Uchaguzi 2020 Wakurugenzi waliowaondoa Wagombea wa Upinzani kwa maelekezo ya CCM wafutwe kazi, wana ajenda yao wakiachwa wataleta machafuko

Uchaguzi 2020 Wakurugenzi waliowaondoa Wagombea wa Upinzani kwa maelekezo ya CCM wafutwe kazi, wana ajenda yao wakiachwa wataleta machafuko

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Baada ya Tume ya Uchaguzi kuthibitisha kwamba haikuwa sahihi kuwaengua Wagombea wa Upinzani kama ilivyofanywa na Wasimamizi wa uchaguzi ambao ni wanachama wa CCM, kuna haja ya kuwaondoa kabisa wakurugenzi hao kwenye usimamizi wa uchaguzi huu ili kuepusha maafa.

Hawaaminiki tena na wala hata wao wenyewe hawajiamini, kwa mfano Mkurugenzi wa Ubungo Beatrice Dominic, pichani

2244685_Mkurugenzi_wa_manispaa_ya_Ubungo_Beatrice_Dominic__amekiandikia_barua_chama_cha__640_X...jpg
Hapaswi kuwa msimamizi wa uchaguzi wa eneo hilo kwa vile anazo chuki binafsi na Mstahiki Meya wa Zamani wa Manispaa hiyo ambaye pia ni mgombea ubunge wa CHADEMA wa Jimbo la Ubungo, mama huyu akiachwa ataleta machafuko ambayo hayatakuja kukoma, aondolewe mapema msije kusema hatukuwaambia, sambamba na huyu wakurugenzi wengine wote walioboronga waondolewe, hawaaminiki tena.
 
Magufuli anaposema hawezi kulisha chakula watoto wa baba mwingine, akimaanisha kupeleka maendeleo sehemu walizochagua upinzani. Hivi hiki chakula cha kuwalisha watoto wake anakipata wapi?
 
Katika ile misingi ya maendeleo TANU amabyoeninafikiri ndiyo misingi ya CCM:
Watu
Ardhi
Elimu
Siasa safi
Na uongozi bora
Magufuli ana tick kwenye mangapi katika haya?
Ilishatupiliwa mbali kwenye ghala la sahau
 
Magufuli anaposema hawezi kulisha chakula watoto wa baba mwingine, akimaanisha kupeleka maendeleo sehemu walizochagua upinzani. Hivi hiki chakula cha kuwalisha watoto wake anakipata wapi?
Haya ni maneno ya kijinga kabisa yanayovunja katiba.

Yawezekana yanatokana na mihemko ya kisiasa ama kwa kujua au kutojua.

Hata hivyo, siasa zinafanywa kipuuzi kwa kuwa wananchi wanapenda na kushabikia upuuzi.

Hoja zenye ukweli, ustaarabu na hekima haziwavutii wengi.
 
Magufuli anaposema hawezi kulisha chakula watoto wa baba mwingine, akimaanisha kupeleka maendeleo sehemu walizochagua upinzani. Hivi hiki chakula cha kuwalisha watoto wake anakipata wapi?
Ulevi wa madaraka wana ccm wapo chini ya robo na tunapambana pamoja kusongesha taifa, kuna siku atawaomba radhi Watanzania kwa kauli za kibaguzi.
 
Humu Niliandika Makala ALIYOYASEMA John Magalle Shibuda Katika Lile Kongamano La Dodoma.

Pamoja na Kuwa Ndg.Zangu CHADEMA,Hamumuamini Shibuda bado MWANADAMU hupimwa kwa MANENO YAKE ANENAYO na pia matendo.

Taifa Letu Litabaki Dahari.
Tuna Wajibu Wa Kuwajengea Vyema VITUKUU VIJAVYO.
 
Magufuli anaposema hawezi kulisha chakula watoto wa baba mwingine, akimaanisha kupeleka maendeleo sehemu walizochagua upinzani. Hivi hiki chakula cha kuwalisha watoto wake anakipata wapi?
Jamaa anajishushia heshima.. Namupnea huruma kwakweli kuna msemo unasema "mwenye kulitafuta ni mwenye kulipata"
 
Baada ya Tume ya Uchaguzi kuthibitisha kwamba haikuwa sahihi kuwaengua Wagombea wa upinzani kama ilivyofanywa na Wasimamizi wa uchaguzi ambao ni wanachama wa CCM, kuna haja ya kuwaondoa kabisa wakurugenzi hao kwenye usimamizi wa uchaguzi huu ili kuepusha maafa...
Wafutwe na nani?!
 
Naunga mkono hoja, majimbo yote waliowafuta wagombea wa upinzani nao wasimamishwe kazi au wafutwe ,chadema itoe tamko kwamba hao wakurungenzi wa hayo maeneno hatuwaamini tena ,haiwezekani upinzani tu kuenguliwa, wakiachwa wataendelea hivo hivo
 
Hivi kwanini wakurugenzi kama hawa wasichapwe wakashikishwa adabu.
 
Back
Top Bottom