Wakristo Kwanini tunakula viumbe vyote ambavyo Mungu aliruhusu lakini tunachagua na kubagua vilivyokatazwa akiwemo Nguruwe?

Wakristo Kwanini tunakula viumbe vyote ambavyo Mungu aliruhusu lakini tunachagua na kubagua vilivyokatazwa akiwemo Nguruwe?

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
ufugaji-wa-nguruwe-1-1024x1024.jpg


Huwa nashangaa sana ni vipi kila kiumbe ambacho Mungu alituruhusu kula huwa kinalika bila tatizo na ni salama kwetu lakini linapokuja suala la viumbe ambavyo alivikataza huwa kuna ubaguzi, mfano viumbe kama nzi, nyau, punda, mjusi na panya watu wanabagua lakini kwa wakati huo huo wanakula vingine vilivyokatazwa kama nguruwe na nyau, ni kwanini ?

Wanyama safi na halali kuliwa ni wenye sifa hizi zote : kwato katika miguu yake + mwenye miguu ya kupasuka kati + mwenye kucheua,.... wanyama kama sungura, nguruwe na paka hawaruhusiwi

"Sifa za viumbe wengine"

Samaki walio halali kuliwa na watu ni lazima awe na mapezi + magamba

Ndege wote wanafaa kasoro tai, furukombe, kipungu, mwewe, kozi, kunguru, mbuni, kirukanjia, dudumizi, kipanga, bundi, mnandi, bundi, mumbi, mwari, mderi, korongo, koikoi, hudihudi, popo.

Wadudu halali kwetu ni wale wenye miguu mirefu maalum kwajili ya kuruka juu na chini kama panzi, senene na nzige

Reptiles wote hawafai : chura, nyoka, vinyonga, kenge, n.k.
 
Kwahiyo tuseme
WaKristo wanaaminika Kula Nguruwe
Waislamu wanaaminika Kula pweza na kambale
Hii ni mada yetu wakristo dada, hao upande mwengine wameingiaje humu ?

Na pia sio wakristo wote wanakula nguruwe kuna madhehebu wanafata sheria zilizowekwa na Mungu, kwao vyakula vyote vilivyokatazwa kama nzi, nguruwe, punda, mbwa vyote ni najisi.
 
Hii ni mada yetu wakristo dada, hao upande mwengine wameingiaje humu ?
Na pia sio wakristo wote wanakula nguruwe kuna madhehebu wanafata sheria zilizowekwa na Mungu

Viumbe vilivyokatazwa kwenye torati
TORATI ni moja na ni ileile inatumika kwa wanaojiita wakristo na waislamu
 
Viumbe vilivyokatazwa kwenye torati
TORATI ni moja na ni ileile inatumika kwa wanaojiita wakristo na waislamu
Ok hao waislam sijajua hali yao wala sijui mpangilio wa vitabu vyao naomba hili suala tujadiliane sisi wakristo,
 
ufugaji-wa-nguruwe-1-1024x1024.jpg


Huwa nashangaa sana ni vipi kila kiumbe ambacho Mungu alituruhusu kula huwa kinalika bila tatizo na ni salama kwetu lakini linapokuja suala la viumbe ambavyo alivikataza huwa kuna ubaguzi, mfano viumbe kama nzi, nyau, punda, mjusi na panya watu wanabagua lakini kwa wakati huo huo wanakula vingine vilivyokatazwa kama nguruwe na pweza, ni kwanini ?

Byakula vilivyoruhusiwa na kukatazwa hivi hapa

Wanyama safi na halali kuliwa ni wenye sifa hizi zote : kwato katika miguu yake + mwenye miguu ya kupasuka kati + mwenye kucheua,.... wayama kama sungura, nguruwe na paka hawaruhusiwi

Samaki walio halali kuliwa na watu ni lazima awe na mapezi + magamba

Ndege wote wanafaa kasoro - tai, furukombe, kipungu, mwewe, kozi, kunguru, mbuni, kirukanjia, dudumizi, kipanga, bundi, mnandi, bundi, mumbi, mwari, mderi, korongo, koikoi, hudihudi, popo.

Wadudu halali kwetu ni wale wenye miguu mirefu maalum kwajili ya kuruka juu na chini kama panzi, senene na nzige

Reptiles wote hawafai : chura, nyoka, vinyonga, kenge, n.k.
Wasabato mna taabu sana😀😀Soma Matendo Ya Mitume 10:15
 
Wasabato mna taabu sana😀😀Soma Matendo Ya Mitume 10:15
Naomba tujikite na maada

Kwanini viumbe vilivyoruhusiwa na Mungu tunavila bila shida lakini ambavyo havikuruhusiwa vinabaguliwa na kuchaguliwa kile kiliwe hiki hapana ?
 
Kol 2:16-23
Kol 2:16-23
Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo. Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili; wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukiruzukiwa na kuungamanishwa kwa viungo na mishipa, hukua kwa maongeo yatokayo kwa Mungu. Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani, Msishike, msionje, msiguse; (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu? Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
 
Naomba tujikite na maada

Kwanini viumbe vilivyotakaswa na Mungu tunavila bila shida lakini ambavyo havikutakaswa vinabaguliwa na kuchaguliwa kile kiliwe hiki hapana ?
Maada ndio nini😀😀😀
 
Wewe hujui utamu wa kitimoto, tumetoka kula hapa na Ngalikihinja yaani huyu mnyama haishi hamu. Acha na hayo yote, wee kula dunia tunapita hii..
 
Kol 2:16-23
Kol 2:16-23
Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo. Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili; wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukiruzukiwa na kuungamanishwa kwa viungo na mishipa, hukua kwa maongeo yatokayo kwa Mungu. Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani, Msishike, msionje, msiguse; (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu? Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
a,e,i,o,u ..... Utaandika vyote lakini tunarudi kwenye mjadala mkuu

Kwanini viumbe vilivyoruhusiwa na Mungu tunavila bila shida lakini ambavyo havikuruhusiwa vinabaguliwa na kuchaguliwa kile kiliwe hiki hapana ?

Kwanini nzi, chura, kasa, nyoka, nyau, n.k vinabaguliwa lakini nguruwe analiwa ilihali vyote vilikatazwa na Mungu ?
 
Wewe hujui utamu wa kitimoto, tumetoka kula hapa na Ngalikihinja yaani huyu mnyama haishi hamu. Acha na hayo yote, wee kula dunia tunapita hii..
Kama kitimoto kinaliwa kwasababu ya utamu huku ikijulikana ni najisi kuna utofauti gani na kuhalalisha uzinzi kisa kuna utamu ?
 
Utaandika vyote lakini tunarudi kwenye mjadala mkuu

Kwanini viumbe vilivyoruhusiwa na Mungu tunavila bila shida lakini ambavyo havikuruhusiwa vinabaguliwa na kuchaguliwa kile kiliwe hiki hapana ?

Kwanini nzi, chura, kasa, nyoka, nyau, n.k vinabaguliwa lakini nguruwe analiwa ilihali vyote vilikatazwa na Mungu ?
Soma vifungu hivyo vya Biblia kamakweli una nia ya kujifunza la sivyo kabishane huko Facebook ndio level zako.Kwa kifupi Biblia haikatazi kula vyakula aina fulani vyote vinaruhusiwa kwa Mkristo isopokua Biblia imeweka uhuru kulingana na utamaduni wa jamii husika.Kwa mfano wachina wanakula Punda lakini Tanzania inaonekana sio utamaduni wala Mila zetu
 
Kama kitimoto kinaliwa kwasababu ya utamu huku ikijulikana ni najisi kuna utofauti gani na mzinzi anaezini kwasababu anasikia utamu ?
Unachekesha sana wewe msabato ....nani kwakwambia kitimoto ni najisi😀😀

Mathayo 15:11
kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni kile kitokacho kinywani mwake.”
 
Kwani nguruwe kawakosea nin, mim nimeanza kula NGURUWE tangu niote meno adi sasa ivi naitwa baba sijawai kuiona iyo dhambi Physically wala impact yoyote juu ya iyo nyama.

ata ivyo nimetoa oda ya nusu kilo na viazi vya 2000 muda huu nipo nasubiri nishushie na Kvant.

nakeleka sana na izi mada za kumuhusu uyu mpendwa wetu. izo dhambi mbona hatuzioni zinavyotukumba tulapo,
 
Back
Top Bottom