Wakristo mjitafakari kwenye suala la mahari, mnawakosea sana binti zenu. Kilichotokea hivi karibuni kwa jamaa yangu kina funzo

Mwanaume uliyekamilika unaoje mwanamke ambaye tayari kashazalishwa? Hivi kweli na akili yako unaenda kuintroduce single maza kwa mzazi wako. Hapana jamani. Wanaume tuwaonee huruma mama zetu.
Kama huyo muoaji au mzazi wake wanatokana na single mother je ? Usafi na utakatifu upo wapi hapo wa kumnyanyapaa huyo single mother?
 
Mimi ni mkatoliki,mahari si pingamizi kwenye swala la ndoa.Unaweza kufunga ndoa bila mahari.
Hilo jambo lililowakuta ni swala la familia husika na mila/taratibu zao
 
Kuangalia kama ina complication😂😂😂
 
Kama huyo muoaji au mzazi wake wanatokana na single mother je ? Usafi na utakatifu upo wapi hapo wa kumnyanyapaa huyo single mother?
Mbona mnamimbiliaga sana kwenye suala la je kama ni mzazi wako. Sasa kama mzazi nae alikuwa malaya kisa ni mzazi basi jambo haliwi baya tena? Tuache hivyo.
 
Naunga mkono hoja.hata Mimi binamu yangu baada ya KUJIFUNGUA tu,wakwe wakaja kujitambulisha na kumaliza kila kitu.Sasa shangazi akataka mahari 3M.Kilichotokea Ni kwamba walitoa laki 3 tu,na wakasema mabinti wako wengi wazuri kuliko huyo binamu yangu kwa hiyo mama(shangazi)abaki na binti take.wao wanabeba Mtoto wao wanaenda kulea.
Binamu yangu akamwambia mama yake sibaki nyumbani maadamu wamekuja Hadi hapa naenda kwa bwana yangu.Laki 3 zikawekwa mezani,Wakwe hawakula chakula Wala vinywaji wakaondoka.Wakamuacha shangazi analia.Mpaka Sasa wameshafunga ndoa ya kanisani na Wana watoto 3.
Ifike kipindi watoto wa kike tujitambue na tukubaliane na Hali za hao mabwana zetu.ukiendekeza Wazazi Sana utazeekea kwa wazazi wako.
 
Moja ya vitu vinavyosingiziwa ukristo ni swala la mahari.
Ukristo haupo specifically kuhusu insu ya mahari..ukristo ni mtu kumuacha Baba yake na Mama yake, swala mahari kiasi hiki ama kile ni tamaa za wakristo si ukristo.
Hapo nimekuelewa mkuu....unajua nimeshawahi shuhudia wakristo wameoana kanisani Tu na hakukuwa na sherehe wala nini na wanandoa wakaendelea na Maisha Yao....basi kuna haja kubwa ya kuliangalia Hilo swala kwani Lina waangusha Sana!
 
MAELEZO YAKO YANAONYESHA WEWE NA RAFIK YAKO NA MPENZI WAKE MNA MATATIZO...
 
Aisee ni heri mtu akuoneshe uhalisia wake. Akitaka kuondoka aondoke kwa amani. Hayo mambo yanataka hiyari ya moyo na sio minyororo!
 
Samahani umetaja ukristo sawa ila kiasi fulani tusema ni maendeleo na usasa wa kweli ..Kuna mzee mmoja ni mkristo alioa huko lushoto miaka mingi maana now ana miaka kama 55 na kuendelea ..alisema enzi alioa mwanamke yeye mwenyewe hakuwa na kitu kabisa alitoa vitu kadhaa ambavyo sio vya thamani ni sehemu ya mazao yake aliyopandailikuwa ni viazi na makabichi ni huko lushoto...ila kwa sasa ypo mbali ana FUSO kadhaa na mkewe sema kijiji wanatoka ni kimoja..

Waislamu kwa sis wapo ambao ni expensive na tambua wazazi wengi wanaleta Tamaa kweny mahali kitu ambacho ndo kinaathiri sana .Binafsi mzee wangu alioza wanae bila ya kuchukua mahali kwanza walitaka wenyewe dada zangu wote ni watu wazima ...kingine mzee wetu alitusihi sana Yale mambo sijui kukaa mlangoni kutaka pesa akasema atakaye kaa kuleta ujinga atajuta, na hata Yale mambo ya kumuomba pesa shemeji zetu alikataa kabisa sio vizuri
 
Hata kama ni alternative ndo uoe binti aliyemaliza form four??
 
Suala la mahari sio la ukristo ni la kifamilia au kitamaduni, umesema binti alikuwa wa Uganda. Maana yake huo ni utaratibu wao, na Tanzania bado familia au kabila nyingi zinafanana katika suala la mahari.
Kuoa au kuolewa na mtu wa imani tofauti sio suala la kujivunia sana, linaweza kuwaletea shida kiasi kwamba wakachukia ndoa yao.
Vizuri kuwa wazi, ilikuwa haina haja kudanganya, angeweka wazi pale pale kuwa hawezi ili ampe uhuru binti wa kufanya maamuzi.
 
Mi sijaona tatizo la mahari ila nimeona tatizo la Braza miaka 37 ukakavae kabint ka miaka 20 hapa wanaume ndio maana tunakufaga na presha.

Sio dunia ya Leo kuoa kabint ulikokapita miaka mingi.

Lazima katamsumbua tu.
Basi hakuna Jambo zuri kama kumpita mkeo miaka kadhaa....Kwanza heshima inakuwepo kubwa Tu...na mwanaume unatakiwa uwe mkomavu zaidi kuliko mwanamke ili uweze kumhandle vizuri

Pili huenda hujui wanawake wanavyozeeka mapema kutokana uzazi na kulea....tatu kumsumbua ni Tabia ya mtu binafsi.

Think big!
 
Nakubaliana na wewe ktk swala la kuoa Imani tofauti...kutokana na mazingira yafuatayo...kama jamaa ameoa Tu Kwa ndoa ya kiislam kwakuwa haikuwa ghali..hapo kuna kosa kubwa kutoka Kwa wazazi WA binti...kwasababu ili uoe kiislamu lazima uwe muislamu,so kama kabakia na ukristo na kaoa Tu kiislamu hapo kuna tatizo...Ila kama muoaji kabadili Kwa hiari yake na kwakukusudia ni sawa
 
Dini haipangi mahari, imetoa miongozo tu ya mtu na mwenza wanavyopaswa kuandamana pamoja kwenda kuanza maisha. Mahari inapangwa na familia ikishirikiana na wapambe. Mfano, kwa ndugu zangu waruguru ukiwapelekea jogoo aina ya kuchi unaondoka na kitu safi kutoka Mgeta au Mlima Kolelo kwa akina Kunambi kule.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…