Wakopeshaji umiza kwa watumishi wa umma ni matokeo ya sera za CCM

Wakopeshaji umiza kwa watumishi wa umma ni matokeo ya sera za CCM

Ubarikiwe sana. Umenipa elimu kubwa sana, itanisaidia jamaa yangu alikopa shilingi milioni 4 kila mwezi tiba ni 670,000/= mwisho atapaswa alipe principal ya milioni 4. Kwa vile katikati ya muda wa marejesho, kapagawa kwa vile malipo wanataka alipe milioni 4 jumlisha rejesho miezi 10 ni 6,700,000/= na faini ya kuchelewa kulipa rejesho ni laki 4 kwa mwezi ujumla yake milioni 4. Hivyo jumla kuu hadi Februari 2020 ni shilingi 14,700,000/=; kinachoendelea sasa ni kuzungushana tu, wapo kwenye mgogoro

Pole yake sana huyo ndugu....

Lakini tukumbuke kuwa dawa ya deni ni kulipa. Na kwa kweli kama alichukua pesa, basi sharti ailipe kwa mujibu wa makubaliano yao ya awali.....

Shida inakuja kwa aliyekopesha kutaka kumkomoa mteja wake na kwa kutumia hesabu ambazo hazijulikani ziko ulimwengu gani kulikuza deni kwa zaidi ya 250%.....

Haiwezekani mtu akope milioni 4 alipe milioni 14.7 hata kama deni lina umri Mkubwa kiasi gani....

USHAURI:

å Asimkimbie mkopeshaji wake. Na kamwe asiliogope deni. Vunginevyo litamharibia maisha yake kabisa. Muhimu ni kukubali kuwa alikopa fedha na ikasaidia kutatua shida yake ya kifedha wakati huo....

å Aende na wakae mezani na kujadili kwa pamoja ili aone namna ya kurejesha pesa ya mtu aliyemkopa pamoja na riba kidogo kulingana na muda aliyokaa nayo....

å kama katika milioni 4, si vibaya akarejesha hata milioni 5 kwa maana awape na milioni 1 ya ziada....

å Wasipoelewana, kesi iendelee mahakamani. Muhimu ni yeye kujenga hoja thabiti....

å Sema tu kuwa hawa jamaa huwa wana ujanja fulani ambao huutumia huutumia kumweka mdeni wao mahali wanapotaka awe kisheria ili iwe rahisi kwao kumwibia...

å Watakuita ofisini kwao. Wanakushawishi kuwa ukubali umekopa 14.7M huku ukweli ukiwa kuwa ulikopa ni Milioni 4 tu + accumulated interest ya 40% (mfano) ambapo kwa ujumla deni lote linakuwa 5,600,000...

å Kwa ushawishi wa hali ya juu, utaingia kingi. Hapo jamaa wanakuwa hata tayari kukupa pesa nyingine hata Milioni moja kabisa....!

Kukubali maana yake, utanasaini makaratasi yao.. Hilo linakuwa kosa lako na ndiyo watakapokunyongea hapo mkifika mahakamani....!

Na usipopata mwanasheria mahiri, utashindwa na utazilipa ama kutaifishiwa chochote chenye thamani hiyo iwe nyumba, gari nk....

√• Lakini kama màandishi watakayokwenda nayo mahakamani ni yale ya Sh. Milioni 4 + accumulated interest ya 40% ambayo ni sawa na Tshs. 5,600,000 basi uwezekano wa kushinda kesi ni Mkubwa na mahakama itaamuru ulipe 5.6M hiyo hiyo hata kama amekaa nayo miaka 10...!!
 
Mimi nadhani tatizo hapa siyo MTU KUKOPA ama KUKOPESHA ama KUKOPESHANA watu.....

Tatizo lililopo ni wakopeshaji ambao kwa kweli wengi wao wako kisheria na wamesajiliwa na BoT chini ya sheria ya "Micro finance services " kukiuka masharti yayowaongoza kufanya kazi zao....

Hivi vitaasisi vya fedha vidogo vidogo vya kukopesha vikifuata utaratibu ulioko kisheria, hawataweza kuhimili kuwepo sokoni kwa sbb wateja wengi wako absorbed na mabenki ambazo zinafanya jukumu hili kwa uwazi zaidi na kwa riba ndogo zaidi....

Wanachofanya hawa Mashailoki ni kutumia shida na "ujinga" wa watu wanaowakopesha kuwaibia kwa njia hii....

Wote tunafahamu kuwa shida haina adabu. Mtu ukiwa na shida inayohitaji fedha kutatuliwa, mara chache huwa hatukirii namna bora na salama ya kupata fedha hiyo. Njia yoyote inayokuja mbele yako inaweza kuwa sawa tu kwa wakati huo, madhara baadae...

Na kwa sababu hiyo ndiyo maana watu tunajikuta tumejiingiza kwenye madeni ya hatari kutoka kwa hawa jamaa na namna ya kujichomoa huko inakuwa ngumu kwelikweli....

Na mtu hugundua kuwa nilifanya maamuzi yasiyo sahihi huku akiwa tayari anaogelea kwenye madhara ya maamuzi yake yanayomuathiri yeye binafsi, kazi na familia ya wote wanaomtegemea....

Na hawa jamaa (Shylocks) wamefanya mambo yafuatayo kuvuta ndege wengi wajinase wenyewe.......;

1. Kwanza ukienda, wao wanazo keshi hapo hapo ofisini kwao. Huhitaji mzunguko wala mchakato kama ule wa kibenki amabao huchukua hadi wiki kupata fedha yako...m

2. Hawana mlolongo sijui usainishe fomu kwa mwajiri wako, ama serikali ya mtaa ama mahakamani nk nk

3. Wao fomu zao walishakula "deal" tayari na viongozi hawa na wana wanasheria wao na pengine mahakimu kabisa wa mahakama za chini ambao wote hawa wana fungu lao katika wizi na hujuma hii dhidi ya raia hawa masikiñi wa kipato na akili na upande mwingine Serikali kukosa mapato

4. Kinachotakiwa ni mteja kuwa na vitu viwili ama vitatu tu;
å Valid kadi ya benki unakopitia mshahara wako
å Bank statement ya unakopitia mshahara wako kuithibitisha hiyo akaunti yako

å Copy ya kitambulisho chako cha kazi

Ukiwa na hivi vitu utajaza fomu yao hapo hapo fast fast na kupewa fedha yako CASH hapo hapo. Kama utaenda baa kunywa, unaenda. Kama una akili utazielekeza kwenye kusudi la kukopa....

KWA HIYO;

å Ni kweli kabisa riba (accumulated interest) yao ni kubwa kupita kiasi na ni kati ya 40% na 50%......

√• Mfano, unachukua Tsh. 1,000,000 kwa muda wa miezi 6 na kama interest ni 50% , maana yake utarejesha Tshs. 1,500,000 ÷ 6 = 250,000 kila mwezi...!!

5. Sharti moja ni kuwa WEWE MTEJA HAWAKuRUHUSU UENDE AMA KUKUPA NAKALA YA MKATABA ULIOJAZA...!!

Hivi ndivyo biashara hii nono inavyofanyika...

Hata hivyo wakopeshaji wengi wameshaingia kwenye mgogoro na baadhi ya wateja wao (wajanja na wenye akili) waliowakopesha baada kuigundua janja hii na kugoma kulipa....

Nimeishudia kesi hii mwenyewe ikimhusu mtumishi wa umma (idara kapuni) na mkopeshaji (jina kapuni) ktk wilaya ya Shinyanga...

Kilichofanyika, ndugu huyu alienda akakopa Tshs 1,000,000 kwa riba ya 40% kwa marejesho ya miezi 5 sawa na Tshs 1,400,000 ÷ 5 = 280,000....

Ndugu huyu akafanya rejesho moja tu.....

Miezi iliyofuata na kwa kuwa kadi ya benki aliacha kwa mkopeshaji kama dhamana, alichofanya ni kwenda benki na kui - block kadi hiyo na akapewa kadi mpya.....

Mkopeshaji kila alivyoenda benki kuchukua chake, akawa hana access, kupata fedha, Card blocked....!

Baada ya muda fulani wakamfungulia kesi ya madai huyu ndugu. Kosa moja wakafanya hawa jamaa. Wakatumia kanuni na ujanja janja wao wa kimahesabu na kuliongeza deni hadi ikazidi principal amount aliyokopa huyu ndugu mara mbili....!

Alikuwa anadaiwa 1,120,000, sasa deni ni karibu 3,500,000+....!!

Kesi iliunguruma kwa kama miezi miwili hivi. Amini usiamini, mkopaji alishinda na kuamuliwa na mahakama alipe hela ileile aliyokopa....

Hapa tatizo hili kweli lipo na haliwahusu walimu ama manesi tu bali ni watumishi wote kada ya umma ama binafsi na hata watu wa kawaida tu wenye shughuli/biashara zao binafsi ili mradi wanakopesheka na wana dhamana fulani....

TUKUMBUKE PIA KUWA;

å Kisheria mtu mwingine kukaa na kadi ya benki ya mtu mwingine ni kosa....

å Vivyo hivyo katika Sera ya fedha na mikopo za taasisi za fedha hakuna riba ya kiwango cha 40%+....

å Kwa tafsiri ya haraka na ya wazi ni kuwa, wanachofanya hao Mashailoki ni WIZI kwa wateja wao na ni WIZI wa mapato ya serikali....!!

Narudia tena KUKOPA na KUKOPESHANA wala siyo tatizo na siyo dhambi....

Tatizo linakuja NIA na DHAMIRA za pande zote mbili (mkopaji & mkopeshaji) ni nini....

ALL in ALL, biashara hii ni nzuri sana lakini it's totally illegal....

Maana kama una mtaji wa 10,000,000 tu na ukawa na wateja 100 tu na unawakopesha kwa staili hii na wote wakawa wanakurejeshea bila shida.....

Kwa kweli ndani ya muda mfupi sana wewe unakuwa milionea...!!

Tatizo ni WIZI...
Kwa maelezo uliyoyatoa ni wazi kabisa kuwa wewe ni moja kati ya mashailock wanaotuumiza sisi watumishi.. Ila yote kwa yote Malipo ni hapahapa Duniani.
 
Kwa maelezo uliyoyatoa ni wazi kabisa kuwa wewe ni moja kati ya mashailock wanaotuumiza sisi watumishi.. Ila yote kwa yote Malipo ni hapahapa Duniani.

Hapana mimi siyo "Shylock" na sijawahi kopesha mtu kwa njia hii...

Isipokuwa mimi ni muathirika (victim) pia wa biashara ya watu hawa na kunipa uzoefu wa kutosha na nikajifunza sana juu ya mikopo.....
 
Hapana mimi siyo "Shylock" na sijawahi kopesha mtu kwa njia hii...

Isipokuwa mimi ni muathirika (victim) pia wa biashara ya watu hawa na kunipa uzoefu wa kutosha na nikajifunza sana juu ya mikopo.....
Ulichoandika ndo kinachotokea mtaani Mimi pia ni victim ambaye ninapambana kujitoa japo sijamaliza hata wiki toka nimetoka kukopa kwa hao watu.. Umeandika vitu on point kabisa mpaka nikawa nahisi wewe ndo uliyenikopesha.
 
Ulichoandika ndo kinachotokea mtaani Mimi pia ni victim ambaye ninapambana kujitoa japo sijamaliza hata wiki toka nimetoka kukopa kwa hao watu.. Umeandika vitu on point kabisa mpaka nikawa nahisi wewe ndo uliyenikopesha.
Wewe ni mwalimu? Hii tabia niliikua naiona sana Kasulu, Kigoma
 
Mara kwa Mara ukiiangalia taarifa za habari utakutana na watu wanaoitwa wakopeshaji umiza. Hawa ni shylocks kwa lugha ya Kiingereza au ukipenda waite "mashailoki". Hawa jamaa wanawakopesha watumishi wa uma kwa masharti makali na ya aibu mno.

Kwanza riba ni kubwa sana inaanzia 40%+ lakini pia watumishi wa umma wanatakiwa kuacha kadi kwa Shylock huyo pamoja na namba ya Siri halafu mshahara ukitoka yule Shylock ndio anaenda kumchukulia mtumishi mshahara. Hii ni aibu mno kwenu watumishi wa umma.
aisee . . . naomba nikuambie kitu mzee. Sio watumishi wote wanapenda maisha hayo. Kipato kisipokidhi mahitaji ndio huko wengi wanapoangukia. Ila pia masharti mengine ni uchuro kabisa. Eti nikupe ATM card yangu, hivi unaijua hela wewe ?
 
Kweli hao wakopeahaji nimewaahuhudia sana mkoa wa MARA.
 
Pole yake sana huyo ndugu....

Lakini tukumbuke kuwa dawa ya deni ni kulipa. Na kwa kweli kama alichukua pesa, basi sharti ailipe kwa mujibu wa makubaliano yao ya awali.....

Shida inakuja kwa aliyekopesha kutaka kumkomoa mteja wake na kwa kutumia hesabu ambazo hazijulikani ziko ulimwengu gani kulikuza deni kwa zaidi ya 250%.....

Haiwezekani mtu akope milioni 4 alipe milioni 14.7 hata kama deni lina umri Mkubwa kiasi gani....

USHAURI:

å Asimkimbie mkopeshaji wake. Na kamwe asiliogope deni. Vunginevyo litamharibia maisha yake kabisa. Muhimu ni kukubali kuwa alikopa fedha na ikasaidia kutatua shida yake ya kifedha wakati huo....

å Aende na wakae mezani na kujadili kwa pamoja ili aone namna ya kurejesha pesa ya mtu aliyemkopa pamoja na riba kidogo kulingana na muda aliyokaa nayo....

å kama katika milioni 4, si vibaya akarejesha hata milioni 5 kwa maana awape na milioni 1 ya ziada....

å Wasipoelewana, kesi iendelee mahakamani. Muhimu ni yeye kujenga hoja thabiti....

å Sema tu kuwa hawa jamaa huwa wana ujanja fulani ambao huutumia huutumia kumweka mdeni wao mahali wanapotaka awe kisheria ili iwe rahisi kwao kumwibia...

å Watakuita ofisini kwao. Wanakushawishi kuwa ukubali umekopa 14.7M huku ukweli ukiwa kuwa ulikopa ni Milioni 4 tu + accumulated interest ya 40% (mfano) ambapo kwa ujumla deni lote linakuwa 5,600,000...

å Kwa ushawishi wa hali ya juu, utaingia kingi. Hapo jamaa wanakuwa hata tayari kukupa pesa nyingine hata Milioni moja kabisa....!

Kukubali maana yake, utanasaini makaratasi yao.. Hilo linakuwa kosa lako na ndiyo watakapokunyongea hapo mkifika mahakamani....!

Na usipopata mwanasheria mahiri, utashindwa na utazilipa ama kutaifishiwa chochote chenye thamani hiyo iwe nyumba, gari nk....

√• Lakini kama màandishi watakayokwenda nayo mahakamani ni yale ya Sh. Milioni 4 + accumulated interest ya 40% ambayo ni sawa na Tshs. 5,600,000 basi uwezekano wa kushinda kesi ni Mkubwa na mahakama itaamuru ulipe 5.6M hiyo hiyo hata kama amekaa nayo miaka 10...!!
Mkuu nazidi kuishabikia na kukubali JF ni bahari ya maarifa; nashukuru sana na msaada wa mawazo hivyo nitamshauri ndugu yangu kwa kifua aende kuonana na jamaa wakae mezani kwa majadiliano namna ya kumalizana kwa faida ya pande zote mbili
 
Mkuu umefafanua vizuri sana,Watu wanadhani watumishi wanapenda kujiingiza kwenye hizi shida.Mimi mara kadhaa nimewasikia wakuu wa wilaya wakiwashangaa na kuwalaumu watumishi wanaoacha kadi kwa wakopeshaji wa aina hii, mwenye shibe hamjali mwenye njaa .Mimi nina uhakika kabisa kuna hadi wakuu wa Idara wenye mishahara minono na marupurupu wamewahi kukopa .Shida inapokuja huo muda wa kusubiri mlolongo wa kuchakata namna ya kupata pesa bila kuumia haupo.Ingawa pia kuna watumishi wameingia kwenye shida hizi kwaajili ya starehe tu.Kuna wakuu wa wilaya walio wahi kuwa walimu nao walipita kwenye mfumo wa uachaji kadi kwa wakopeshaji hawa, lakini baada ya kuwa kwenye green pasture sasa wamekuwa wakiwakejeli wanaotatua matatizo yao kwa kuacha kadi ili wapate fedha kwa haraka.
Serikali inapaswa kulitafutia ufumbuzi wa kudumu hili swala.Tatizo no kwamba swala hili linatumika kutafuta sifa za kisiasa.Baadhi ya wakuu was mikoa wanalitumia pia kujipatia sifa binafsi kwa kuanika wahusika kwenye makamera waonekane kweli wanafanya kazi.Luna wafanyakazi ufanisi wao kazini umeshuka kwa. Hofu ya kutafutwa na hawa wakopeshaji, wengine wameugua hadi maradhi ya moyo.Kinachofanyika taasisi za kitapeli zimewashika wakurugenzi na maafisa utumishi yani fomu ya mkopo inapelekwa asubui mchana unaingiziwa hela yako.Upande was pili zile benki kubwa hazitoi rushwa kwa maafisa utumishi wala wakurugenzi yaani mfanyakazi unapeleka fomu yako inakaa kwenye failing hadi wiki nne afisa utumishi hataki kusaini kwa sababu hujampa chochote.Wale matapeli kama Bayport, platnam na faidika hela utaipata Siku hiyohiyo wana mtandao had I hazina kote huko wametoa hela.Sijui kwa nini inawalea hawa watu yani riba zao ni kubwa mno hata ukitaka kuwalipa ujitoe hawakubali au watakubambikia deni kubwa mpaka uchanganyikiwe.Tatizo serikali haijaamua kumaliza huu utapeli
 
Sio makaratasi tu na ATM card Yangu.
Daaah aisee kwaio unaweza kuta baada ya miezi 6 deni linaisha unafika unakuta unadaiwa milioni 9 zingine wameshachakachua form za mikopo etc..
 
Back
Top Bottom