Makanisani wakristo wengi wakishatoa sadaka kanisani ndio shughuli imeishia hapo. Ni rahisi sana kuwakuta wachungaji mabilionea wanaotajirika kwa sadaka za waumini lakini kuna waumini wana changamoto zinazoweza kutatulika kwa milioni 10 ila wanaombewa badala ya kusaidiwa
Licha ya kwamba waislamu wengi ni maskini ukilinganisha na wakristo, Nimegundua waislamu hawatoi sana sadaka misikitini lakini huwa wanasaidia sana huku nje.
Nimewahi kupata shida ya maji na niliweza kuchota maji bure kabisa msikitini wiki nzima.
Niliwahi kufikia sehemu sina pa kulala nilienda kanisani nikiwa muumini wa kanisa tangu mtoto lakini nilikataliwa kabisa, sehemu iliyonitunza ni msikiti, kanisa waweza kukuta lina mabomba ya kutosha ila ni kwajili ya matumizi ya kikanisa tu.
Mwezi wa Ramadhani ule mwezi mzima ni kawaida sana kuwakuta waislam wanasaidia vyakula watu wenye shida.
Waumini wana magonjwa ambayo yanatibika kwa milioni 10 lakini wachungaji wenye account zinazosoma Bilioni wapo kujifanya wanawaombea, Kweli? Haya kama sio maombi ya kinafki tuyaitaje?
Pamoja na mazuri haya kilichonitatiza kuhamia uislam ni dini ambayo ina baadhi ya sheria zenye mirengo mikali sana, hakuna free will uhuru wa kiimani kwamba unaweza kuchagua dini nyingine, kukariri koran na kuomba kwa lugha usiyoijua, mistari yenye kuchochoea chuki dhidi ya wasio waislam, n.k.