Wakumbuka nini enzi za shule ya msingi?

Wakumbuka nini enzi za shule ya msingi?

Kila siku mapumziko kumikuwa na jamaa anauza gubiti. Wakitoa hela wengi naingiza mkono nachomoa.

Siku moja akaniona akanikimbiza akanikamata bwana.

Alinipiga mtama nikaangukia kisogo huku shule nzima inaona. Toka siku hiyo nikaacha wizi wa gubiti.

Sijui gubiti zikipotelea wapi.
 
Umenikumbusha nilivyokuwa mwoga wa kinyonga, hadi leo namwogopa kinyonga.

Siku moja nacheza peke yangu mbele ya kichaka najipikilisha. Ghafla nikaona kinyonga yuko kwenye tawi mbele ya uso wangu. Nikakimbia mbio kuelekea nyumbani napiga kelele.

Wakati nakimbia nikakanyaga spongi, mimi nikajua nimekanyaga kinyonga mwingine, sasa nikapiga kelele zaidi.

Ilikuwa balaa.

Daaah... nakumbuka nilikuwa nikinunua kachori nakimbia kwenda kujificha kwenye Korongo. ili wenzangu wasiniombe.. siku moja nilikimbilia kule kumbe sikujua kulikuwa na madondola ya linipiga sindano za uso , Aise niliumuka sasa kama maandazi yaliyowekwa Amira

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila siku mapumziko kumikuwa na jamaa anauza gubiti. Wakitoa hela wengi naingiza mkono nachomoa.

Siku moja akaniona akanikimbiza akanikamata bwana.

Alinipiga mtama nikaangukia kisogo huku shule nzima inaona. Toka siku hiyo nikaacha wizi wa gubiti.

Sijui gubiti zikipotelea wapi.
Gubiti ni nini?
 
Nakumbuka jinsi mechi za mpira navaa magwanda ya chipukizi ili tuokote mipira.

Bahati nzuri nilikuwa na umbo dogo hivyo nimeifanya hiyo kazi hadi standard six.

Mdogo wangu wa kike yeye naye aliokota mipira na ile mechi ya Simba na Nationa Al Ahly ya Misri pale CCM Kirumba alikuwa chipukizi.

Sasa siku hiyo yakatokea mambo mawili yaliyofanya aache kuokota mipira.

Kwanza Zamoyoni Mogela alipiga shuti lililotoka nje akaudaka ule mpira akidhani anadaka ile mipira ya naaage. Bwana ule mpira ukambabua.

Pili kaka yetu mtoto wa mjomba kesho yake akamtania "nilikuona unaokota mipira".

Toka siku hiyo akaacha.
 
Dah last seen ya mwanzisha uzi ni tar 28 may 2018!! Mwaka umekata sasa hatumuoni!! But still uzi upo kwa miaka 9 sasa
 
Binafsi nimesoma Shule ya msingi Jamhuri mjini Moshi, nilikuwa naishi Police line.Mambo nayoyakumbuka nilipokuwa nasoma Primary:
1.Kupigana siku ya kufunga shule.
2.Kutoroka darasani kwa kupitia dirishani Mwl wa Hisabati anapofundisha.
3.Kwenda Uzunguni kuangua maembe na kuchuma zambarau.
4.Kutoka Police line hadi Kwa Fonga TPC kuchukua miwa.
5.Kwenda CCP na karandinga la Polisi kuangalia michezo mbalimbali iliyokuwa inajumuisha Polisi wa Mikoa yote Bara na Visiwani.
6.Nawakumbuka baadhi ya wachezaji wa Polisi waliokuwa na mashuti makali kama Mohamed Ndutu,Brown Mwaitegete, Pius aliyekuwa Kikosi cha Kutuliza Ghasia na wengine wengi.
6.Kutoroka darasani kwenda kusaka kware.
7.Mechi ya mpira kati watoto wa Police line na wale watoto wa ng'ambo Police Dog Section, kila tukicheza nao lazima tuwafunge na ngumi lazima zipigwe.
8.Kushindanishwa shule kitaaluma Korongoni, Muungano,Mwenge, Jamhuri na Mawenzi, shule yetu kila tukishindanishwa tunakamata nafasi ya pili, licha ya kuwa na watoto watukutu wa line.
Wewe unakumbuka nini enzi ukisoma Primary?
 
wafanya fujo iwe 10 bora,5,3 au 1 nilikua sikosi,sikupenda kabisa kunyimwa uhuru wa kuongea,kama hawakutaka niongee ilitakiwa mwalimu awepo darasani
 
Mkuu hiyo tumeifanya sana ya kuchungulia sehemu nyeti za wasichana kwa kuweka chini kipande cha kioo.
 
Bakora za mwalimu kijaji, alois na chakusaga mpiga tarumbeta.
siku Za zamu zao zikifika kama umechelewa bora urudi ukalale
 
Binafsi nimesoma Shule ya msingi Jamhuri mjini Moshi, nilikuwa naishi Police line.Mambo nayoyakumbuka nilipokuwa nasoma Primary:
1.Kupigana siku ya kufunga shule.
2.Kutoroka darasani kwa kupitia dirishani Mwl wa Hisabati anapofundisha.
3.Kwenda Uzunguni kuangua maembe na kuchuma zambarau.
4.Kutoka Police line hadi Kwa Fonga TPC kuchukua miwa.
5.Kwenda CCP na karandinga la Polisi kuangalia michezo mbalimbali iliyokuwa inajumuisha Polisi wa Mikoa yote Bara na Visiwani.
6.Nawakumbuka baadhi ya wachezaji wa Polisi waliokuwa na mashuti makali kama Mohamed Ndutu,Brown Mwaitegete, Pius aliyekuwa Kikosi cha Kutuliza Ghasia na wengine wengi.
6.Kutoroka darasani kwenda kusaka kware.
7.Mechi ya mpira kati watoto wa Police line na wale watoto wa ng'ambo Police Dog Section, kila tukicheza nao lazima tuwafunge na ngumi lazima zipigwe.
8.Kushindanishwa shule kitaaluma Korongoni, Muungano,Mwenge, Jamhuri na Mawenzi, shule yetu kila tukishindanishwa tunakamata nafasi ya pili, licha ya kuwa na watoto watukutu wa line.
Wewe unakumbuka nini enzi ukisoma Primary?
Madam Salome Haule kama upo humu jf mm ni mwanafunzi wako,ulihama shule ile (huko simiyu) baada ya sisi kumaliza,ninakumbuka mambo mengi ulinitendea mazuri na yaliyofungua njia ya mafanikio yangu,nimejitahd sana kukutafta kwny mitandao ya kijamii sijafanikiwa kukupata,Tafadhali sana madam,mm mwanafunzi wako nakutafta sana japo niseme asante kwako,nafsi inanilazmisha nihtaj kuonana naww ila nashindwa sabab sjui nianzie wapi,please ukisoma ujumbe huu jua mwanafunzi wako BUFFET anakutafta sana
 
Mwalimu Kimbengele wa somo la hisabati pale Naura Primary school alikuwa na tabia ya kumuita mwanafunzi mbele ya darasa na kumuambia asolve hesabu fulani, ukikosea yeye alikuwa anachapa fimbo kwenye vigimbi ilikuwa hatari tupu, huyu mwalimu alikuwa anaishi mtaa wa Bondeni pale Arusha mjini na alikuwa na mtoto wake anaitwa Hamza. Sijui kama mwalimu huyu bado yuko Arusha.
 
Vita ya wanafunzi wa Nassa Ginnery na Mwagulanja, chanela hiyo.
 
Back
Top Bottom