mtoto wa kike. Watoto wa kike wanatumia muda mwingi zaidi mbali na wazazi wao jambo ambalo linawapelekea kujiingiza kwenye ukahaba, wazazi hawana control tena. Kama unabisha angalia vitoto vya primary na sekondari, ama jaribu kufuatilia maisha ya vyuoni uone watu wanavyokulana huko.Tena wengine wanashinda kwenys vilabu vya usiku kusaka mabwana wa kulala nao kwa ujira.

Sikatai kuwa mtoto wa kike asipate elimu, ila huo ni mfumo tofauti kabisa na ule wa awali. Ni ukweli mgumu kuukubali kwamba elimu ya mwanamume inapaswa kuwa tofauti na elimu ya mwanamke kwa sababu ya tofauti ya majukumu. Mmoja ni mtafutaji mwingine ni mlezi. Kuwapa wote elimu aina moja ya utafutaji kumemwondoa mwanamke kwenye majukumu yake na sasa hajitambui badala yake anafukuzia maisha ya kiume. Mkanganyiko huu ndio umemfanya awe victim wa mateso, manyanyaso, kutu,ikishwa kingono, kugeuzwa chombo cha starehe cha mwanamume, kuwa chombo cha kutangaza biashara n.k.
 
Naskiaga single mama wanapenda for real pale ukiwa nae ngoja nikatest nkatongoze mmoja nifanye experiment nije wapa mrejesho nione kama hii research iko sahihi
 
Nyenyere, Oohh sawa sawa kwahiyo wanaume wanaowafanyia wanawake hayo yote wako sahihi si ndiyo??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…