Wakulima Jiandaeni Kisaikolojia na Kuporomoka Kwa Bei ya Mahindi Mwaka huu 2023, Kenya Gunia la Mahindi Imeshuka hadi Tsh. 80,000

Mkuu hapa nakuelewa na naungana na wewe.
 
Mkuu hapa nakuelewa na naungana na wewe.
Mleta uzi ni mbinafsi anataka bei iendelee kupanda huku wananchi wakitaabika alafu kikundi cha madalali wachache wakiendelea kunufaika

Mfano kwa mwezi huu wa pili hakuna mkulima mwenye mazao ni madalali/mabwanyenye ndo wanamazao na ndo wanufaika wakubwa wa huu mfumuko wa bei
 
Kwani agenda mnayoitaka kwa sasa sio kumtaka Samia azuie export ya mazao au?
 
Mchele kutoka wala automkomoa yeyote sana sana utapunguza gharama za maisha kwa wananchi,anayemudu mchele supa wa mbeya anunue na wale wenzangu na mimi tutakimbilia kwenye huo kitumbo kg buku ili mradi tujaze tumbo
Wananchi wa wapi? Asilimia 65% ya watu ni wakulima Sasa uwaletee mshindani hapo unapunguza umaskini au kuongeza?
 
Anajifanya mjuaji sana na anajua kila kitu.
 
Wabinafsi ni nyie mapoyoyo wa mjini mnaotaka kunufaika Kwa jasho la mkulima.

Yaani watu 30% mnufaike Kwa kuwanyonya 70%,hii chini ya Samia haitokaa itokee..

Kwanza nyie wapuuzi ndio mlikataa kutoa tozo za miamala Ili serikali iboreshe Huduma za Afya Vijijini na Barabara..

Good enough wapiga kura wako Vijijini wanalima nyie wa Mjini endeleeni kurundikana kwenye Mikutano ya Chadema watawapa msosi.
 
Unaielewa vizuri tasnia na haujakurupuka, hongera, ila sababu zako hazitoshi kushawishi. Tujipe muda zaidi
 
bAada ya mwez wa kwanza mahindi kushuka huku kwetu mwanza,mwez huu wa pili yamepanda tena kwa speed ya 5G

Nasema hivi huo ni uongo gharama za chakula zitaendelea kupaa tu
Mbeya kwa sasa debe la viazi mviringo limeshuka kutoka tshs15000/14000 mpaka 10000/9000=
 
Nani anataka azuie exports ya mazao? Nyie ambae sio wakulima ndio mnataka hivyo ila sisi wakulima hapana
Kwa nini iwe sawa kumlinda mkulima, lakini isiwe sawa kumlinda mlaji?

Kama unasema mkulima amelima mazao yake na anayo haki ya kumuuzia yeyote anaemtaka iwe ndani au nje, kwa nini mlaji asiwe na haki ya kununua kwa yeyote anaemtaka iwe hapa ndani au nje?

Haiwezekani tuu kumlinda mkulima kwa kumuumiza mpaji, nafikiri lazima kuwe na balance katika hili
 
Wakulima yaani peasants ni 70% vs 30% ya nyie walafi wa Sokoni, wewe utachagua Kulinda yupi?

Pili Serikali inalinda wote Kwa kuhakikisha inampunguzia gharama za uzalishaji mkulima Ili bei ziwe himilivu Kwa mlaji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…